Mr Dudumizi
JF-Expert Member
- Sep 9, 2020
- 7,799
- 14,215
Habari za asubuhi ndugu zang wa JF,
Ama baada ya salam naomba nielekee sasa kwenye mada yangu. Ndugu zangu wakati nchi yetu inalazimishwa kuingia katika mfumo wa vyama vingi na nchi za magharibi, serikali ya Tanzania chini ya raisi wa wakati huo mzee Rukhsa ilikataa mfumo huu kwa kuona kwamba ni wa hatari na wenye lengo la kuitumbukiza nchi yetu katika machafuko ya kisiasa kama zilivyotumbukia baadhi ya nchi zilizokimbilia kukuubali mfumo huo.
Kwa vile wananchi (bila kujua faida au hasara ya mfumo huu) waliuhitaji, na kupitia mashinikizo mbali mbali kutoka kwa nchi hizo za magharibi including na baba wa Taifa mwalimu Nyerere, serikali haikuwa na jinsi zaidi ya kukubaliana na mfumo huo kwa shingo upande. Lakini kabla ya kuukubali na kuupitisha mfumo huu serikali kupitia chama kilichokuwa kinatawala chini ya mwenyekiti wake mzee Ally Hassan Mwinyi, ilibidi wakae kwanza kikao cha dharura na faragha ili kuangalia namna watakavyo usimamia mfumo huo ili usije ukaleta madhara ya uvunjifu wa amani au vita katika nchi yetu.
Katika kikao hicho ndo ilipatikana idea au mawazo ya kuwa na watu wa mfumo ambao watakuwa wanapenyezwa kimya kimya katika vyama vya upinzani na hata tawala ili kujua mienendo na malengo ya vyama vyao hasa katika swala la amani, maendeleo na mshikamano wa Taifa letu lkn pia kuvuta mpunga kutoka katika nchi hizo za magharibi ili zisaidie kujenga shule, barabara, hospital nk. Baada ya kukubaliana na wazo hilo ndipo serikali ilipoukubali mfumo huo, na kuruhusu vyama vingi kuanzishwa kwa lengo la kuleta demokrasia, lkn yenye faida na manufaa ndan ya nchi.
Vyama vilipoanzishwa wazee wa kazi wakaingizwa kazini kusimamia kile walichoambiwa. Mwaka 95 NCCR kilikuwa juu sana lkn hakikuonesha sura ya kitaifa, kwahiyo wazee wa kazi wakaingia kazini na matokeo yake watu wakapigana viti katika mkutano wao wenyewe na kupelekea aliekuwa mwenyekiti wa chama hicho mh Augustino Mrema kuhamia chama kingine, na hapo ndio ukawa mwisho wa NCCR. Mwaka 2000 mpaka 2005 CUF ndio kilikuwa chama kikuu cha upinzani lkn macho kama kilivyokuwa NCCR, hakikuonesha kukomaa kupewa serikali hasa baada ya kugundulika kuwa chama hicho kina ukaribu zaidi na dini, wazee wa kazi wakaingia kazini chama hicho kikawa cha historia tu mpaka leo.
Baada ya hivyo vyama kuanguka, kikaja Chadema ambacho nacho hakikuonesha sura ya utaifa na kibaya zaidi kilijionesha kwamba kinaweza kupambana hata na serikali pale kinapohisi kuonewa. Chama hichi kilikuwa na vijana wengi ambao wengi wao hawakuonesha kujali chochote kuhusu amani ya nchi. Kilifanya maandamano mbali mbali, kilipambana na dola na kuzusha tuhuma mbali mbali ambazo zingine zilikuwa za kweli na zingine za uongo. Baada ya mwenendo huo uliotishia amani na usalama wa nchi, mwaka 2015 ndo wazee wa kazi wakaingizwa tena kazini ili kuangamiza na kumaliza kabisa fyoko fyoko zao. Na kwa vile chama hicho kilikuwa na mchanganyiko wa wasomi na wasio wasomi basi ilibidi serikali ije na mbinu za kisomi kwa kutengeneza mazingira yakayowaingiza mkenge walengwa wao.
Mbinu hizi zilihitaji pesa na ugomvi wa hapa na pale ili kurahisisha kazi. Na kweli ugomvi ukatengenezwa katika ya mwenyekiti wa chama tawala na mkuu wa nchi wa enzi hizo dhidi ya swahiba wake wa miaka mingi. Na kweli mbinu hiyo pamoja na pesa iliyotaarishwa na wenye mipango iliwezesha kuwaingiza kingi viongozi wa upinzani ambao waliweka mbele tamaa ya pesa, na uroho wa kushika madara. Katika hilo wazee wa kazi walifanikiwa kuisambaratisha ngome iliyokuwa inaitwa UKAWA na kuwaacha vipande vipande wasioaminiana.
Yan Chadema haiamini NCCR na NCCR haiamini Chadema. Hapo hatujazungumzia madiwani, wabunge na zile nguvu walizokuwa nazo katika kukabiliana na vyombo vya dola. Mwaka 2020 anaeitwa kachero mbobezi na yeye alipewa test ndogo tu ya kukasambaratisha kachama kadogo na kenye umri mfupi toka kaanzishwe lkn cha kushangaza mbobezi alishindwa mapema sana kumalizia kazi na kibaya zaidi alishindwa hata kuondoka na mwenyekiti wa serikali za mitaa hata mmoja.
Tofauti na mwenzake ambae alifanikiwa kuusambaratisha umoja wa ukawa na pia aliondoka na mamia ya madiwani na wabunge huku akiwaacha wapinzani wenyewe wakishikana uchawi wasiaminiane hata wenyewe kwa wenyewe ndan ya vyama vyao. Hizi ndio siasa za Tanzania bwana kama huzijui unaweza kuingizwa chaka na wajinga wajinga.
