Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako!

Dah umenitia moyo ila penye mapanga huwa ni mziki😂😂😂
Sema ntaicheki
 
DAEMUSHIN sunbae hicho ulichofuta ni nini? Halafu hiyo tabia wala sio nzuri kila siku nakuambia

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
nilikuwa nakusalimia lakini baadae nikakumbuka:
oohhhh! huyu bibi si ndiye yule aliyekuja na comment yenye upovu ndani yake.
hujaacha kuangalia wakorea bali umepumzika tu, ukaendelea kusema hata mimi nishawahi kupumzika miaka 10.
hivyo nilikhofia salamu yangu hutoitikia.
===========
 
nimevutiwa na speed ya hii drama katika kutuhadithia matukio ya kihistoria ambayo yamerekodiwa huko nyuma, ukijumlisha na mzuka wa kutokuangalia traditional epic sageuk kwa muda mrefu nimejikuta naitamani weekend ifike tena, hii ndio drama niliyoichagua kuiangalia katika safari yangu ya kumalizia mwaka (kuna drama nyingi nimezisamehe).

hadithi yake imeturudisha pale magenerali wawili (yi seong gye na jo min su) waliopewa amri ya kuanzisha vita dhidi ya Ming kwa lengo la kugomboa ardhi ya liaodong ambayo hapo zamani ilikuwa ni sehemu ya Goguryeo walipoamua kugoma na kurudi mji mkuu wa Gaegyeong.

kama umeangalia jung do jeon, the great seer na six flying dragons unajikuta unafanya mrejeo wa tukio hilo. Ila kwa kuwa jung do jeon drama ni traditional epic sageuk sina budi kuwapa credit kwa kutujuza kilichotokezea kwa ushahidi wa kihistoria tofauti na drama nyenginezo tajwa hapo juu.

fikiria episode 2 tu zimetupa matukio haya yafuatayo
  1. kushindwa vita kwa general choi yeong hatimaye kupewa adhabu ya uhaini: yeye ndiye alikuwa mstari wa mbele kumshawishi mfalme apeleke jeshi la kupambana na ming.
  2. kuondolewa madarakani kwa mfalme na hatimaye mwanawe mwenye miaka 9 kuirithi nafasi yake.
  3. general jo min su kutake power ya royal family.
  4. yi seong gye kumsambaratisha general jo min su (japokuwa tukio hili limeonyeshwa kwa sekunde chache)
  5. mfalme alioondolewa madarakani kutuma wauaji dhidi ya yi seong gye, tukio hili ndipo ilipoishia episode 2. Nafikiri hii itakuwa ni drama ya 4 kutuonyesha tukio hili (kwa aliyeangalia the great seer pia atakuwa analikumbuka hili tukio la mfalme kumpa mtumishi wake kisu)
what next huko mbeleni kabla hatujaingia kwenye upande haswa wa YI BANG WON
  1. Yi seong gye kuanguka na farasi
  2. kifo cha poeun
  3. kuanguka kwa goryeo
  4. kifo cha malikia
  5. mapinduzi ya yi bang won yaliopelekea kifo cha jung do jeon na wafuasi wake pamoja na watoto wa mke wa pili wa Yi seong gye.
ngoja tuweke oda ya ubuyu wa babu issa.
YI BANG WON alikuwa ni mtawala mwenye maarifa ya kutosha, lakini yote hayo hayaondowi ukatili wake usiomithilika
  1. aliwaua macomrade wake wengi aliopambanana nao pamoja kwenye mapinduzi ya kwanza na mapinduzi ya pili
  2. aliwaua ndugu zake
  3. aliwaua ndugu wa mke wake (Lady Min)
  4. alimuua baba mkwe wa mtoto wake (sejong)
  5. alimuua jung do jeon (sambong) na jeong meong jo (poeun)
  6. n.k yote hayo lengo kuu ni kuimarisha royal family.

