Kwa yanayoendelea Simba SC kipi kati ya haya mawili kilikuwa cha muhimu ilipocheza na Vipers FC leo Kampala?

Kwa yanayoendelea Simba SC kipi kati ya haya mawili kilikuwa cha muhimu ilipocheza na Vipers FC leo Kampala?

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Je;

1. Simba SC icheze mpira wake wa Samba Loketo ila ifungwe au iambulie sare/suluhu kisha timu na mashabiki tuvurugane zaidi, tuchapane bakora, tuchekwe na watani zetu Yanga SC na mgogoro uzidi Kukua.

au

2. Simba SC icheze vibaya kama ilivyocheza leo (tena ikiwa ugenini) Jijini Kampala dhidi ya timu ambayo ilikuwa inahitaji ushindi wa udi na uvumba na ipate Ushindi wa goli/bao moja iliyoupata ili kutuliza hali mbaya kikosini, kwa uongozi na kwetu mashabiki akina GENTAMYCINE, kisha kurejesha morali kwa wapiganaji wetu (wachezaji) na kurejesha saikolojia iliyopotea ghafla kwa wachezaji.

Ili tukirejea Dar es Salaam tutulie, tumalize tofauti zetu, tushirikiane na tuunganishe nguvu zetu, ili alama sita (6) muhimu za Vipers FC na Horoya FC kwa Mkapa tuzipate na tuwe na jumla ya alama tisa (9) ambazo zitatupeleka Knockout Stage (Robo Fainali) ya CAFCL kisha tuendelee kulinda heshima yetu, kuitangaza vyema nchi yetu na kuongeza alama (points) zaidi ambazo zitasaidia Tanzania kama nchi kuingiza tena timu nne (4) kwa msimu ujao wa mashindano.

Nasubiria majibu yenu ila niseme tu kuwa kwa hali iliyokuweko Simba SC kabla ya Mechi yake dhidi ya Vipers FC leo nilitegemea wana Simba SC wote tungeanza kuhamasishana ili twende kuwapokea mashujaa na wapiganaji wetu (Wachezaji wa Simba SC) kwa huu ushindi muhimu wa leo dhidi ya Vipers FC tuliokuwa tunauhitaji kwa kumuomba Mwenyezi Mungu na mizimu yetu ya Kizanaki, Kimakuwa na Kitutsi.

Wachezaji wametuheshimisha mno.
 
Kwa ule umaliziaji butu kama ule tutaweza kupata alama 6 kwa mkapa kweli?
Maana hata goli lenyewe kushukuru sana, halafu jamaa kama walinyimwa penalti moja
 
Pamoja na ushindi wa leo lakini Simba chini ya Robertinho siwaelewi. Mpira gani wa kubutua butua tu? Toka lini Simba wameanza kucheza mpira wa long balls? Hivi kwa Horoya, ninavyowatizama muda huu na Raja, tutatoka kweli? Mbona naiona Simba ya hovyo sana wakati huu wakati wachezaji ni wale wale? Huyu mwalimu ana shida ya kifalsafa dhidi ya faksafa asili ya Simba. Tuombe Mungu abadilike lkn sioni tukiifunga Horoya kwa Mkapa kwa mpira wa leo dhidi ya Vipers.
 
Kwa ule umaliziaji butu kama ule tutaweza kupata alama 6 kwa mkapa kweli?
Maana hata goli lenyewe kushukuru sana, halafu jamaa kama walinyimwa penalti moja
Tutajipanga na tutakuwa Bora mno.
 
Pamoja na ushindi wa leo lakini Simba chini ya Robertinho siwaelewi. Mpira gani wa kubutua butua tu? Toka lini Simba wameanza kucheza mpira wa long balls? Hivi kwa Horoya, ninavyowatizama muda huu na Raja, tutatoka kweli? Mbona naiona Simba ya hovyo sana wakati huu wakati wachezaji ni wale wale? Huyu mwalimu ana shida ya kifalsafa dhidi ya faksafa asili ya Simba. Tuombe Mungu abadilike lkn sioni tukiifunga Horoya kwa Mkapa kwa mpira wa leo dhidi ya Vipers.
Tutabadilika na tutafanya vyema mno.
 
Kwa hali ilivyo niseme tu rasmi nimeamini wachezaji wetu miili imekataa japo roho inataka mafanikio kwa timu

Mzamiru anashindwa kupress tu afunge anacheck ampasie mtu mwingine wakati mwenzake kabanwa ,
Chama wa kukimbia na mpira vile afu abutue kiwango kile kweli?

