FirstLady1
JF-Expert Member
- Jul 29, 2009
- 16,789
- 5,401
Kusema ukweli ile habari ilinivunja moyo halafu binti mwenyewe alivyokuwa anafanana na mamake!! Mh hata sijui tufanyeje hapo usikute alionywa kidogo tu akaona anaonewa. Nadhani kwa staili hii itabidi tuwe tunawaonya watoto wetu kwa kuwalia timing kama tunavyofanyaga kwa spouses wetu!! unasubiria kwenye good mood ndo unaanza lakini mwanangu, siku ile kusema ukweli sikufurahia...........
Swali la 2 ni: How to balance! kuwa mzazi/rafiki/mshauri kwa watoto wetu? hii siku nyingine wapendwa.
Nakubali kukosolewa ili nijifunze zaidi
Mix with yours
kutokana na maelezo ya mama na dada wa binti aliejinyonga pamoja na majirani, kunauwezekano kuwa binti alikuwa na ujauzito, alijaribu kutoa ikashindikana akaamua kujiua, siku moja kabla ya kujiua alikuwa amejifungia ndani muda mrefu, dada yake alikuja jioni na kumgongea mlango lakini alichukua muda mrefu kufungua, haijulikani nini alikuwa akifanya, inaonyesha ndo siku aliyojaribu kutoa mimba, usiku wake mama yake alimuona katika hali ya utulivu sana hakuwa akiongea na mtu, akamuuliza lakini mtoto akasema kuwa hakuna shida, siku ya kijiua alikwenda bafuni kuoga kama vile anajiaanda kutoka kwenda kwenye shunghuli zake.
swala linaloshangaza nikuwa alikutwa na kamba ya kujinyongea shingoni lakini hakuwa amejitundika popote kama ilivyo kawaida ya watu wanaokutwa wamejinyonga, maiti ilikutwa nyuma ya mlango ikiwa imezua mlango kwa ndani, kutoka damu sehemu za siri, majimaji.
Kuna maswali mengi ambayo familia na majirani wakiulizwa unaweza kupata majibu sahihi katika hili
Huu ni mtazamo wangu, polisi nao watakuwa na yao.
Kwanza nikushukuru Kwapwani na wale wote waliochangia mada hii, Nimepata faraja moja kubwa sana kuwa wapo watu ambao wanatafakari namna bora ya makuzi ya watoto, tuendelee na kazi hii ngumu na wala tusichoke wala kukata tamaa. ila napenda kuongezea kuwa katika malezi haya na hasa katika kujenga mahusiano kati ya mzazi na mtoto ni wajibu au ni vyema na inapendeza sana kushirikishana wazazi wote wawili yaani baba na mama, maana naamini tumekulia katika tamaduni tofauti na mapokeo ya maisha pia ni tofauti itakuwa ni jambo la busara mkikaa kama wazazi na kuweka mikakati ya pamoja ya namna bora ya kulea watoto hasa ukiangalia changamoto za maisha. kuna njia nyingi za kufundishana siku hizi vipeperushi vimejaa vya namna ya kufungua amongezi, usiseme umechelewa hata sisi na uzee huu naamini tunatamani wazazi wetu wawe karibu zaidi na sisi waoneshe kutupenda, kutusikiliza na kutuamini kile tunachowaambia. unaweza pi search parental child communication kwa maelezo zaidi.
Mungu Awajae zekhi na baraka tele wazazi wote na wape subira na uvumilivu katika malezi.
Kwa kweli ni muhimu sana wazazi wa sasa kuwa karibu na watoto wetu kwani hatari ambazo zinawazunguka watoti wetu ni nyingi,hasa kwa wenye watoto wa kike hatari pale nyumbani ,hatari barabarani na hata huko shuleni.Ni muhimu kuwa karibu na watoto wetu ili waweze kutuuliza na sisi ndio tuwe watu wa kuwapa majibu ya maswali mengi waliyonayo kuliko wapate majibu hayo kutoka kwa watu wengine ambao wanaweza kumpotosha.
Asante sana Kapwani..
