Kwa wadau wa tiba mbadala fuateni maelekezo yasiwapate haya

Kwa wadau wa tiba mbadala fuateni maelekezo yasiwapate haya

Kyenju

JF-Expert Member
Joined
Jun 16, 2012
Posts
4,632
Reaction score
1,773
Juzi lafiki yangu alitumia tiba mbadala ili kutibu matatizo ya tumbo, baadaye kilichompata ilibidi tumkimbizie hospitalini.

Rafiki yangu huyo alitumia juice ya ukwaju ambapo alichanganya kiasi fulani cha ukwaju kwenye maji lita moja, nilimuuliza nani alimfundisha hii tiba akaniambia amejifunza kutoka kwa dr. bingwa wa tiba mbadala kupitia star TV.

Nilipo muuliza kuhusu ratio yaani mchanganyo anachanganya na ukwaju kiasi gani aliniambia kuwa kiasi cha ukwaju hakumbuki ila anakumbuka maji ni lita moja, dakika kama 20 baada ya kunywa juice ile alianza kukosa nguvu miguu ikalegea, akatokwa na jasho jingi mwili mzima ikabidi apelekwe chumba cha mapumziko maana tulikuwa kazini.

Jioni alirudishwa nyumbani lakini usiku hali ilikuwa mbaya maana alialisha sana kiasi cha kutokea hali fulani ya damu damu, kesho yake yaani jana ilibidi tumpeleke hospitali kwasasa amelazwa hospitali yuko kwenye dose.

Dr. alisema kuwa tatizo ni ukwaju ulikuwa mwingi sana kuliko maji ambapo umetengeneza acid tumboni.
 
Tatizo ni ndugu yako wala tatizo sio tiba mbadala,yeye alishindwa kukumbuka ratio ya tiba yeye akaendelea kujitengenezea bila kipimo chochote,kosa la daktari wa tiba mbadala au ukwaju ni lipi hapo ? amekurupuka kujitengenezea dozi na kujinywea yamemkuta anatafuta mchawi wakati ni yeye mwenyewe. Umekurupuka
 
Sijasema dr. wa tiba mbadala amekosea wala ukwaju una tatizo, na ndiyo maana kwenye title nimesema kama utatumia fuata maelekezo ya dr.
 
Sijasema dr. wa tiba mbadala amekosea wala ukwaju una tatizo, na ndiyo maana kwenye title nimesema kama utatumia fuata maelekezo ya dr.
Mkuu Kyenju Kwa hiyo Ukwaju ndio uliomdhuru? kwanini

hakutumia kwa kpimo Dozi Maalumu? yeye kaamuwa kuweka anavyojuwa yeye mwenyewe? kila kitu kina kipimo chake

hata dawa za hospitali ukinywa pasipo an Ushauri wa Daktari unaweza hata kufa itakuwa Dawa za Kienyeji? angeliweka

ukwaju kwa kipimo chake wala usingeweza kumdhuru kazidisha kipimo ndio umemdhuru mpe pole sana.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom