Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako!

Utafanya hii kitu niichukue usiku huu. Na vile sina Korea Drama yoyote ile kwa sasa baada ya kumaliza Drama ya Yi Soon Shin. Tatizo sehemu nilipo mitandao ya huku wanatoa MB chache mno.
Hyung kwa jinsi utazamaji wako ulivyo, hii haikufai.
Kwanini? 'sababu bado ni ongoing. Itakupa tabu kuifuatilia so ni bora tu ungojee iwe complete na box yake.
 
Cha Seung-won, who stars in the new movie "Believer," speaks during a showcase for the action film at a Seoul theater.
The movie, which is about a war with Asia's biggest drug ring, will hit local screens on May 24.

hii ndio movie ya mwisho kwa muigizaji kim joo hyuk kushiriki kabla hajafikwa na umauti.
endelea kupumzika kwa amani huko uliko.
kabla ya kifo chako ulituachia zawadi nzuri ya drama inayokwenda kwa jina la god of war.
hadithi inayozungumzia maisha ya mtumwa Kim In-Joon ambaye baadae anafanikiwa kuwa kiongozi mwenye nguvu kwenye utawala wa GORYEO kwa miaka 60.
Hapo ndipo nilianza kumfahamu huyu late ahjussi.
so sad.ulikuwa na ndoto ya kufunga ndoa na mpenzi wako ila Mungu hakuipenda mipango yako na yeye ndiye anayejua sababu kwa nini alikuchukua mapema.
 
Utafanya hii kitu niichukue usiku huu. Na vile sina Korea Drama yoyote ile kwa sasa baada ya kumaliza Drama ya Yi Soon Shin. Tatizo sehemu nilipo mitandao ya huku wanatoa MB chache mno.
Upo North Korea nini?
 
Sijaelewa aliyekufa nani?
 
Basi sawa ngoja nisubiri kitu kiwe kizima kabisa. Mda huo nasubili ngoja nianze kutizama Waikiki
Hyung kwa jinsi utazamaji wako ulivyo, hii haikufai.
Kwanini? 'sababu bado ni ongoing. Itakupa tabu kuifuatilia so ni bora tu ungojee iwe complete na box yake.
 
Sijaelewa aliyekufa nani?
aigooooo inaonekana nimetumia kiswahili kibovu
mian-hae
kwa ufupi kama umebahatika kuangalia drama ya Argon au god of war basi fahamu ya kwamba lead actor ambaye ni kim joo hyuk ameshafariki dunia kutokana na ajali ya gari.
 
Ntaiangalia ila Bado Bado Kwanza Navuta Pumzi kuna kipindi Kikfika Ntaangalia tu.

Ila Lawless lawyer Naisubili.
 
aigooooo inaonekana nimetumia kiswahili kibovu
mian-hae
kwa ufupi kama umebahatika kuangalia drama ya Argon au god of war basi fahamu ya kwamba lead actor ambaye ni kim joo hyuk ameshafariki dunia kutokana na ajali ya gari.
Sote ni wake, na kwake sote tutarejea.
R.I.P
 
Ntaiangalia ila Bado Bado Kwanza Navuta Pumzi kuna kipindi Kikfika Ntaangalia tu.

Ila Lawless lawyer Naisubili.
tvN wako vizuri sana kwenye kuchagua waigizaji wenye umaarufu kwenye sanaa jambo linalopelekea project zao kuwa na mafanikio makubwa, drama nyingi zinazofanya vizuri nchini korea siku hizi zinaonyeshwa na cable tv.
jaribu kufikiria upcoming drama na lead actor wanaoziongoza utagundua jinsi gani wanavyoziweka kwenye wakati mgumu vyombo vya habari kama sbs, kbs na mbc na kupelekea kuongezeka kwa ushindani wa kibiashara.
  • mr sunshine = lee byung hun na kim tae ri.
  • Knowing Wife =ji sung na han ji min
  • lawless lawyer = lee joon gi na seo ye ji
  • memories of alhambra = hyun bin na park shin hye
  • why secretary kim = park seo joon na park min young
 
aigooooo inaonekana nimetumia kiswahili kibovu
mian-hae
kwa ufupi kama umebahatika kuangalia drama ya Argon au god of war basi fahamu ya kwamba lead actor ambaye ni kim joo hyuk ameshafariki dunia kutokana na ajali ya gari.
Haha mwanzo ulitumia kijapan na sie humu wakorea,sasa nimekupata.
 
Ilipewa promo balaa Lakin sikutaka kuitizama kwasababu ilikuwa ni Ongoing. Kwa Ongoing Drama niliyo tizama ni Black pekee. Ata misty bado sijaicheki ila nikirudi huko nyumbani nitaipakua yote.
Nami nitaijaribu nione hiyo waikiki maana si mchezo ila sasa naangalia comedy nyengine inaitwa modern farm.
 
Namuona Kim nana wangu hapo.
 
Ni Kweli KBS, MBC SBS Wanazidiwa Na Inaonesha Kabisaaa Inavyozidiwa Izi Cable Tv Wanatoa Drama Kali Sana Siku Izi
 
Ichi kilichotokea Leo Korea Na Kifananisha na Drama Ya King 2 Hearts Alocheza Seung ji Na Ha Ji Won Na Ata Ule Mstari ulowatanganisha Kusini na Kaskazini Sikuwa Najua kama ni kweli Upo.

Kweli Nimeamini Korea Inayaweka Maisha Yao Ili Jamii Nyingi Wayajue Kupitia Sanaa Na kwa Kuingiza Pesa Na Kutangaza Nchi Yao. Safi Sana.
 
ni tukio la kihistoria ambalo naamini wakorea zaidi ya million 80 limewafurahisha siku ya leo, mungu azidi kuwasimamia ili waweze kutimiza yale walioahidiana.
sijui hapa nilipo kuna mtu anamenya vitunguu maji najikuta natokwa na machozi baada ya kuisoma hii habari kwenye tovuti ya soompi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…