Kwa wanaoamini kila kifo ni kwa sababu ya CORONA msikikilizeni Baba Askofu Kasala

Kwa wanaoamini kila kifo ni kwa sababu ya CORONA msikikilizeni Baba Askofu Kasala

comte

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2011
Posts
9,019
Reaction score
6,825
“Walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakayokula matunda ya mti huo utakufa hakika.” (Mwa.2:17).
Shetani alidai “Hakika hamtakufa.” (Mwa. 3:4).
Lakini baada ya kutokutii, Adamu na Hawa waligundua kuwa mshahara wa dhambi kwa uhalisi ni “mauti” (Rum.6:23).
Hukumu yao ilibeba maneno haya:

“kwa jasho la uso wako utakula chakula, hata utakapoirudia ardhi, ambayo katika hiyo ulitwaliwa; kwa maana u mavumbi wewe, nawe mavumbini utarudi.”(Mwa.3:19)

-----
Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Geita, Fravian Kasala amesema watu wanatakiwa kutokuwa na wasiwasi kuhusu kifo na kinapotokea watambue kuwa ni mpango wa Mungu.

Ametoa kauli hiyo leo Jumamosi Februari 6, 2021 katika ibada ya mazishi ya aliyekuwa katibu tawala wa Mkoa wa Arusha, Richard Kwitega iliyofanyika kijiji cha Ngoma Wilayani Sengerema katika kanisa la Mtakatifu Benerdicto.

Amesema kifo cha Kwitega ni mwanzo mpya wa maisha yake mbinguni, “tunapaswa kumwombea na tuyaenzi yote aliyofanya hapa dunia kwa kuwa ameacha alama isiyofutika katika utumishi wake wa umma.”

"Tusali kila siku hatujui siku wala saa ya kuondoka hapa duniani. Maombolezo haya ya leo yasiwe ya kukata tamaa, yalete tumaini jipya kwa mwanadamu. Mwanzo wa kufa ni mwanzo wa maisha mema huko mbinguni, “ amesema Askofu Kasala.

Kwitega alifariki Februari 3, 2021 katika ajali wakati akitoka Arusha kwenda Dodoma baada ya gari alilokuwa amepanda kugongana uso kwa uso na basi. Katika ajali hiyo watu wanne walijeruhiwa ambao ni dereva wake na wanawake watatu waliokuwa kwenye basi hilo.


Chanzo: Mwananchi
 
sioni namna ya kukusaidia Mkuu
Kuna kitu hakikosawa kwenye maelezo yako. Ni kama ulishindwa kumwelewa Askofu. Yeye kaongelea teolojia ya kifo wewe unaongelea korona. Kwa kifupi umemlisha maneno
 
Kuna kitu hakikosawa kwenye maelezo yako. Ni kama ulishindwa kumwelewa Askofu. Yeye kaongelea teolojia ya kifo wewe unaongelea korona. Kwa kifupi umemlisha maneno
Mkuu teolojia na mimi tunakutana kwenye kifo- NINI CHANZO CHA KIFO-NOTE PLEASE NOTE- sioengelei sababu ya kifo. Unajua kwa kila jambo kuna why na how yake. Why ya kifo inajulikana- Mungu alituadhibu binadamu- how ya kifo kila mtu anajibu lake. Kinachoshangaza sasa hivi ni hii tabia mbaya ya kuadhania kuwa kila kifo HOW yake ni CORONA
 
Mkuu teolojia na mimi tunakutana kwenye kifo- NINI CHANZO CHA KIFO-NOTE PLEASE NOTE- sioengelei sababu ya kifo. Unajua kwa kila jambo kuna why na how yake. Why ya kifo inajulikana- Mungu alituadhibu binadamu- how ya kifo kila mtu anajibu lake. Kinachoshangaza sasa hivi ni hii tabia mbaya ya kuadhania kuwa kila kifo HOW yake ni CORONA
Kwani wewe unasemaje, hakuna wanaokufa kwa Corona?
 
Kwani wewe unasemaje, hakuna wanaokufa kwa Corona?
Mkuu WAPO na hilo halina ubishi- ninalolikataa na nisilolipenda na kulazimisha kuwa Corona ndiyo imeleta vifo Tanzania kwamba zamani havikuwepo
 
Back
Top Bottom