Kwa wanaume tuu.... Ushauri wenu tafadhali

Uko sahihi kaka, ila watu wanfanya makosa makubwa kuangalia uzuri wa nje na urembo, mwisho wa siku ni kilio.

Fanya makosa mengine lakini usifanye kosa kwenye kuoa/kuolewa,itakuvurugia future nzima,ingawa watu huwa wanasema wako wengi me naona kama ni upotoshaji tu.
 
Naomba niwakague kisha ntakupa jibu sahihi. Ukiwa tayari ni PM
 
Mi mtazamo wangu ni kuoa B. Hakuna kitu kinachoboa kwenye maisha kama kuwa stuck na mtu ambaye hayuko interesting. Kama hapo tu hajaolewa wala hana mtoto halafu amezubaa namna hiyo, itakuwaje mkishaishi pamoja 10 years? Swala la kuwa eti anapenda maendeleo nalo ni tatizo lingine. Ina maana atakuwa too busy na mambo yake kiasi kwamba wewe mwanaume utakuwa humuoni kabisaa.. Na kuna baadhi ya majukumu hataweza kuyatimiza kwasababu ya ubusy. Pia wanawake wa hivyo huwa hawana muda wa kujitake care mf. kujiweka sop sop, usafi wa nyumba nk ni sifuri.. Cha maana ni kuoa B ili akupe changamoto za ku fight maendeleo uyalete wewe na uishi kwa furaha!
 
Namshauri mchague A sababu mambo yamapenzi unaweza mkafundishana na kumjenga kisaikolojia akawa kwenye njia yenyewe kuliko huyo kicheche B

usijidanganye kaka. Mwanamke kama hayuko interested na mapenzi ni ngumu sana kumfundisha akabadilika. Ile ni kitu inatakiwa itoke ndani ya mtima. Ni either ipo au haipo! Na ni nani aliesema mwanamke akiwa mzuri, mcheshi, mchangamfu lazima pia awe kicheche? And vice versa? Mbona wapo wengi wapole, wenye heshima na wapenda maendeleo lakini ni vicheche wa hatari?
 

A, otherwise mchukue uyo b kama hm ndogo!
 

Hapo umenena mkuu....mtu kama A wanaboa sana.ndo wale unajikuta ukitoka mzigoni unafikia baa mpaka usiku wa manane urudi home ukalale tu.
 

hakuna uhusiano wa moja kwa moja kati ya 'maendeleo' na 'furaha'. Kuna familia nyingi zenye maendeleo na hazina furaha yoyote. Tena mara nyingi kadri maendeleo (pesa) inapoongezeka, ndivyo furaha ya kweli inavyopungua. Experience
 
ume generalize sana mkuu uliposema 'wote'.
 
simple,muoe A halafu B mgeuze nyumba ndogo

au kama dini inaruhusu, oa wote! Ila nakuhakikishia muda wote utakuwa kwa B, sehemu zote utaenda na B, mialiko yote utamchukua B, outing zote B, in the end A atabaki kama picha tu kwn hiyo nyumba. (wachagga wana kitu inaitwa 'kuoa trekta'!)
 
Fanya makosa mengine lakini usifanye kosa kwenye kuoa/kuolewa,itakuvurugia future nzima,ingawa watu huwa wanasema wako wengi me naona kama ni upotoshaji tu.

Kweli kabisa ndugu,

Mtu unapoamua kuwa serious na kutafuta mchumba, utaanza kumwangalia kila potential candidate kwa vigezo vyako ulivyojiwekea. Hapo ndipo unapogundua kuwa watu wa kuoa/kuolewa ni wachache sana kwa sababu unatumia kipimo chako kuwapima. Mungu hakuwa mjinga, ndiyo maana watu wa dizaini yako wanahesabika au hawapo kabisa duniani. Ndipo linapokuja suala la kupunguza vigezo na kutafuta balance,

The bottom line...waoaji/waolewaji kwa kila mmoja wetu hawazidi 2...ukibahatisha uwe na sample ya watu 10. Unapokosea kupata correct hit.....Unakuwa tayari umeiweka future yako kwenye mashua yenye matobo wakati huo ukijipanga kwa safari ndefu ya baharini!!

Babu DC!!
 
Hapo kuna mbegu ya mahindi na kuna njugu.
kama unataka kupanda na kuvuna basi chukua mbegu. (A)
kama unataka utamu basi chukua njugu, ongeza chumvi, kunywa na bia. ikibidi alika na rafiki mchangie (B)


I am getting curious na huyu mtu anaitwa Mwali......Anafanana fanana na mtu ambaye tulikutana mahali!!

Babu DC!!
 
Hivi jamani kuna sababu gani ya kuchagua mwanamke hivi as if yeye mwenyewe yuko kamili kila kitu??wewe unajua wamekuweka kundi gani? inawezekana hata A au B haupo kabisa. Inawezekana mtu mwenyewe hujatulia ila unataka mke aliyeko kama malaika!!!
 
We babu acha uongo, tulikutana wapi? lol

Ngoja nikamwombe bibi DC anisaidie ufunguo wa memory.....Yaani kuna dada mmoja hivi, kila kitu anaandika na kufanya kama Mwali!!

Uzee huu jamani...uwiiiii....Enzi zangu ningeshakakumbuka hako kajukuu!!
 
Kaka mchukue A, that shouldnt even be a question. mapenzi atafundishwa tu mbele kwa mbele, ndo maana kuna Singo na Kitchen Party. Inawezekana anaboa kwenye mapenzi due to her past experiences , i.e. her previous lovers weren't as good so kaamua kuchukulia poa sana mambo hayo. sasa ukionyesha maujanja ya kutosha na kumpa attention ipasavyo she will open up. potezea huyo B kabla hujafa kwa presha/STDs.
 
Happiness in life everything ma Friend. mambo mengine huwa yanakuja tu kama uko na furaha maishani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…