Kwa waliobobea kwenye lugha msaada kwa hili

Kwa waliobobea kwenye lugha msaada kwa hili

Babarita

JF-Expert Member
Joined
Dec 14, 2011
Posts
386
Reaction score
126
Wana jamvi tusaidiane LUGHA MAMA(lugha ya kikabila) inaathiri vipi maendeleo ya mwanafunzi kujifunza?
 
Babarita Swali lako haliko wazi; kujifunza nini? Lugha nyingine mf. Kiingereza, au kujifunza masomo mengine lakini yanayofunzwa kwa kutumia lugha tofauti na ya mama?
 
Babarita Swali lako haliko wazi; kujifunza nini? Lugha nyingine mf. Kiingereza, au kujifunza masomo mengine lakini yanayofunzwa kwa kutumia lugha tofauti na ya mama?
Kujifunza masomo mf.Lugha mama ya mwanafunzi ni kihaya alafu darasani mwalimu anatumia kiswahili kufundishia
 
Wana jamvi tusaidiane LUGHA MAMA(lugha ya kikabila) inaathiri vipi maendeleo ya mwanafunzi kujifunza?
Sijabobea katika lugha ila nahisi naweza kukusaidia. Ni hivi Babarita,lugha mama ni lugha ambayo mtu amekua akiiongea na hivyo kujikusanyia misamiati mingi ya lugha hiyo,sasa linapokuja swala la kujifunza kwa mtu ambaye amekuwa akitumia lugha mama tu kwa mawasiliano,na akatakiwa ajifunze kwa lugha tofauti hapo inakuwa ngumu kwa sababu mtu huyo hana misamiati ya kutosha ya ile lugha nyingine na hivyo kujikuta akishindwa kuelewa baadhi ya mambo katika kujifunza kwa sababu ya upungufu wa misamiati wa lugha ya kujifunzia.
 
Sijabobea katika lugha ila nahisi naweza kukusaidia. Ni hivi Babarita,lugha mama ni lugha ambayo mtu amekua akiiongea na hivyo kujikusanyia misamiati mingi ya lugha hiyo,sasa linapokuja swala la kujifunza kwa mtu ambaye amekuwa akitumia lugha mama tu kwa mawasiliano,na akatakiwa ajifunze kwa lugha tofauti hapo inakuwa ngumu kwa sababu mtu huyo hana misamiati ya kutosha ya ile lugha nyingine na hivyo kujikuta akishindwa kuelewa baadhi ya mambo katika kujifunza kwa sababu ya upungufu wa misamiati wa lugha ya kujifunzia.
Mdau asante kwa majibu mazuri. Blue G, je kuna athari nyingine kijamii mwanafunzi atazopata?
 
Last edited by a moderator:
Mdau asante kwa majibu mazuri. Blue G, je kuna athari nyingine kijamii mwanafunzi atazopata?
Ndio kijamii pia zipo.kwa mfano ikiwa alizoelea kukaa katika jamii iliyo na watu wanaozungumza lughamama kama yake hatopata athari zozote hasa za mawasiliano.Lakini pindi ikitokea amelazimka kuhamia ene jingine ambapo watu hawzungumzi lugha mama kama yake,kijamii atapata athari kwani atashindwa kuwasiliana na wengine,mpaka kipindi fulani cha wakati kipite.sijui umenielewa Babarita?
 
Last edited by a moderator:
Ndio kijamii pia zipo.kwa mfano ikiwa alizoelea kukaa katika jamii iliyo na watu wanaozungumza lughamama kama yake hatopata athari zozote hasa za mawasiliano.Lakini pindi ikitokea amelazimka kuhamia ene jingine ambapo watu hawzungumzi lugha mama kama yake,kijamii atapata athari kwani atashindwa kuwasiliana na wengine,mpaka kipindi fulani cha wakati kipite.sijui umenielewa Babarita?
Nimekuelewa mkuu.Rejea kwenye athari za kimasomo alafu onesha uhalisia kwenye jamii za kitanzania
 
lugha mama humuathiri mtu anayetaka kujifunza lugha nyingine katika
matamshi, na sarufi yani (grammar) hapa ndio utaona mtu anahangaika kubadilisha tensi ya kiswahili kwenda kingereza
mfano mzungumzaji wa kiswahili kama lugha mama akitaka kuuliza kingereeza are you calling me? atasema you are calling me eehhh? hii ni athari ya sarufi ya lugha yake mama
haya ndio matatizo makubwa ya lugha mama katika kujifunza lugha nyingine.
 
lugha mama humuathiri mtu anayetaka kujifunza lugha nyingine katika
matamshi, na sarufi yani (grammar) hapa ndio utaona mtu anahangaika kubadilisha tensi ya kiswahili kwenda kingereza
mfano mzungumzaji wa kiswahili kama lugha mama akitaka kuuliza kingereeza are you calling me? atasema you are calling me eehhh? hii ni athari ya sarufi ya lugha yake mama
haya ndio matatizo makubwa ya lugha mama katika kujifunza lugha nyingine.

To do you do you......to say you say me lol
 
Nakubaliana na wachangiaji wa mwanzo ni kweli lugha mama huathiri sana katika kujifunza na hasa katika uelewa wa mambo, na athari hii tunaiona sasa kwa wanafunzi wetu wanapoingia shule ya upili wakitokea shule ya msingi! kule chini masomo karibu yote isipokuwa kiingereza tu, hufundishwa kwa lugha ya kiswahili, wanapofika shule ya upili mara ghafla masomo yote hufundishwa kwa kiingereza isipokuwa kiswahili tu! hapo ndio uelewa wa wanafunzi unaanza kudumaa, maana wote walimu na wanafunzi hawana misamiati tosha ya kuelezea kile wanachosoma na kusomeshwa! Nilipokuwa shule ya msingi mjini Mwanza, maeneo ya Nyakato ( siku hizi ni wilaya ya Ilemela), siku moja tulikuwa darasani wakati huo niko darasa la Tatu! mwalimu wa somo la kiswahili alimtaka mwanafunzi mmoja atunge sentensi kuhusiana na neno"Tango"; yule mwanafunzi alisimama na kusema" jana usiku nilikuwa wali na matango ya kuku" wengi mule darasani walicheka sana, mimi sikuelewa alimaanisha nini, ila baadae nilipouliza niliambiwa neno matango kwa lugha ya kisukuma lina maanisha mapaja! so yule mwanafunzi alikuwa na maana ya kusema jana usiku alikuwa wali na mapaja ya kuku!
 
Back
Top Bottom