Kwa wasiojua kupika wali, watoa bokoboko hii ni njia rahisi kwao

Kwa wasiojua kupika wali, watoa bokoboko hii ni njia rahisi kwao

Finegirlone

JF-Expert Member
Joined
Oct 9, 2018
Posts
1,836
Reaction score
3,609
Habari zenu wapendwa, amani iwe nanyi

Kwa kuanza bandika sufuria lako la maji jikoni ila maji yanatakiwa yawe mengimengi kuzidi kiasi cha mchele tofauti na ule wali wa kukadilia maji kutokana na kiasi cha mchele.

Baada ya maji yako kupata moto tia chumvi kulingana na kiasi unachopenda, funika acha ya chemke.

Baada ya kuchemka tia mchele wako ulioshwa na kulowekwa kama dakika kadhaa hata kama haujaloweka sio kesi ila mchele ukitaka unyooke uwe mtamu ni vema kuloweka dakika kadhaa hata saa kabla ya kuupika.

Uchemke hadi ufikie kiasi cha kuwa mgumu hivi ukiutafuta kama unaugumu fulani lakini ile hali ya ubichi wa mchele ushapotea umebaki mgumu.

Epua, chukua chujio lako kubwa na bakuli kubwa au sufulia ama vipi utafanya kusudi ni kuuchuja ule mchele, yale maji mwaga halafu mchele urudishie kwenye sufuria yako ileile rudisha jikoni, tia mafuta kwa juu ya wali kiasi upendacho hata kama haupendi mafuta sio lazima kuweka, seti moto wako hafifu kiasi, kama jiko la mkaa pia fanya moto mdogo sana maana wali umebaki hatua ndogo kuiva kwa hiyo hauhitaji moto mwingi, baada ya dakika 5- 7 utakuwa umeiva.

Tayari kwa kuliwa, kwa njia kamwe hautopika bokoboko au kuunguza chakula.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mh,,haijaeleweka ,,,


Yani Maji mengi mpaka yabaki ya kuchuja?? Kwann nisiweke Maji kiasi cha ya kikauka inatosha
 
Sijui lini nitaanza kujifundisha Kupika.

Hapana, Kupika kuna wenyewe
 
Nataka kupata hili somo lakini Nina mashaka na Shule uliyotoa, nitaendelea kupika bokoboko mpaka nitakapopata Mwalimu mzuri
 
Binafsi napenda wali uive vizuri ikibidi hata ukiwa bokoboko poa tu kuliko wali wa kudunda!
Wali mkavu wa kuchambuka hapana!
Nauona mbichi!
Ndo maana ni nadra sana Kwangu kula wali wa majiani


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Binafsi napenda wali uive vizuri ikibidi hata ukiwa bokoboko poa tu kuliko wali wa kudunda!
Wali mkavu wa kuchambuka hapana!
Nauona mbichi!
Ndo maana ni nadra sana Kwangu kula wali wa majiani


Sent using Jamii Forums mobile app
Dah tuko tofauti aisee boko boko mimi hapana gusa kabisa, fortunately mke wangu is a great cooker... Wali wa nazi mmoja mmoja, njegere kidogo au sometimes iliki..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Miwali ya bokoboko inakera sana...

Asante kwa somo zuri!!
 
Sasa tabu zote za nini wakati rice cooker ni 50,000/= tu.
 
Nitajaribu hii njia ya kuchuja Kuna sehemu pia nimeona ingawa naamini kabisa virutubisho vinapotea.Kinachonishanga ni kuloeka mchele, nahisi utakuwa bokoboko
 
Back
Top Bottom