Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako!

tunaotumia vitochi haya mabadiliko ya JF yanatuadhibu. Font za kichwa cha habari na maelezo yake utadhani matangazo ya msiba. Kitufe cha all forums kimefichwa mbali utadhani chakula cha bibi na bwana harusi kwa siku 3 za mwanzo. Baadhi ya nyakati thread inakurudisha kurasa ya kwanza kanakwamba nilikimbia jf.
 
Pole buana, karibu maana ulipotea
 
Karibu kwa wasukuma ufaidi,msukuma anapenda kununua mavitu makubwa makubwa kupita uwezo wake mfano simu😂😂😂😂😂wenye masimu makubwa wanaona mabadiliko kama hayawahusu vile
 
google wameniambia neno fanboy lina maana ya shabiki wa kiume juu ya jambo husika mfano muziki n.k. Je wewe ni mwanaume au nimeelewa vibaya andiko lako. Siku zote nakuchukulia wewe ni jinsia ya kike. Mwengine ni huyo aliyeweka avatar ya lee seung gi nafikiri ni mqaxy. Hivi Khantwe wewe ni keee au mbuzi meee. Nakusalimia mchumba wa siri wa marehemu said mabastola.
 
Karibu kwa wasukuma ufaidi,msukuma anapenda kununua mavitu makubwa makubwa kupita uwezo wake mfano simu😂😂😂😂😂wenye masimu makubwa wanaona mabadiliko kama hayawahusu vile
na nimesikia wanataka kufanya maandamano ya amani ya kumpongeza Maxence Melo na timu yake ya madeveloper kwa mabadiliko haya. Hii nchi uhuru umekuwa mwingi sana mpaka waziri anakimbia bungeni bila ya taarifa.
 
Jamani huyu mwandiko wake unaonyesha kabisa ni me, hata mimi ni me
 
Wanawake wa kikorea wanachukia vingi mpaka naona ni kazi mno kuwaelewa ila vingine wanabuni kwa manufaa yao ya ubinafsi(uchoyo tu)
kwa mujibu kdrama wanawake wa korea wanachukizwa na menopause, sijui maana yake nini hilo neno maana naliona sana likitamkwa na madaktari kwenye dramas zao.
 
umeangalia drama ngapi za huyo dada, nimeona mbili na mpaka kesho sitozimaliza.. Ukianza zoezi la kutafuta mchumba muislamu tafadhali nitaarifu, ninaye ndugu wa kike ni mrefu kama lionel messi. Uzuri ana degree ya kupaka makeup.
Eti mrefu kama lionel Messi dah! Unajua kunifurahisha, drama za huyo dada sikumbuki majina yake lakini ni mtu ambaye wakulilia mwenye machungu na huzuni kwa drama zote zake nilizocheki
 
DOCTOR LAWYER inaanza leo, natumai haitokuwa mbaya ukilinganisha na projects nyenginezo nilizozijaribu kwa mwaka huu zikanishinda. Karibu tena kwenye tasnia ya sanaa bwana harusi SO JI SUB. Ninachohitaji ni kuiona sura ya mchumba wangu sijui ni IM SE MI au IM SOO HYANG. Dah hata casts nimeshawasahau. Nimemkumbuka mwengine SHIN SUNG ROK.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…