Kwa wanaume tu; soma hapa!

Kama hujikubali hakuna atakayekukubali?
Kwani kama jamaa anampenda na anajua ana watoto wawili, yeye tatizo kaliona wapi hadi kuuliza haya??

Huoni kuna ka "inferiority" fulani hivi?

Maana huyo jamaa kaona wasichana wangapi lakini bado kaenda kwake???

Nadhani haumtendei haki nivea...
 
BAK mkuu nimekupata vizuri na nimejifunza kitu kikubwa.

Umejifunza kitu gani? Say umeachana na huyo mume wako vizuri tu, na labda anaprovide kwa hao watoto, waweza kata mawasiliano kweli? au utawazuia wanao wasiwasiliane na baba yao/zao? Na hili swali BAK linakuhusu pia.
 
Last edited by a moderator:

Sio kila mwanaume anapoenda kwa mwanamke anaenda na ukweli. Na ukimwamini kila mwanaume anayekuambia anakupenda, unaweza kuwa jamvi la wageni. Nivea anajua kabisa kuwa na mtoto/watoto kabla ya kuolewa inapunguza 'points' za kuwa wife material (najua hilo hulikubali, but ndo ukweli)
 
Anachopaswa kufahamu muuliza swali ni kuwa kupenda hakuna fomula. Waswahili wanasemaukipenda boga penda na ua lake, lakini kuna mifani mingi ya kuonyesha jinsi hilo linavyoshindikana.
Kupenda ni suala linalohusiana na feelings, hivyo ni vigumu sana kujua iwapo mtu utawapenda watoto au la kwa sababu nayo inategemea pia na hulka na tabia za watoto hao.
 
Kwa wanaume wengi hili si tatizo ali mradi tu huyo Baba wa watoto asiwepo kwenye picha, mara nyingi kama bado kuna mawasiliano naye basi varangati huweza kutokea na kuharibu amani katika mahusiano.


BAK my dear, mawasiliano yepi unategemea yasiwepo?
 
Last edited by a moderator:
Reactions: BAK

Sasa je kama huyo mwanamke ni hohehahe/kajamba nani, utaongeleaje kuhusu hilo???huyo mwanaume atakua kafata nini???
 
Kwa wanaume wengi imekuwa nadra sana kutokea hivyo nadhani kwasababu ya kuhofia zaidi "nini watu wanaonizunguka watasema" lakini ikitokea wanaume hawana shida sana juu ya hilo. Mimi binafsi kwangu haina shida pia kama ingetokea.
 

HorsePower :A S thumbs_up: :A S thumbs_up::A S thumbs_up::A S thumbs_up::A S thumbs_up:
 
Last edited by a moderator:
Lakini jamaa si kataka kukuoa pamoja na watoto wake?

Kwani wanaoumizwa kwa kudangyanywa na wanamme kuwa wanawapenda na baadae kuwaacha wote wana watoto??

 
Mie nashangaa tu, eti baba wa mtoto asiwepo kwenye picha, how??
Yaani uwakosanishe baba wa mtoto na mwanae kisa ndoa mpya?

Hapa nahitaji mtu wa kuelewesha
Umejifunza kitu gani? Say umeachana na huyo mume wako vizuri tu, na labda anaprovide kwa hao watoto, waweza kata mawasiliano kweli? au utawazuia wanao wasiwasiliane na baba yao/zao? Na hili swali BAK linakuhusu pia.
 
Siwezi bagua mke mwenye watoto kama nimempenda na ninaona ananifaa kwa hali na mali kwa ajili ya kujenga familia yenye upendo.
 
Kupenda ni kuchagua, kama huyo mwanamke nimempenda kiukweli haina shida yoyote kumuoa lakini hao watoto si wanababa yao? itabidi tu awalee.
 
bwana mzee mm nakushauri somba mali zako weka ndani usiulize mtu uliza moyo wako kaka jadiliana na bibiye kuhusu baba za hao watoto wekeni misingi imara ya mahusiano yenu asiwaingilie mtu kwenye hilo hivi kama una ulemavu wa uzazi ukaasili mtoto kisheria utakuwa umefanya kosa?
 
ndio maana siamini kwenye ndoa baada ya kuvunjika ya kwanza ni mtazamo wangu tu.

Chauro hata mimi huwa naamini zaidi hivyo, ingawa inawezatokea mmeachana mkiwa bado hamjazaa, hivyo ukaenda kuanza upya kwa mwingine.

Lakini mkiwa na watoto tayari ni risk kwa wote, siyo kwa mwanamke tu. Hata mwanaume unawezajikuta watoto wako wanateseka ile mbaya, kisa umeamua kuacha mama yao na kuoa mwanamke mwingine.
 
Sasa je kama huyo mwanamke ni hohehahe/kajamba nani, utaongeleaje kuhusu hilo???huyo mwanaume atakua kafata nini???

Unachosema Yummy ni kweli, wewe jaribu tu kuwachunguza kiundani wenzi wa jinsi hiyo utajua ninachomaanisha. Hapo nilitoa mfano mmoja tu wa mali za mjane. Lakini kama ulivyosema kuna wakati inatokea mwanaume ndo anawatoto lukuki, halafu anahitaji mama kwa aili ya kumlelea wanae. Kwa mfano tumeshuhudia harusi mwanaume ana watoto 3 na yuko safi tu kimaisha, halafu anaoa mwanamke ana mtoto 1 (huyo unayesema hohehahe) akiamini kuwa atatulia ndani kwa kuwa alishazalishwa bila kuolewa, pia atakuwa mlezi mzuri kwa wanae kuwa ana mtoto tayari.
 
Jmos iliyopita nilikuwa kwenye harusi ya dada mmoja anaolewa na ana watoto wanne
Mwanaume ni kijana kabisa nadhani 30-35 years na yeye hana mtoto.
Maswali milioni yalikuwa yanatembea kichwani kwangu...

Situation kama hiyo FirstLady1 si bure, hapo huyo kijana lazima ana zaidi ya love kichwani mwake. Hebu tujuze kidogo kuhusu profile zao financially, mali, elimu n.k
 
kama ni watoto wadogo under 7yrs naweza nikamuoa mamayao na kusetle nae.ila kuna restrictions flan flan hivi(sitaki kuwaona baba yao kwangu)
upande wa pili wa sh ni wanandugu wa mwanaume sizani kama wanaweza wakawa comfotable na huyo mwanamke.
 
Situation kama hiyo FirstLady1 si bure, hapo huyo kijana lazima ana zaidi ya love kichwani mwake. Hebu tujuze kidogo kuhusu profile zao financially, mali, elimu n.k

Nikiangalia wote wako vizuri kabisa ..mdada ni mjasiriamali na Kijana ni msomi na ana kazi yake nzuri tu..
Labda hapo kuna true love..?
 
Nikiangalia wote wako vizuri kabisa ..mdada ni mjasiriamali na Kijana ni msomi na ana kazi yake nzuri tu..
Labda hapo kuna true love..?

Mmh haya bana, may be that one is exceptional!! Let us wait and see...., but I'm very skeptical!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…