Ama baada ya salam naomba nielekee sasa kwenye mada yangu. Ndugu zangu wakati nchi yetu inalazimishwa kuingia katika mfumo wa vyama vingi na nchi za magharibi, serikali ya Tanzania chini ya raisi wa wakati huo mzee Rukhsa ilikataa mfumo huu kwa kuona kwamba ni wa hatari na wenye lengo la kuitumbukiza nchi yetu katika machafuko ya kisiasa kama zilivyotumbukia baadhi ya nchi zilizokimbilia kukuubali mfumo huo.
Kwa vile wananchi (bila kujua faida au hasara ya mfumo huu) waliuhitaji, na kupitia mashinikizo mbali mbali kutoka kwa nchi hizo za magharibi including na baba wa Taifa mwalimu Nyerere, serikali haikuwa na jinsi zaidi ya kukubaliana na mfumo huo kwa shingo upande. Lakini kabla ya kuukubali na kuupitisha mfumo huu serikali kupitia chama kilichokuwa kinatawala chini ya mwenyekiti wake mzee Ally Hassan Mwinyi, ilibidi wakae kwanza kikao cha dharura na faragha ili kuangalia namna watakavyo usimamia mfumo huo ili usije ukaleta madhara ya uvunjifu wa amani au vita katika nchi yetu.
Katika kikao hicho ndo ilipatikana idea au mawazo ya kuwa na watu wa mfumo ambao watakuwa wanapenyezwa kimya kimya katika vyama vya upinzani na hata tawala ili kujua mienendo na malengo ya vyama vyao hasa katika swala la amani, maendeleo na mshikamano wa Taifa letu lkn pia kuvuta mpunga kutoka katika nchi hizo za magharibi ili zisaidie kujenga shule, barabara, hospital nk. Baada ya kukubaliana na wazo hilo ndipo serikali ilipoukubali mfumo huo, na kuruhusu vyama vingi kuanzishwa kwa lengo la kuleta demokrasia, lkn yenye faida na manufaa ndan ya nchi.
Vyama vilipoanzishwa wazee wa kazi wakaingizwa kazini kusimamia kile walichoambiwa. Mwaka 95 NCCR kilikuwa juu sana lkn hakikuonesha sura ya kitaifa, kwahiyo wazee wa kazi wakaingia kazini na matokeo yake watu wakapigana viti katika mkutano wao wenyewe na kupelekea aliekuwa mwenyekiti wa chama hicho mh Augustino Mrema kuhamia chama kingine, na hapo ndio ukawa mwisho wa NCCR. Mwaka 2000 mpaka 2005 CUF ndio kilikuwa chama kikuu cha upinzani lkn macho kama kilivyokuwa NCCR, hakikuonesha kukomaa kupewa serikali hasa baada ya kugundulika kuwa chama hicho kina ukaribu zaidi na dini, wazee wa kazi wakaingia kazini chama hicho kikawa cha historia tu mpaka leo.
Baada ya hivyo vyama kuanguka, kikaja Chadema ambacho nacho hakikuonesha sura ya utaifa na kibaya zaidi kilijionesha kwamba kinaweza kupambana hata na serikali pale kinapohisi kuonewa. Chama hichi kilikuwa na vijana wengi ambao wengi wao hawakuonesha kujali chochote kuhusu amani ya nchi. Kilifanya maandamano mbali mbali, kilipambana na dola na kuzusha tuhuma mbali mbali ambazo zingine zilikuwa za kweli na zingine za uongo. Baada ya mwenendo huo uliotishia amani na usalama wa nchi, mwaka 2015 ndo wazee wa kazi wakaingizwa tena kazini ili kuangamiza na kumaliza kabisa fyoko fyoko zao. Na kwa vile chama hicho kilikuwa na mchanganyiko wa wasomi na wasio wasomi basi ilibidi serikali ije na mbinu za kisomi kwa kutengeneza mazingira yakayowaingiza mkenge walengwa wao.
Mbinu hizi zilihitaji pesa na ugomvi wa hapa na pale ili kurahisisha kazi. Na kweli ugomvi ukatengenezwa katika ya mwenyekiti wa chama tawala na mkuu wa nchi wa enzi hizo dhidi ya swahiba wake wa miaka mingi. Na kweli mbinu hiyo pamoja na pesa iliyotaarishwa na wenye mipango iliwezesha kuwaingiza kingi viongozi wa upinzani ambao waliweka mbele tamaa ya pesa, na uroho wa kushika madara. Katika hilo wazee wa kazi walifanikiwa kuisambaratisha ngome iliyokuwa inaitwa UKAWA na kuwaacha vipande vipande wasioaminiana.
Yan Chadema haiamini NCCR na NCCR haiamini Chadema. Hapo hatujazungumzia madiwani, wabunge na zile nguvu walizokuwa nazo katika kukabiliana na vyombo vya dola. Mwaka 2020 anaeitwa kachero mbobezi na yeye alipewa test ndogo tu ya kukasambaratisha kachama kadogo na kenye umri mfupi toka kaanzishwe lkn cha kushangaza mbobezi alishindwa mapema sana kumalizia kazi na kibaya zaidi alishindwa hata kuondoka na mwenyekiti wa serikali za mitaa hata mmoja.
Tofauti na mwenzake ambae alifanikiwa kuusambaratisha umoja wa ukawa na pia aliondoka na mamia ya madiwani na wabunge huku akiwaacha wapinzani wenyewe wakishikana uchawi wasiaminiane hata wenyewe kwa wenyewe ndan ya vyama vyao. Hizi ndio siasa za Tanzania bwana kama huzijui unaweza kuingizwa chaka na wajinga wajinga.