Kwa uwekezaji aliofanya shetani kwenye muziki, suala la Diddy sio la kukushtua kama tayari unajua kuwa muziki ni haramu

Kwa uwekezaji aliofanya shetani kwenye muziki, suala la Diddy sio la kukushtua kama tayari unajua kuwa muziki ni haramu

MamaSamia2025

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2012
Posts
14,588
Reaction score
32,361
Nimepokea messages nyingi sana toka kwa wanaJF wengi kutaka kujua maoni yangu kuhusu suala la Diddy kwasababu mimi ni shabiki mkubwa wa muziki wa Hiphop na mtu mwenye akili mingi. Nilikuwa sitaki kuongelea hili jambo ila nimeona niongelee muziki kwa ujumla jinsi ulivyo katika ulimwengu wa leo. Ingawa sijaona uzi wa Lucas Mwashambwa akizungumzia hizi ishu ila watu wengi wameandika mitandaoni ikiwemo JF.

Muziki sio jambo baya kwasababu hata kwa sisi wakristo tumeona muziki ukitajwa kwenye biblia. Mfalme Daudi alikuwa mwanamuziki professional mwenye kipaji. Tatizo ni kuwa shetani naye kama kiumbe smart sana huwa anawekeza kwenye mambo yanayopendwa na binadamu ili kupata wafuasi wengi. Muziki na mavazi ni mambo ambayo shetani kafanya uwekezaji mkubwa mno unaomletea mafanikio kila kukicha. Tuhuma alizo nazo Diddy sio za bahati mbaya. Zimeanzia kwenye muziki hadi kwenye mambo hizo tuhuma.

Miziki ya aina zote hadi huu wa injili una mkono wa shetani. Angalia idadi ya ndoa za wanamuziki wa injili zilizovunjika baada ya kuingia kwenye muziki utapata jibu sahihi. Hata kwenye kundi ninalolipenda la Zabron Singers kuna kashfa mbaya ya binti kujiengua kwenye kundi kisa kikitajwa ni kukosana na hawara yake aliye naye kundini. Yaani ushenzi mtupu. Kwenye kwaya makanisani nako kuna kashfa za watu kupelekeana moto. Yaani muziki kwa ujumla una ushetani ndani yake.

Ikumbukwe muziki ndo kazi ya halali yenye pesa nyingi zaidi kwahiyo ni ngumu mno kwa wanamuziki kukwepa mitego ya shetani aliyoiweka kwenye muziki. Kuhusu Diddy tusubiri hukumu ya mahakama. Kwa sasa hana hatia hadi mahakama itakapothibitisha tuhuma zake.
 
Mimi nimejikita zaidi kwenye Siasa ambayo ndio ipo Damuni mwangu. Hata ukiniamsha usingizini ukasema nikutajie mambo mengi na mazuri aliyoyafanya Rais Samia.naweza kukutajia yote mpaka ukabakia unabubujikwa na machozi ya furaha utafikiri umemwagiwa pilipili kichaa machoni
 
وَمِنَ النَّاسِ مَن يَشْتَرِي لَهْوَ الْحَدِيثِ لِيُضِلَّ عَن سَبِيلِ اللَّـهِ بِغَيْرِ عِلْمٍ وَيَتَّخِذَهَا هُزُوًا ۚ أُولَـٰئِكَ لَهُمْ عَذَابٌ مُّهِينٌ ﴿٦﴾

6. Na miongoni mwa watu, yuko ambaye hununua maneno ya upuuzi(mziki) ili apoteze (watu) Kuiacha Njia ya Allaah bila ilimu, na huzichukulia (Aayaat) mzaha. Hao watapata adhabu ya kudhalilisha.[2]
وَإِذَا تُتْلَىٰ عَلَيْهِ آيَاتُنَا وَلَّىٰ مُسْتَكْبِرًا كَأَن لَّمْ يَسْمَعْهَا كَأَنَّ فِي أُذُنَيْهِ وَقْرًا ۖ فَبَشِّرْهُ بِعَذَابٍ أَلِيمٍ ﴿٧﴾

7. Na anaposomewa Aayaat Zetu, hugeuka huku akitakabari kama kwamba hazisikii, kama kwamba kuna uziwi masikioni mwake. Basi mbashirie adhabu iumizayo

Suurat Luqmaan
 
Shetani kwa kusingiziwa, kibaya zaidi mwenyewe hajibu shutuma
 
Ulivyojitaja una akili nikaanza kukuonea huruma.
Nb hakuna mtu mwenye akili aliyewahi kujisifu ana akili mingi kama wewe ulivyosema
 
Back
Top Bottom