Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako!

Moonshine nzuri sana mkuu endelea nayo hadi mwisho

Halafu sijui ep ya 13 kama imetoka
Sina mpango wa kuiacha ila hapo kwenye uzuri mmh, asingekuwa Yoo seung ho ningeiachia mwanzoni tu. Visa vya mapenzi vinaeleweka ila siasa ya mule hata siielewi
 
Huyo kila drama ninayomuona ni comedian mzuri tu,kwenye uncle mwanzon kaweka ndevu sikumtambua ila alipozitoa nikatabasamu.
Sana hata kwenye it's okay not to be okay Yule sang tae (kaka mtu) alifanya kazi kubwa sana
Red sleeve mwanzon tamu sana utainjoy.
Hahahah mpaka unajiuliza kwani nakuwa monitored kutizama.

Mimi Bossam imefanya niogope hizi historical za miaka hii, Nataman kuivuta Io red sleeve Ila trauma ya bossam haijaniacha poa.
Kuna hii Happiness niliona inasifiwa sana sehemu nikaivuta. Nimevutiwa na Doctor mjenda naenda nayo mpaka mwisho ili tu nimuone😂😂😂
 
Sina mpango wa kuiacha ila hapo kwenye uzuri mmh, asingekuwa Yoo seung ho ningeiachia mwanzoni tu. Visa vya mapenzi vinaeleweka ila siasa ya mule hata siielewi
Siasa za mule hahah

Pale chief state counselor na chief royal secretary wote ni opportunists mule .

Chief Royal secretary ndio mysterious mechant anaeforce prohibition ya pombe il yeye a take advantage ya soko la kitaa kwa kumtumia mechant nani yule sijui(majina ya kikorea magumu kwangu[emoji2])

Chief royal secretary ana mpush mfalme kwenye ajanda zake bila mfalme kujua kuwa jama ni bonge la villain anamzunguka tu.

Anamtumia crown prince kama mwamvuli wa madhambi yake.

Chief royal secretary na mama yake crown prince ni ndugu wote walikuwa slaves wakapata freedom.

Saaa dogo inspector nam young atakuja kuwacharaza bakora wote Chief royal secretary na chief state counselor maana wana mishe mishe nyeusi coz dogo ni very patriotic na mbaya zaidi crown anajielewa sana huko mbele

Watakuwa mwiba mkali sana
 
Usiwe unahadithia mkuu unapunguza uhondo. The king affection nimeivuta yote ila mpaka sasa najivuta kuiangalia sababu ya hadithi za humu
 
Ebwana eeh nilikuwa napata tabu kudownload hata episodes 5 kwa Wire Tun kumbe tatizo dogo sana sasa hivi nakimbiza hadi episodes 15 kwa siku speed ya 800kbps hadi 2mbps.[emoji2956][emoji2956]

Halafu mtu akinitext pm anitaarifu hapa mi mvivu kuangalia notifications nimekuta watu zaidi ya 10 message zao za tangu January mwanzoni wakitaka hints ila nna imani washaelewa kupitia kwa wengine
 
Tupe ujuzi tukimbizezaidi na sie.

Vipi kwenye upande wa kuisha chaji. Kwangu napata speed tamu ila chaji majanga

Halafu tatizo la wire ukiisifia popote tu wanaanza kuzingua sijui kwann
 
Tupe ujuzi tukimbizezaidi na sie.

Vipi kwenye upande wa kuisha chaji. Kwangu napata speed tamu ila chaji majanga

Halafu tatizo la wire ukiisifia popote tu wanaanza kuzingua sijui kwann
Tumia line ya Tigo 4G halafu pale ambapo huwa speed inashuka hadi 0.0kbps kama dk 3 we zima data then unawasha inaendelea kusonga tu.

Tigo ni moto speed yake inapiga hadi 2mbps now ttcl natumia muda wa kuperuzi tu
 
Usiwe unahadithia mkuu unapunguza uhondo. The king affection nimeivuta yote ila mpaka sasa najivuta kuiangalia sababu ya hadithi za humu
Umeongea vyema...kila siku huwa nasema humu ila hamjawahi kuniunga mkono kumbe wengi hampendi...wabaya sana ninyi[emoji16][emoji16][emoji16]. Kama mimi wakati naangalia mwanzoni nilijua chief secretary ni mtu mzuri kabla ukweli haujajulikana episode sijui ya kumi na moja huko. Ningekuwa sijaangalia bado ndio basi tena nisingeiangalia tena
 
Shukrani sana. Nimejikuta nacheka maana sijawahi kumiliki laini ya tigo sasa hapa nina laini zoootee kasoro tigo,mwaka huu tutakoma wapenda mseleleko
Tumia line ya Tigo 4G halafu pale ambapo huwa speed inashuka hadi 0.0kbps kama dk 3 we zima data then unawasha inaendelea kusonga tu.

Tigo ni moto speed yake inapiga hadi 2mbps now ttcl natumia muda wa kuperuzi tu
 
Asante nianze na happiness tu
 
Young lady and gentleman Japo ni ongoing ila inanipa burudani weekend hii
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…