Tukasajili wachezaji zaidi kwa hali hii tutageuka Liverpool soon
 
Je,....

1. Simba SC icheze Mpira wake wa Samba Loketo ila ifungwe au iambulie Sare / Suluhu kisha Timu na Mashabiki tuvurugane zaidi, tuchapane Bakora, tuchekwe na Watani zetu Yanga SC na Mgogoro uzidi Kukua
Usijibaraguze, dua yako imekataliwa. Mungu huwa hasikilizi dua ya mpumbavu

Maombi yangu kwa Mwenyezi Mungu na Mizimu ya Kwetu ni Kuomba tu Simba SC tufungwe ili Safari hii tutoane Roho na Klabu isiwepo tena katika Ramani ya Soka Duniani.
 
mkuu unacheki mechi ya Horoya na Raja?
horoya haitakuwa mteremko kwa Mkapa kama wanaSimba wengi wanavyodhani
Tutawaroga kuliko tulivyowahi Kuziroga Timu zingine zote Kubwa na Ngumu zilizokuja kucheza nasi Simba SC hapa kwa Mkapa nchini Tanzania na atafungwa nyingi na za Ajabu Ajabu hatoamini na hamtoamini nyote.
 
mkuu unacheki mechi ya Horoya na Raja?
horoya haitakuwa mteremko kwa Mkapa kama wanaSimba wengi wanavyodhani
Horoya, Vipers na Al Hilal wote wana timu zinazofanana. Defence zao ziko ok ila mbele hawana wafungaji wala mbinu za kutengeneza mashambulizi. Ukiwangalia hauoni goli watapataje.

Simba akianza na kikosi kama cha leo, Horoya na Vipers wanafungwa bila shida kwa Mkapa. Shida yangu ni Saido tu asianze na Chama.
 
Kwa hali ilivyo niseme tu rasmi nimeamini wachezaji wetu miili imekataa japo roho inataka mafanikio kwa timu

Mzamiru anashindwa kupress tu afunge anacheck ampasie mtu mwingine wakati mwenzake kabanwa ,
Chama wa kukimbia na mpira vile afu abutue kiwango kile kweli?

Tukasajili wachezaji zaidi kwa hali hii tutageuka Liverpool soon
Nadhani wachezaji wa Simba hawafanyi mazoezi magumu. Angalia video za mazoezi yao Bunju au hata wakiwa gym, ni nadra kuona wachezaji wanatoka hata jasho. Wakifika kwenye mechi unaona wanakuwa hoi. Wako relaxed mno.
 
Pamoja na ushindi wa leo lakini Simba chini ya Robertinho siwaelewi. Mpira gani wa kubutua butua tu? Toka lini Simba wameanza kucheza mpira wa long balls? Hivi kwa Horoya, ninavyowatizama muda huu na Raja, tutatoka kweli? Mbona naiona Simba ya hovyo sana wakati huu wakati wachezaji ni wale wale? Huyu mwalimu ana shida ya kifalsafa dhidi ya faksafa asili ya Simba. Tuombe Mungu abadilike lkn sioni tukiifunga Horoya kwa Mkapa kwa mpira wa leo dhidi ya Vipers.
Gemu ya horoya na Simba ni Simba ndio walikosa nafasi za wazi kumfunga horoya ,kiufupi horoya aliyeshindwa kumfunga vipers hawezi kumfunga Simba nyumbani hata nafsi yako inajua ni ukaidi TU.
 
Huyu the genius matope bana, ameshabadilika tayari na kuona moshi mweupe kwa mnyama.

Karibu tena kundini the citizen na mwananchi [emoji28][emoji28]
 
Nadhani wachezaji wa Simba hawafanyi mazoezi magumu. Angalia video za mazoezi yao Bunju au hata wakiwa gym, ni nadra kuona wachezaji wanatoka hata jasho. Wakifika kwenye mechi unaona wanakuwa hoi. Wako relaxed mno.
Umeandika Jambo la Ukweli kabisa Mkuu. Heko sana na Watu wa Simba SC ( walio na Timu ) walioko hapa JamiiForums wauchukue Ushauri wako huu mzuri na Waufanyie Kazi haraka mno.
 
Gemu ya horoya na Simba ni Simba ndio walikosa nafasi za wazi kumfunga horoya ,kiufupi horoya aliyeshindwa kumfunga vipers hawezi kumfunga Simba nyumbani hata nafsi yako inajua ni ukaidi TU.
Horoya alikuwa hatafuti ushindi kwa Vipers, atakuja pia kutafuta draw kwa Mkapa na Simba walivyo na washambuliaji butu hilo linawezekana
 
Back
Top Bottom