Kwa unyanyasaji huu wa walimu elimu itaboreka kweli tanzania?

Kwa unyanyasaji huu wa walimu elimu itaboreka kweli tanzania?

Mkulia

JF-Expert Member
Joined
Apr 26, 2012
Posts
375
Reaction score
95
Imekuwa ni jambo la kawaida kwa walimu kunyanyaswa kwa namna mbalimbali hapa nchini. TAZAMA HII:
Mimi ni mwalimu ninayefundisha katika shule ya msingi katika halmashauri ya wilaya ya Masasi. Nimepata tatizo la kifamilia ambalo kwa namna moja ama nyingine linaweza kuathiri utendaji wangu wa kazi za kila siku. Nikaamua kwenda kwa afisa elimu wilaya(DEO) ili anisaidie kwani jambo lenyewe lipo chini ya uwezo wake. Cha kushangaza,ile naingia tu ofisini na kutoa utangulizi wa kile kilichonipeleka pale,DEO alikataa kunisikiliza kisha akaondoka na kuniacha nikiwa nimekaa pale ofisini kwake. Katika hali hii tunategemea nini katika elimu ya nchi hii? Ni mwalimu gani atafanya kazi kwa moyo katika unyanyasaji kama huu? NIMEUMIA SANA!!!!!!
 
Pole sana! Ama kweli inasikitisha, cha kufanya we vumilia. Ila fanya kazi kwa muda flani, miaka miwili au mitatu alafu ukasome. Anakunyanyasa kwasababu elimu yako ndogo, ila nina wasiwasi na elimu yake pia, amekosa utu kabisa. Siku ukienda na MA au PhD ndo atakuheshimu. Pole sana mkubwa.
 
Pole sana! Ama kweli inasikitisha, cha kufanya we vumilia. Ila fanya kazi kwa muda flani, miaka miwili au mitatu alafu ukasome. Anakunyanyasa kwasababu elimu yako ndogo, ila nina wasiwasi na elimu yake pia, amekosa utu kabisa. Siku ukienda na MA au PhD ndo atakuheshimu. Pole sana mkubwa.

Ahsante sana kwa hilo. Elimu yangu kwa sasa ni SHAHADA (BAED) labda nikasome hiyo MA lakini sidhani kuwa ndio utakuwa mwisho wa manyanyaso haya.
 
Komaa naye!!! Usikubali kuachia ngazi. Kama unaamini anayo suluhu, pia, ikiwa kama unaweza kwenda hata kila siku, nakushauri uende. Watawala wa nchi hawaendi bila ya shinikizo.
Kwenda kusoma si suluhu. Nasema hivyo kwa kuwa hata Maprofesa wanavilio kila kona. Muda si mrefu Maprofesa wataandamana.
 
naona suppression za kimyakimya zimeanza kwa waalimu mara huyu kapigwa risasi mara hawa eti na rushwa ya500 ..tusubiri
 
Pole sana! Ama kweli inasikitisha, cha kufanya we vumilia. Ila fanya kazi kwa muda flani, miaka miwili au mitatu alafu ukasome. Anakunyanyasa kwasababu elimu yako ndogo, ila nina wasiwasi na elimu yake pia, amekosa utu kabisa. Siku ukienda na MA au PhD ndo atakuheshimu. Pole sana mkubwa.

DEO mwenyewe wanalingana elimu
 
Back
Top Bottom