Uchaguzi 2020 Kwani CCM mlitakaje!? Lissu ana kosa gani?

TAMKO

JF-Expert Member
Joined
Oct 11, 2011
Posts
1,090
Reaction score
763
Ajabu Sana, CCM na Serikali mlitakaje kwani! Kwamba Lissu asimame Kwenye Majukwaa kama Paroko anaye ongoza Misa au Kama msanii! Mlitakaje ndugu zangu!

Lissu Yuko kwenye Battle Field , Anatafuta anacho Kitafuta, anapigana Vita, Kwenye Vita hatuchaguliani Siraha, Chochote Cha Kuua na Kupiga Huwa Kinakusanywa Lengo Adui Auawe. Sasa Cha Ajabu Kipi wana CCM na Serikali , Unajua sometime Tuwe tunavitumia vichwa Vyetu kuwaza kabla ya Kutenda. Tume Kumwita Lissu ni kumwongezea maillage tu.

Nimetembea mikutano kadhaa ya wagombea Urais CCM na CHADEMA. Nimeona Mambo Kadhaa kama Dondoo. Katika Mikutano Yote Niliyo Tembelea CCM inajaza watu Wengi sana Kuliko Chadema Lakini Kuna Namna ya Akili CHADEMA wanafanya. CCM inatenga Mikutano yao kwenye Mauwanja Makubwa sana watu ni wengi Lakini hawaujazi uwanja.

CHADEMA wanachagua Viwanja Vidogo na Wanavijaza.. Mgombea wa CCM anazunguka na Convoy yenye Full President Protocal (Of Course lazima Iwe Hivyo Kwa Sababu still Bado ni Rais wa Nchi) convoy ambayo haimpi Nafasi ya Kujichanganya na raia.. Lissu anatumia Ujanja, Anapita katikati ya UWANJA wakati anaingia na wakati anatoka, Ile movement ya watu inachukuliwa Picha na ikienda Mitandoni inaleta HABARI ILIYO SHIBA, Ni Akili na Ujanja na Mbinu.

Mgombea wa CCM anatoa Takwimu Za Kweli za Yale Aliyo Yafanya na Yale Atakayo Yafanya. Mgombea wa CCM anatoa Takwimu Za Bilions and Trillions Wananchi wanao msikiliza Mfukoni wamechacha Ingawa Maelezo Yake ni Ya kweli. Uwezo wa Wananchi Kuchuja kwamba Mzee anatutengenezea Daraja la Maendeleo in future Days Hawana, wao wakila Kwa siku moja inatosha. Sasa akija Lissu, Haangalii Sura ya mtu, Matatizo Yote ya eneo Husika anakusanya na Kujazia Chumvi Za Kutosha anawamwagia wananchi. Anamimina Ahadi kwamba zinawezekana au Haziwezekani Hilo hajali sana Lengo lake akoshe mioyo ya Wananchi POTELEA MBALi ikitokea amekuwa Raisi Atajua Cha Kufanya mbele ya safari.

Lissu anamimina Maneno Yoyote, ya kweli ya Uongo Mwaga tu, Asingizie Serikali, Asingizie Chama, asingizie mkeo au mumeo Potelea mbali Maadam anawin mioyo ya watu. Mimi sioni KOSA Katika Hili maana Ndio MAANA YA VITA. Vita ni Vita.Chochote Cha kumpigia adui TUMIA ili USHINDE!

Ukichukulia siasa hizi Za Vyama Vingi Hazina mifumo zinajiendeaga tu, na Hii ni shida sana, Ndio maana ya Uhitaji wa KATIBA mpya Haya Yote Yangenyooshwa. Kuna pahala Lissu alitema Takwimu Za Masheick walio Fungwa na Serikali Hii mikoani kiasi Hata wana Chadema walio Kuwa Karibu Yangu waliguna wakasema Hapo amefika Mbali. Hawazi Baada ya Uchaguzi Maisha Yapp!

