Salamu sana. Na baada ya salamu je hujambo? Mimi sijambo kabisa.
Dhumuni la waraka huu ni kukupongeza kwa utendaji kazi wako. Ilikuwa jana 24/8/2017 ambapo katika mojawapo ya kijiji cha wilaya ya Mwanga wakazi wake walifanya kosa la kulisha mifugo kwenye eneo jipya ambalo serikali imeamua liwe hifadhi.
Mifugo yao ilikamatwa kwa kosa hilo. Kinachonifanya nikusifu Mkuu wa Wilaya ya Mwanga ni pale ulipofika eneo la tukio, ukaamua mgogoro huo ambao ulifanya maamuzi ambayo ni FAIR, hukuwapendelea wale wenye mifugo na wala hukuipendelea serikali, ulihakikisha haki inatendeka kwa pande zote mbili. Ahsante sana.
Nakuomba upange ratiba yako ya ziara uje hapo kijijini uongee na hao wananchi lakini katika masuala utakayoongea nao mojawapo uwakumbushe utunzaji wa mazingira na pia kuwasisitiza kuwa kuna maeneo ambayo hawaruhusiwi kulisha mifugo yao.
Kama uko JF utasoma huu ujumbe wangu, kama hauko hapa naamini kuna wapambe wako watakupa salamu zangu, na hata bosi wako mama Anna Mghwira yumo humu JF.
Ahsante JPM kutuletea jembe wilaya ya Mwanga, ila sasa nakuomba kale "kamsuguano" kako na DAS wako mkamalize ili muweze kusimamia vema wilaya ya Mwanga.
Sina mengi kwa leo, kalamu naweka chini
Wako mtiifu,
NAHUJA
mzaliwa wa kijiji hicho
Dhumuni la waraka huu ni kukupongeza kwa utendaji kazi wako. Ilikuwa jana 24/8/2017 ambapo katika mojawapo ya kijiji cha wilaya ya Mwanga wakazi wake walifanya kosa la kulisha mifugo kwenye eneo jipya ambalo serikali imeamua liwe hifadhi.
Mifugo yao ilikamatwa kwa kosa hilo. Kinachonifanya nikusifu Mkuu wa Wilaya ya Mwanga ni pale ulipofika eneo la tukio, ukaamua mgogoro huo ambao ulifanya maamuzi ambayo ni FAIR, hukuwapendelea wale wenye mifugo na wala hukuipendelea serikali, ulihakikisha haki inatendeka kwa pande zote mbili. Ahsante sana.
Nakuomba upange ratiba yako ya ziara uje hapo kijijini uongee na hao wananchi lakini katika masuala utakayoongea nao mojawapo uwakumbushe utunzaji wa mazingira na pia kuwasisitiza kuwa kuna maeneo ambayo hawaruhusiwi kulisha mifugo yao.
Kama uko JF utasoma huu ujumbe wangu, kama hauko hapa naamini kuna wapambe wako watakupa salamu zangu, na hata bosi wako mama Anna Mghwira yumo humu JF.
Ahsante JPM kutuletea jembe wilaya ya Mwanga, ila sasa nakuomba kale "kamsuguano" kako na DAS wako mkamalize ili muweze kusimamia vema wilaya ya Mwanga.
Sina mengi kwa leo, kalamu naweka chini
Wako mtiifu,
NAHUJA
mzaliwa wa kijiji hicho