Kwa hii Post yako nakumbuka machungu yaliyonipata nikiwa na umri mdogo sana13-15 lakini kwa sababu wazazi wetu enzi zile hawakutuweka karibu sana ..walijenga mazingira ya sisi kuwaogopa hata ukiwa na jambo kumuanza unaona issue sana unajihoji mara mia
Sitasahau ...sitasahau
Kabinti kangu sasa kanasoma baby class najitahidi kuwa karibu nae nimwelewe hatua kwa hatua katika ukuaji wake hata sasa akitoka shule ananipa vituko na viugomvi vyao vya kitoto nafarijika.Pale napoona kakosea namwambia tu hapa sio hivi mwanangu ...
Nitajitahidi kuwa karibu nae siku zote za maisha yangu.
Inasikitisha
Mie niko karibu sanasana kwa kweli, kitu chochote lazima aniambie yaaani, na ninamweleza wazi mambo ya dunia yalivyo, tangu hivi na umri mdogo, kwa hiyo hata akikua nitaendelea hivihvi, sasa mie nina ndugu zangu ni wakali hatar, utakuta watoto wao wanakuwa karibu na mie na kunieleza mambo mengi kuliko hao wandugu, na mie natumia nafasi hiyohiyo kuwapa mafunzo ya dunia inavoenda na kuwa kama mwongozo bila kuwasemea au kuwakaripia
Kwa huyo mtoto itakuwa tu mambo ya wanaume tu, mtoto akiingia uteenager usipokuwa na busara unaweza ua, sababu wanakuwa wanafikiri wanajua kuliko wewe, yaani wanaweza mwona mzazi kama mshamba fulani hv, inabidi uwe na zaidi ya busara kuweza kuwa handle hawa watoto
...Tuko pamoja nami pia hiyo ilinishangaza kidogo. Niliwahi kushuhudia bwana mmoja amejinyinga miaka ya 80 lakini sikuona akitokwa na damu kwa hiyo hata kwa yule binti kuona ametoka damu ilinishangaza at least kwa mkojo inaeleweka maana kule ku-suffocate lazima matundu yaweza kutoa kutoa some discharge!!!..I thought some fishy thing was behind the whole story!!!...Ahsante sana mpendwa kwa hilo, huu ni ukweli usipingika,mimi niliona taarifa hiyo ilisikitisha sana, ila kinachonishangaza sana ni kuona damu, hivi kweli mtu akijinyonga anatoka damu au kuna kitu kimejificha hapo!!!!!
....Kapwani unachosema nakiona mara kwa mara kwa my wife wangu.Tuna mabinti wawili 1st born ni 9 years na 2nd born ni 6 yrs. Huyu mdogo yeye akiwashwa kidogo mbio kwa mama yake kumuonyesha tena anavua na chupi kabisa. Nilichogundua kwa mke wanguni hofu kubwa inayomkumba kwa hiyo humpekenyua sana na maswali mengi. Kwa kweli nami pia nashawishika kuwa amakini na mienendo ya watoto wetu lakini tusikimbilie sana kutumia mabavu katika kutafuta ufumbuzi ni hatari.Pole kwa yaliyokupata dear...nami nakumbuka siku moja nilichezea majani ya magimbi baadae nikajishika sehemu*****kwa bahati mbaya nadhani nilikuwa na miaka 9 ivi, basi nikajisikia kuwashwa sana na maumivu ....nikaamua kumweleza mama kuwa najisikia hali hii mahali hapa....looh aliniuliza tu swali moja...je umeshaanza kucheza na wavulana.....maskini sikuwa hata na idea hiyo nikajibu kwa hofu hapana....jamani mama akakaa kimya, hakunikagua wala kufanya lolote ( kumbuka sikuwa nimwemwambia habari ya najani yale).....next day akasema bado unaumia nikajibu no nae akala kona..... basi sikukata tamaa nikatamani sana kujua why nilipatwa nahali ile....baadae wenzangu wakaniambia kuwa ni utomvu wa majani ya magimbi na kuniasa nisishike tena
mix with yours