nimechelewa kumtakia kheri ya kuzaliwa
Mr Song Il kook ahjussi siku ya jana kwa sababu zilizo nje ya uwezo wangu
kutoka 01/10/1971 hadi 01/10/2018 ni miaka 47 kwa mahesabu ya kawaida ameshatimiza mwanadamu huyu tokea afanikiwe kuuona muangaza wa jua na mwezi wenye kung'ara nyakati za usiku.
ila kwa kutumia kikokotoa cha korea kama sijakosea atakuwa ametimiza miaka 49
musiniulize kwa nini umri wa wakorea unaongezeka kwa miaka 2.
wakorea wanaanza kuhesabu mwaka wako pindi unapokuwa tumboni kwa mama yako, inamaana ukizaliwa unakuwa na mwaka mmoja na si mwaka 0 kama tunavyoaminishwa na wamagharibi, wanatumia neno
한 살(han sal) = mwaka mmoja.
pia wakorea wanahesabu tarehe ya mwaka kuanzia mwezi january haijalishi umezaliwa tarehe inayotofautiana na mwezi january.
ina maana kama umezaliwa 30/12 siku mbili zijazo utakuwa na miaka miwili tokea uanze kupambania maisha yako
kwa mfano mkorea anapokwambia ana miaka 20
스무 살(seumu sal) =“twenty years old” kwa kutumia kikokotoa cha kwao tafsiri yake ana miaka 18 kwa kikokotoa cha wamagharibi au miaka 19.
kwa maelezo zaidi tembelea tovuti hii.
- vile vile 1 october ni siku ya maadhimisho ya kijeshi nchini korea.
- siku ya uhuru kwa nchi ya nigeria
wanaijeria musije mukanifuata PM na kunimwagia povu la matusi kwa kushindwa kuweka picha yenu, hakuna asiyewafahamu mabwana nyinyi kwa maneno ya ovyo kuliko wavuvi wa kipemba.