 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787] naona umeniita ahjuma umechoka sasa waniita bibi. Una mashaka mno na maisha yako

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Sababu kuu ya kutomalizia Six flying dragons ni baada ya kuona yi bang won anaanza kuwa msenge msenge...nilikosa kabisa hamu ya kuendelea kuangalia na hivi umeshaniambia hapo ndio basi nimeshaimaliza

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Duh kumbe kuna vingi, mie naangalia tu bila kujali quality. ninachozipendea hizo site mbili link zake hazina expire date wala time kama kissiassian. nkiri na kimoi unaweza laza kiporo leo ukamalizia kesho au kesho yake bila kuhangaika kuirudia drama sehemu husika.
kimoitv video quality yake ni ndogo sana ukilinganisha na tovuti ya nkiri.
raha ya mkorea umuone na weupe wake.
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787] naona umeniita ahjuma umechoka sasa waniita bibi. Una mashaka mno na maisha yako

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
huongozwa na mashaka yenye kuambatana na wasiwasi kwa kila ninachokiandika au kukizungumza mbele ya hadhira. hufikia hatua huliwazia jibu nitakaloweza kujibiwa.
Ndio maana hufikia uamuzi wa kufuta baadhi ya comment zangu (hufanya hivyo kwa watu maalumu)

wasiwasi wako ndio maradhi yako.
 
Jioni ya Ijumaa nilishusha episode 7 za vicenzo drama (nimechoka kusifiwa) kupitia tovuti ya nkiri, usiku ulipoingia mwenyewe najikaza nataka kuziangalia.

episodes zote zinacheza sauti kama matangazo ya redio lakini video haionyeshi.
nilichafukwa kwa hasira zenye malalamiko ndani yake.
usawa huu wa kununua bando la GB 1 kwa shilingi 2000 hutakiwi kufanya makosa.
 
Bulgasal drama mpya ya moto sana sitaki kuwa spoiler nadhani mnsmuelewa Lee Jin Hyeok

Snowdrop nayo ni balaa hasa ikia kwenye political plot male lead Soo Ho anasakwa hatari mno na askari na usalama wa Taifa

Kuna chuo cha wanawake anachosoma female lead wetu Eun Young-ro(Jisoo) humo ndani huwezi kununa fujo tupu[emoji23]
 
Pole sana maana nishasahau kuwa mteja wa bando la drama. Walinitesa sana wapandisha data,shuaini zao
 
Unatakiwa kufikiria hayo kabla ya kuandika

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Tofauti kati ya uc browsers

UC browser saa nyingine ukiwa unadownload ukatoka kwenye hio browser mfano kujibu watsup,sms au kwenda app nyingine inastop downloading(pause)

UC mini browser inakupa uhuru wa kuzurura na unarudi unakuta bado inadownload ila nayo unatakiwa kuichangamsha unaweza dhani inaendelea kudownload kumbe imestop. hivyo ukiona namba hazitembei pause kisha resume download itaendelea
 
Hii mbinu na mimi nimeigundua ya kupause na kuresume...sasa hivi naserereka tu [emoji1787][emoji1787]

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
mbinu safi sana. nikiwa uc browser inabidi kudownload episode moja kwenye huu mseleleko ila uc mini unapiga hata nne kwa wakati mmoja.

nipo na one the woman bila kusahau gangnam scandal
Hii mbinu na mimi nimeigundua ya kupause na kuresume...sasa hivi naserereka tu [emoji1787][emoji1787]

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
mbinu safi sana. nikiwa uc browser inabidi kudownload episode moja kwenye huu mseleleko ila uc mini unapiga hata nne kwa wakati mmoja.

nipo na one the woman bila kusahau gangnam scandal
Mimi kweny hiyo hiyo uc browser nikiona kuna network nzuri naanzisha episode kama nne hivi halafu naanza kwenda nayo moja moja kwa mtindo wa ku- pause na ku-resumehadi zinaisha

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
kwann wanaifuta?
Mambo ya historical inaccuracy kuhusu historia zao enzi za Dictatorship tule miaka ya 1980's na kuingia kwa spies toka North Korea yaani mambo mengi viewers zaidi ya laki 2 wamesign petition ya kucancel drama.

Pia makampuni yaliyokuwa kwenye sponsorship yameanza kujitoa yaani uwezekano wa hii drama kuendelea ni 1% yanakuwa kama ya Joseon Exorcist
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…