The Phylosopher
JF-Expert Member
- Mar 11, 2015
- 1,968
- 2,957
Hii hali ya kujidanganya kwamba Tanzania tuna mfumo wa vyama vingi kunatupotezea muda wa kupata demokrasia halisi ya vyama vingi, mimi nishauri hivi vyama vilivyopo vingekubaliana kuweka mpira kwapani ili dunia nzima ijue kuwa serikali ya Tanzania haina nia ya kuruhusu upinzani.
Kuna namna nyingi ambayo serikali yetu inatamani kuidanganya dunia kuwa nchini kwetu kuna demokrasia ya vyama vingi wakati sio kweli hata kidogo.
Yaani kwa mwenye akili yeyote anajua kuwa chama tawala kinahodhi kila kitu, yaani kama ni nyama basi ccm wanafaidi minofu yote kisha wapinzani wanaachiwa vimchuzi na mifupa ili kuidanganya dunia kuwa eti kuna usawa mbele ya bakuli la supu.
Kuna namna nyingi ambayo serikali yetu inatamani kuidanganya dunia kuwa nchini kwetu kuna demokrasia ya vyama vingi wakati sio kweli hata kidogo.
Yaani kwa mwenye akili yeyote anajua kuwa chama tawala kinahodhi kila kitu, yaani kama ni nyama basi ccm wanafaidi minofu yote kisha wapinzani wanaachiwa vimchuzi na mifupa ili kuidanganya dunia kuwa eti kuna usawa mbele ya bakuli la supu.