Mchumba
JF-Expert Member
- Jul 27, 2012
- 280
- 262
Serikali ya awamu ya tano chini ya Dr John Magufuli wakati ikipambana kuhakikisha nchi inakua kiuchumi kuna baadhi ya viongozi wa ovyo wao akili zao wanawazia nafasi za uongozi wao. Ni tarehe mbili mwezi wa saba tu mwaka huu Tanzania inafanikiwa kuingia kwenye uchumi wa kati wa chini ambapo tangu Tanzania ipate uhuru tulikuwa hatujawahi kufikia hatua hiyo.
Wakati Mwijage anatumbuliwa kwenye cheo cha uwaziri baadhi ya watu walijua alionewa lakini kwenye jimbo la Muleba Kaskazini siku hiyo ilikuwa ni ya nderemo na vificho kwa wananchi kutokana na kutumbuliwa kwake. Charles Mwijage ni wabunge ambao ni dhaifu lakini alibahatika kuaminiwa na serikali na kupewa majukumu makubwa ambayo hayaendani na uwezo wake. Ni waziri ambaye alishindwa kupafomu vizuri wilayani kwake wakati akinadi kampeni ya Tanzania ya viwanda nchini huku yeye mwenyewe anaua viwanda vinavyojengwa wilayani kwake kwa kuogopa kwamba watachukua nafasi ya ubunge.
Mwijage akili yako imechoka na uwezo wako umeishia hapo, achia nafasi kwa watu wengine wenye nguvu na maono. Ni aibu kuwa na mtu ambaye kamuangusha Rais wetu katika utendaji kazi. Umeshindwa kwendana na kasi yake waachie watakaoweza wafanye hiyo kazi. Sasa hivi umeishiwa hoja unakimbilia siasa za matusi, fitina na kuendekeza chuki kwa wananchi. Siasa za hivyo zimepitwa na wakati ndio maana kwa sasa unatumia nguvu nyingi kumwaga pesa ili watu wakupende. Uongo na ukweli havikai pamoja. Mwijage wewe ni muongo na huo uongo wako umekua ukijisifia kuwa ni propagandist.
Sasa hivi unalia na kulalamika kwamba watu wanataka hicho kiti cha ubunge, Miaka 10 uliyofanya yanatosha kuendelea kutaka hicho kiti ni kudhihirisha usemi wako uliozoea kusema kuwa lazima watakupa kura tena kutokana na ujinga wao. Watanzania siyo wajinga na hii nchi ni ya demokrasia lazima utoke waingie wengine hiki siyo kiti cha ufalme. Je kama Rais alikuamini na ukamuangusha je sasa hivi ndio kusema umepata mbadala wa matatizo yote.
Miaka 10 ni mingi sana kwako utakumbukwa kwa propaganda chafu ambazo zinarudisha nyuma maendeleo. Tumeingia kwenye uchumi wa kati hatutaki kurudi nyuma kama ilivyo kwenye dira ya taifa tunahitaji viongozi wabunifu na wenye fikra chanya kwa maendeleo ya watanzania.
Muleba `kaskazini ni kubwa kuliko Mwijage kuwa mpole tumia pension yako vizuri katika kustaafu kwako. Umewaumiza watu wengi kwa roho mbaya yako na watu wanaokuzunguka kwa kuangalia maslahi yako. Tunajua hauna uchungu na Muleba Kaskazini bali unataka kuendelea kujinufaisha kutokana na uchu wako wa madaraka. Watia nia ni wengi mwaka huu. Kwa taarifa yako hutaweza kupita kwa visiki vilivyopo Muleba `kaskazini.
Kama siku ya kuvunja bunge ulisahau kupiga picha pole sana. Imeishakula kwako mzee.
Wakati Mwijage anatumbuliwa kwenye cheo cha uwaziri baadhi ya watu walijua alionewa lakini kwenye jimbo la Muleba Kaskazini siku hiyo ilikuwa ni ya nderemo na vificho kwa wananchi kutokana na kutumbuliwa kwake. Charles Mwijage ni wabunge ambao ni dhaifu lakini alibahatika kuaminiwa na serikali na kupewa majukumu makubwa ambayo hayaendani na uwezo wake. Ni waziri ambaye alishindwa kupafomu vizuri wilayani kwake wakati akinadi kampeni ya Tanzania ya viwanda nchini huku yeye mwenyewe anaua viwanda vinavyojengwa wilayani kwake kwa kuogopa kwamba watachukua nafasi ya ubunge.
Mwijage akili yako imechoka na uwezo wako umeishia hapo, achia nafasi kwa watu wengine wenye nguvu na maono. Ni aibu kuwa na mtu ambaye kamuangusha Rais wetu katika utendaji kazi. Umeshindwa kwendana na kasi yake waachie watakaoweza wafanye hiyo kazi. Sasa hivi umeishiwa hoja unakimbilia siasa za matusi, fitina na kuendekeza chuki kwa wananchi. Siasa za hivyo zimepitwa na wakati ndio maana kwa sasa unatumia nguvu nyingi kumwaga pesa ili watu wakupende. Uongo na ukweli havikai pamoja. Mwijage wewe ni muongo na huo uongo wako umekua ukijisifia kuwa ni propagandist.
Sasa hivi unalia na kulalamika kwamba watu wanataka hicho kiti cha ubunge, Miaka 10 uliyofanya yanatosha kuendelea kutaka hicho kiti ni kudhihirisha usemi wako uliozoea kusema kuwa lazima watakupa kura tena kutokana na ujinga wao. Watanzania siyo wajinga na hii nchi ni ya demokrasia lazima utoke waingie wengine hiki siyo kiti cha ufalme. Je kama Rais alikuamini na ukamuangusha je sasa hivi ndio kusema umepata mbadala wa matatizo yote.
Miaka 10 ni mingi sana kwako utakumbukwa kwa propaganda chafu ambazo zinarudisha nyuma maendeleo. Tumeingia kwenye uchumi wa kati hatutaki kurudi nyuma kama ilivyo kwenye dira ya taifa tunahitaji viongozi wabunifu na wenye fikra chanya kwa maendeleo ya watanzania.
Muleba `kaskazini ni kubwa kuliko Mwijage kuwa mpole tumia pension yako vizuri katika kustaafu kwako. Umewaumiza watu wengi kwa roho mbaya yako na watu wanaokuzunguka kwa kuangalia maslahi yako. Tunajua hauna uchungu na Muleba Kaskazini bali unataka kuendelea kujinufaisha kutokana na uchu wako wa madaraka. Watia nia ni wengi mwaka huu. Kwa taarifa yako hutaweza kupita kwa visiki vilivyopo Muleba `kaskazini.
Kama siku ya kuvunja bunge ulisahau kupiga picha pole sana. Imeishakula kwako mzee.