CCM wao wamebakia Kulalamika, wapi UVCCM, wapi Wagombea Ubunge/ Udiwani Kama wanaona Jamaa Kaongea Uongo Wapite wao Kuusahihisha sio Kusimama kama masanamu wakitegemea Serikali Iwatetee wakati Na serikali nayo inapigwa nayo inajitetea Kivyake!

SIASA NI VITA, Wakati wa CCM kutegemea Hela Ifanye Kazi UMEPITA! Kila mwana CCM analalamika kwamba Uchaguzi Mwaka huu hela Hakuna , ni TABIA MBAYA.! Mkigoma Hela Hakuna Chama kitashikiliwa na Nani?

Rais MAGUFULI ni Rais Mkweli, Mwazi, Mchapakazi Ingawa wanachama wengi Wa CCM ni Walimia Matumbo Yao.
 
CCM hawana la ziada. Madaraja, mabarabara... watu wameyasikia kwa miaka 5 sasa. Siyo habari tena. Habari ni maisha ya watu sasa, haki zao.... CCM badala ya kujibu hoja, wamebaki kusema Lissu ni beberu, atauza madini (kana kwamba wao hawauzi), Lisu siyo raia wa Tanzania... Bahati nzuri Singida iko katikati ya Tanzania. Angekuwa anatoka Kigoma, Uhamiaji wangekuwa wameshaomba vyeti vya bibi na babu wa bibi na babu yake.

CCM wajibu hoja. Hawajibu hoja zinazotolewa za ufisadi, maisha magumu, nk. Yaani wame-give up. Wanalazimisha zahama sana - TL asimamishwe kufanya kampeni ama aondolewe katikati ya kampeni. Wanaona kuwa hata Tume kumtangaza Magufuli mshindi 28 Oktoba 2020, haitatosha. Wanataka wamtoe kabla ya tarehe hiyo!

Litakuwa kosa kubwa sana litakalo haribu amani ya nchi yetu. Katika maisha kuna kushinda na kushindwa. CCM wakubali na waweke neno "kushindwa" pia katika kamusi yao. Na maisha yataendelea. KANU (Moi), Kaunda (Zambia), MCP (Kamuzu Banda)... walikubali na maisha yakaendelea.

CCM ijiandae kisaikolojia. Kama si 2020, basi kuna mwaka utakuja wataondolewa. Yale maneno ya miaka 100 hayana uhalisia.
 
Mleta mada unataka kutuambia leo hii Lissu akitaka kuujaza ule uwanja wa uhuru au wa taifa atashindwa? binafsi naamini kabisa hashindwi.

CCM wanamzuia Lissu kufanya kampeni zake kwenye hivyo viwanja kwasababu vingi kati ya hivyo wamejimilikisha, wamevigeuza mali yao binafsi wakati vilipatikana kwa jasho la watanzania wote bila kujali itikadi zao.
 
Ajabu Sana, CCM na Serikali mlitakaje kwani! Kwamba Lissu asimame Kwenye Majukwaa kama Paroko anaye ongoza Misa au Kama msanii! Mlitakaje ndugu zangu!..
Tume ya uchaguzi imemwongezea Lissu political milage
 
Wananchi hawawezi chagua matapeli, na kuwaacha Wazalendo. Magufuli tano tena.
 
NEC na ofisi ya msajili wa vyama vya sasa wanataka kuwachagulia watanzania viongozi wanaowataka. Safari hii wameshika pabaya walizoea miaka yote wanasimamishwa wanaccm kugombea urais Kupitia vyama vya upinzani but mwaka huu ni wa tofauti.
 
Tume ya uchaguzi imemwongezea Lissu political milage
Hapo ndipo wanapoharibu, mahera aachane na kufuata hotuba za wagombea,,itazidi tu kumjenga lisu,watu wataona lisu anasakamwa,atapata kura za huruma.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…