Kwa waliofiwa na baba zao njooni hapa tufarijiane

Kwa waliofiwa na baba zao njooni hapa tufarijiane

Jocasta

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2014
Posts
474
Reaction score
595
Mwaka jana mwezi wa nane baba aliniita nyumbani akaniomba nimununulie chupa kwaajili ya kuwekea chai (japo ilikuwepo).

Pia akaniomba kabla ya kuondoka nimununulie redio, alifurahi sana kufanya alichoniagiza.

Sikujua ya kwamba kumbe hivyo vitu viwili nilivyomnunulia ndiyo vya mwisho kabisa kabla ya kutamatisha maisha yake duniani.

Mwezi wa kumi na mbili wakati nikiwa ziara ya kikazi Mbeya, nilipigiwa simu na mama akiwa analia kwa uchungu na akanisihi niende nyumbani haraka sana.

24/12 nikifika nyumbani nikashangaaa kumuona baba yangu akiwa kwenye wakati mgumu sana. Siku iliyofuata aliaga Dunia.

Nililia sana tena sana, hadi mda huuu huwa nalia. Baba wa Mbinguni toa faraja kwa watu wako waliopoteza wapendwa wao.
 
Mi naona hapa hatufarijiani bali tunakumbushana majonzi. Umenifanya nitokwe na machozi asubuhi hii baada ya kumkumbuka mzee wangu mpendwa ah. His love to his children and as the first born was unconditional, may his soul continue resting in peace mzee wangu.
 
Mwaka jana mwezi wa nane baba aliniita nyumbani akaniomba nimununulie chupa kwaajili ya kuwekea chai (japo ilikuwepo)...

Nilienda kumuona siku ya Jumamosi almost kilometres 400 tangu nilikokuwa, baada ya kumuona sikulala nikageuza ila wakati tunaagana akasema tutaonana kesho kutwa! SIKUMUELEWA!

Alfajiri ya kuamkia siku ya tatu napata simu ya kifo chake[emoji24]

giphy.gif
 
Au basi, pumzika kwa amani Mzee Swai. Umenifundisha na kunikuza katika miiko na maadili ya mwanaume wa kimachame. Do and don't zilikuwa nyingi sana.

Sasa naishi na mataifa huku nyanda za juu kusini. Tutaonana katika pambazuko lile. Naamini tutakuwa pamoja katika ibada ya patakatifu pale kisha kushiriki katika harusi ya mwana kondoo.
 
Poleni sana, wapendwa,nimelia mnooo,mpaka Sasa nalia sijui ntafanyaje ili niweze kusahau,
Mpaka Sasa naliona hili kwangu nizito,mzigo huu umekuwa mzito Sana kwangu,

Mpaka Sasa natamani kusahau,Ni mwaka Sasa unaelekea kuisha japo nashindwa
 
Hapa tunatiana simanzi tu ila mzee wangu alikuwa jembe sana,laiti ningepewa hata robo ya akili zake ningetisha sana duniani.

Baada ya mzee kufariki nikaea napekuwa nyataka zake ndio nikagundua hakuwa mtu wa kawaida alikuwa na akili nyingi mithili ya robot au komputer
 
Poleni sana,wengine hapa baba zetu wamekufa hatuwakumbuki sura,japo naambiwa nilizika ila sikumbuki kitu.Nasikia tu alifia mikononi mwa hawara....lakini hawara nae hakumaliza mwaka eti nae akafa....walipata mtoto mmoja na hawara..mtoto wa kiume...huyo nae kanitafuta mwaka majuzi(2020) ndo tukafahamiana tukiwa wote na familia zetu
 
Hapa kila mtu atamsifia baba yake kumbe wengine baba zao walifia mtaroni wakiwa wamelewa acheni kulia kwenye mipango ya mungu.

Mimi baba yangu alifariki 2005 nikiwa masoma a level niliumia kwa kipindi kile ila alishanifunza kubeba kila jambo hivyo nikabaki na ndugu zangu tukiwa na umoja na tulijua ni mpango wa mungu yeye kutuacha kwa muda ule.

#Kazi yake mola haina makosa ukilia unajitesa tu
 
Hapa kila mtu atamsifia baba yake kumbe wengine baba zao walifia mtaroni wakiwa wamelewa acheni kulia kwenye mipango ya mungu.

Mimi baba yangu alifariki 2005 nikiwa masoma a level niliumia kwa kipindi kile ila alishanifunza kubeba kila jambo hivyo nikabaki na ndugu zangu tukiwa na umoja na tulijua ni mpango wa mungu yeye kutuacha kwa muda ule.

#Kazi yake mola haina makosa ukilia unajitesa tu
Na wote njia yetu moja
 
1997
Nikiwa std 1, Major Ruzige alituacha. Kwa kweli kuna kipindi huwa natamani hata nione simu yake.

2012
Mwl. Catherine ,(Mama) nikiwa chuo 3rd Year nae anatuacha. Hii ndio ilinitesa kwa miaka kadhaa. Sikuwahi kuamin kama mama alifariki na mpaka niliamua kutofanya graduation ya kupata bachelor mana sikuona umuhimu Wake ilhali aliefight mpaka nikifika hapo hakuwepo tena

Ila yote kwa yote ni mipango ya Mungu
Kuondokewa na Wazazi inauma sana
 
Poleni sana, wapendwa,nimelia mnooo,mpaka Sasa nalia sijui ntafanyaje ili niweze kusahau,
Mpaka Sasa naliona hili kwangu nizito,mzigo huu umekuwa mzito Sana kwangu,

Mpaka Sasa natamani kusahau,Ni mwaka Sasa unaelekea kuisha japo nashindwa
Pole sana, Mungu akuvushe.

Ili usiumie sana ni lazima uchukulie huo msiba in a position way.
Kwamba,Baba ameondoka na yupo mahali salama anapumzika.
Huenda angekuwepo pengine angepatwa na majanga,au pengine ingepelekea na nyie kuingia huko.
Mipango ya Mungu si mipango yetu,,,Yeye anafahamu yote.


We have our biology parents for a while,But God is our Father for the rest of our lives.
Baba mzazi hayupo,kazi yake ameimaliza
Ila kumbuka Mungu amesema yeye ni Baba..na Yeye yupo siku zote.
Wewe si yatima maana una Baba ambaye ni Mungu.

Sent from my TECNO CG6 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom