Kwani mtandao wa Airtel makao yenu makuu ni Ukraine?

Mkumbwa Jr

JF-Expert Member
Joined
Mar 23, 2016
Posts
2,668
Reaction score
3,751
Kwa muda usiopungua siku tano sasa mtandao wa Airtel umesababisha usumbufu mkubwa kwa baadhi ya watumiaji wake. Simu za mtandao huo hazitoki na sanasana mteja unaweza ukaambiwa namba unayopiga haiwezi kuunganishwa kwasasa
Wateja wanahangaika na mawasiliano hamna. Vifurushi vyenu vinakata maratu muda unapokwisha bila hata kutumika kutokana na tatizo la kimtandao. Hii sio sawa.

Nikaona niulize au Airtel imeathiriwa na oparesheni ya kijeshi inayoendelea Ukraine? Au mawasiliano yao yamepata mtikisiko kwa maana kwamba ndio chanzo chao kikuu cha mawasiliano huko?

Airtel kama nitimu yenu ya ufundi iliyopo,kazi imewaelemea ongezeni nguvu kazi.
NB. Angalieni utaratibu wa kuwafidia wateja wenu siku ambazo mtandao wenu umesinzia na mawasiliano hayakuepo
Airtel poleni kwa kuathiriwa na oparesheni ya kijeshi inayofanywa na Urusi dhidi ya Ukraine
 
Naomba kulitilia mkazo kwenye hili kwa hali ilivyo sasa hivi kwakweli hali imekua mbaya sana mnakuta hakuna masikilizano mazuri badala yake unatakiwa ukate simu na upige tena hili limekuwa ni jambo la mara kwa mara mpk Inaudhiiiiiiiiii
 
๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚itakua
 
Kwa sababu kuna vita
 
Pengine wale wataalam wabobezi waliokuwepo awali wamepata ajira mpya "inayolipa" huko Ukraine. Waliopo sasa hawana uzoefu ni direct from school.
 
Karibu Vodacom iliyopo Russia
 
Nikituma hela naambiwa salio halitoshi.nilidhani ni tatizo la simu yangu
 
Nikituma hela naambiwa salio halitoshi.nilidhani ni tatizo la simu yangu
Nikihitaji huduma ya TIMIZA naambiwa Endelea kutumia Airtel money zaidi. Nilidhani huduma imesitishwa kwangu.
 
Inawezekana hili ulilohisi ni kweli.
 
Kama ndivyo au ni vinginevyo basi waweke mambo wazi. Wazingatie kwamba Wateja wao ndo wanaowawezesha wao(airtel) waendelee kuwapo hapo. La sivyo, waiuze Kampuni kwa wanaomudu (historia inajirudia).
 
Mitandao ya kidwanzi kama huo na ule mwingine wa jaza ujazwe siwezi kutumia hata kwa bunduki. Ni mitandao ya hovyo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