mwanaume kama hakupendi yaani hata ufanye vipi hatakupenda na atakupa shida sana ila kwa mwanamke mmejaaliwa kujifunza kupenda ndo so vumilia hata kama humpendi jifunze kumpenda na utaona matokeo yake utampenda tu mwenyewe kama unataka mateso kuwa na mwanaume ambaye hakupendi utajuta kuzaliwa.Wanaume tunanyanyasa sana kwa wanawake tusiowapendatunaowapenda wanatupelekesha kama mang'ombe na kwa
suala sio kupigiwa simu mara kwa mara,inategemea ni simu zenye sababu zipi _ maake kuna simu za kuulizwa uko wapi mara unafanya nini mara uko na nani na nyingine kama hizo ndio zinazoboa,.....
Kuna kitu kinaitwa mvuto. Yaani hata kama mtu unampenda sana usitake kumuonyesha kuwa unampenda saana na huwezi ishi bila yeye. Mjali, ongea naye vizuri, msikilize, lakini linapokuja suala hukubaliani nae, mwambie wazi wazi tena straight. Mwonyeshe kuwa uko focused zaidi na maisha, sio na yeye. Usipende kubip bip au kupiga kila saa. Sometimes akikupigia mpotezee, then unakuja kupiga masaa kadhaa baadae, unamwambia kuwa ulikuwa bize na shughuli fulani ya maana, so hukuona call yake. Au unaweza kupokea then, ukamwambia kuwa, sory, kuna kitu cha muhimu nafanya hapa, nitakupigia baadae, I love you, bye.. Ukifanya hivi utajenga mvuto fulani na kila saa atakuwa anakuona mtu wa maana na focused na maisha, na atatamani kuwa na wewe. Atakuona kama mtu ambaye uko siriaz na unaweza kutunza familia ikitokea,
Lakini kama unampenda mtu alafu kila saa unataka kuongea naye, kila saa kuwa naye, kila saa unaongelea I miss you, I love you.. atakuchoka na kukuona huna maana. Automatically atakuona cheap na low grade na atakuacha. Hapa sijamaanisha kuwa mvuto, ndo basi umchunie siku mbili au tatu hujampigia, la, ila ikibidi umpigie, au unataka kusikia sauti yake, piga alafu jifanye unaulizia jambo la muhimu. Kwa mfano piga msalimie, mwambie nimekumiss alaf mwambie nilitaka unishauri labda mtu aliyemaliza form four hajapata shule, kipi cha maana kati ya secretarial na hotel management course. Akikuuliza vipi, mwambie kuna mdogo wangu nilitaka nimtafutie chuo hapa.
Jambo jingine ni kuwa usitake kwenda kwake bila sababu. Kwa mfano mwambie kuwa kama uko hom, nitakuja mara moja kukuletea zawadi yako then nitaondoka maana nataka kwenda so and so, ukitaja hata sehemu za ukweli. Hii itamfanya akuone kuwa unamjali, alafu pia uko bize. Lakini kama unataka kumuonyesha kuwa uko bize, usijisahau ukamwonyesha uko bize na mambo yanayowashirikisha sana wanaume, bali mambo ya kijamii na kielimu. Kama wewe ni mfanya kazi mwonyeshe kuwa kazini kwako uko bize na unathaminiwa. Mwonyeshe kuwa mara nyingi una homework. Katika hali kama hiyo mwache yeye ndiyo apropose kwenda out, na usikatae, bali mwambie kuwa japo nina vijishughuli vya muhimu hapa, then nitakwenda kwa sababu nakujali wewe.
Usitake kumuonyesha kuwa unapenda starehe, bali usijionyeshe kuwa anti-social. Hata kama unapenda kujirusha, lakini siku zote onyesha kuwa unajirusha tu kwa sababu yake, na ukiwa mwenyewe au na watu wengine hauenjoy. Siku zote omba msaada wa mawazo kwake, na epuka kuomba msaada wa ela mara kwa mara. Hakikisha kuwa akikupa elfu 10, basi 2 zinarudi kwake kwa njia ya zawadi au kulipia bill. Sometimes jifanye kuwa una shida kubwa ya hela kiasi fulani, na akikupa, nenda kamnunulie zawadi, tena ikiwezekana ongeza na ya kwako, alafu unamwambia kuwa nilikuomba ile hela kwa sababu niliona hiki kitu fulani nikatamani uwe nacho lakini sikuwa na hela ya kutosha. Hii itamfanya aone kuwa unamjali.
All in all, kumpenda mtu kusimfanye akuone mzigo au kero, bali kuwa na mvuto fulani wa kutaka kukuona kila saa.
nitaendelea baadae...
....Tuko umegonga utosini....yaani ningekuwa nakufanyia interview za wasemaji kwenye makitchen parties....ungeshapita bila kupingwa mkuu.......! una uelewa mkubwa sana kwenye hili somo!Yapo mambo mawili ambayo yamejinga kwenye vichwa vya baadhi ya wanaume siku hizi. Cha kwanza wanaamini kuwa wanawake wengi wanapenda zaidi ela na starehe, na sio mapenzi. Na pia tunaona kama wanawake wengi wanapenda kuolewa tu na sio mapenzi. Jihadhari usionekane kama una hata lengo moja kati ya hayo. Onyesha kwa mwanaume kuwa unathamini sana ela na uwe unamshauri apunguze starehe. Akikutoa kwenda kula piza ya sh 30,000/= mwambie no... kwanini tusiende tu hapo mgahawani tukala chakula cha kawaida, alafu hivyo vitu vikubwa tukafanya siku maalumu tu. Kama kweli anakupenda utashangaa siku anakupeleka sehemu ya matawi ya juu kwa surprise. Kama unakunywa pombe, ukiwa nae mwangalie yeye kwanza anakunywa nini. Kama anakunywa pombe, basi usijivunge, na wewe kunywa asije akakuona mnafiki, ila kama hanywi, take care kumsoma namchukuliaje mtu anayekunywa, kama yuko neutral, then kunywa ili akuone kuwa unajiamini. Usimuachie yeye tu kulipa bill. Kama unajua mtatoka, jitahidi kupata vijisent kadhaa, na mkiwa kwenye starehe, lipia kitu chochote kimoja wapo, hata chumba (kama mtahitaji faragha). Hii itamfanya akuone kuwa unastarehe sio kwa sababu ya pesa zake, bali unapenda kustarehe.
Usipende sana kumsisitiza kuhusu ndoa. Usipende kudiscuss naye juu ya ndoa za rafiki zake au zako. Usipende kumwonyesha kuwa yeye ndiye mtarajiwa wako au wewe ndiye mtarajiwa wake. Usimtambulishe hivyo kwa ndugu au jamaa. Mtambulishe kama rafiki yako wa kiume, basi. Ukiongea naye kuhusu ndoa mwambi ... mi napenda baadaye maisha yangu ya ndoa yawe hivi na hivi.. napenda niwe na mwanaume mwenye tabia nzuri kama za kwako.. Akikuuliza kwa ni huna uhakika kuwa atakuwa yeye..., mwambie yote ni mipango ya Mungu, lakini ungefurahi sana kama akiwa yeye...
Kama unataka akununulie kitu, mwombe akusindikize shopping. Ukifika kule mwambie kuwa una shilingi kadhaa na unataka kununua kitu fulani (hata kama hizo hela alikupa yeye), then chagua kama ni nguo au chochote, jaribu, akikwambia umependeza, jifanye kuulizia bei.. then akiwa kubwa kuliko ulizo nazo, usitake kumwambia akuongezee, bali sema ok,
000
\
Umeme umekatika, UPS yangu inaisha chaji, kwa heri...
Michelle......well said too!Kuna kitu kimoja nami nimejifunza,wanaume wanakimbia wanawake walioko desperate au wenye dalili za kuwa desperate.....yaani...you are too demanding.....si in terms ya hela ila hata attention unayotoa na kutarajia kutoka kwa mwanaume.....wanapenda uhuru wao na wawe na muda wa kufanya na kuamua mambo yao....ukiwa too much available kiasi kwamba una limit freedom yake na kumuonyesha huna maisha bila uhusiano wenu inampa shida sana.....nakushauri,take your time away from him sometimes,distance ni nzuri....show him you have your own life independent without him,love yourself,have time with friends and family and just be happy and show him your happiness does not depend on him alone.....ila ukikosea ukamuonyesha yeye ndo kila kitu,safari ataianza....pia do not pressure himor try to change him to be someone,he will change when he is ready,...uwe na kiasi na mpende alivyo.... and lastly,maybe hawakuwa wako my dear....wako yu njiani na akifika utakuwa na peace of mind and the love you have always desire and deserve.....be happy,stop worrying about men....wapo tu!!!!!!!1
....Yeeap!Sijui katika pitia pitia yako ya kuwasoma wanaume ulikutana nayo haya:
Wanawake wengi huwa possessive wanapompenda mwanamme na huwa wanachukuwa roll ya kuwa dominant na kujifanya wanalinda territory yao. Hilo ni kosa kubwa walifanyalo wanawake bila kuelewa. Hii jifunze kwa kutazama wanyama wanavyoishi, kama vile Simba, Kuku, Swala na kadhalika. Mwanamme ndiye mwenye roll ya ku-possess na ku-dominate na kulinda territory yake.
Ushauri: Wasome hawa wanyama especially wale waliokuwa si wa kufuga, utapata elimu kubwa ya kuishi na umpendae bila matatizo.
Hiyo ni point moja tu na nimeikatiza katiza.
Lingine ni kujaribu kuwasiliana na wakina mama wazee waliokuwa wakiwafunda wari huko nyuma, nna uhakika utapata mengi sana ya manufaa kutoka kwao na si kupata elimu mahusiano kutoka kwa hawa waliorukia hizi kazi, kama wale wanaoongea hovyo kwenye ma-kitchen party, watakupoteza.
Kumbuka, wanaume wengi huwa wanajali sana kudekeza mwanamke iwapo nae ana manufaa kwa mwanamme na si kumfanya mwanamme ndio njia ya kipato chako. Tazama Simba, anahakikisha analinda wanawake zake na himaya (territory) yake na anahakikisha anawatimizia majike unyumba wakati wanapokuwa kwenye heat (ashki) hata mara 30 kutwa kwa wiki nzima au zaidi. Lakini, nae hutegemea kuenziwa kwa wanawake kuchukuwa roll ya kuwinda na kumwachia aanze kula vinono, japo husaidia kuwinda lakini utaona wanawake ndio wenye roll hiyo. Somo ni refu na linataka wasaa.
Mwenzenu nimekaa na kutathimini historia ya mapenzi yangu tangu nilivyoanza mahusiano ya kimapenzi, nikagundua kuwa wanaume ambo niliwapenda sana hatukuweza kudumu kwa mda mrefu, ila ambao sikuwapenda ile kiukweli ndo niliodumu nao sana na mimi ndo nilikuwa nawaacha kwa sababu sikuweza kujilazimisha kuwa nao wakati siwapendi, nikawa najiuliza maswali mengi kwa nini mwanaume ninaempenda sana ananiacha, sikupa jibu sahihi baadae nikaamua kuanza kusoma tabia za wanaume wawapo kwenye mahusiano katika website mbali mbali na vitabu. Waandishi wengi waliandika kwamba wanaume wanapenda sana kutoa I mean kutoa caring, attension na mambo yote yatakayomfanya aonekane kwa mwanamke wake kwamba anajali, lakini inapotokea mwanamke wake akafanya hayo niliorodhesha hapo juu basi mwanaume huyu atajiona kama anadhalaulika,na kuanza ku pull away, je wanaume ni kweli kwamba mnapopendwa huwa mnatabia ya ku pull away, je hampendi wanawake zenu wawaoneshe mapenzi ya dhati, akupe caring attension na vingine vyote? je mnapenda wanawake zenu wabehave vip mnapokuwa kwenye mahusiano.
Tittle ya sredi iheshimiwe.
hiyo list ya wanaume???kichecheeeeeee
Na ww kwa kuangalia mambo yasiyokuhus hujambo,acha bana kuwa na adabusamahani "Kwa wanume tu" Halafu thread yenyewe imeongelewa pande zote mbili.... baadaye..