Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako!

Kabisa zile side dishes si mchezo,asubuhi mchana na jioni. Bado tabia zao za kunywa chai,mgeni anaalikwa chai na sio juisi wala soda..

Wana aina nyingi za chai usijeshangaa unanyweshwa chai ya mchicha ila inapewa jina taamu la kizungu au kikorea
ukiajiriwa kazi ya upishi kwa mkorea jiandikie umeumia, kwa siku wanapika dishi zaidi ya kumi kwa vyakula tofauti. utaosha vyombo mpaka mikono ifanye ganzi
 
Kabisa zile side dishes si mchezo,asubuhi mchana na jioni. Bado tabia zao za kunywa chai,mgeni anaalikwa chai na sio juisi wala soda..

Wana aina nyingi za chai usijeshangaa unanyweshwa chai ya mchicha ila inapewa jina taamu la kizungu au kikorea
Zile chai zao kwanza nahisi hata haweweki sukari, mimi nikienda kwao sitakunywa hata ila mimi nitajaribu ile gisaeng tea sijui nimepatia kuandika
 
Kituko kingine ni utafunaji wao😄.

Aina ya vyakula wanavyokula ndo vinafanya mtu wa miaka 45 umuone kama yule wa 30's , vyakula vyao vingi akipewa mbongo atasema kapewa mtishamba. Sio wakorea tu hata wachina.

Nawakubali sana Wakorea na Wachina linapokuja swala la kanuni za ulaji, sisi wabongo tulitoka kwenye msingi yetu tunataka vyakula wa kimagharibi ambavyo hata hivyo bado tunavikosea kwenye uandaaji, ndoamana kijana akila CHIPS huku anaota matiti.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…