Kwani shida kwenye umeme wetu ni nini?

Kwani shida kwenye umeme wetu ni nini?

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2021
Posts
9,189
Reaction score
16,128
Mwezi wa 11 walisema ni kawaida kuwa na mgao kila mwaka. Hadi Zitto akawaunga mkono. Kama mwezi wa kumi na mbili Wakasema tena kuwa ndani ya siku mbili watatoa majibu na kukomesha mgao. Mwezi huu wakasema mgao mpaka tarehe kumi utakuwa historia lakini wakasema hakuna haja upo wa kutosha.

Maneno yote hayo, na mvua zote hizi lakini bado umeme ni shida. Wameshakata saa hizi. Kazi yangu imeshakwama. Tupate majibu ya ukweli na si maneno mengi. Shida ni nini kwenye umeme?
 
Mvua zote hizi?

Mvua zenyewe za kudunduliza unaona nyingi?

Sorry siwaungi mkono lakin mvua hizi ni kidogo sana sana.

Kunahitajika source nyingine ya kuzalisha umeme. Si kutegemea maji ambayo yanakuja kwa mvua za msimu
 
Mvua zote hizi?
Mvua zenyewe za kudunduliza unaona nyingi?

Sorry siwaungi mkono lakin mvua hizi ni kidogo sana sana.
Kunahitajika source nyingine ya kuzalisha umeme. Si kutegemea maji ambayo yanakuja kwa mvua za msimu
Nyanda za juu kusini, kunakolisha mabwawa mvua zimepiga sana. Lakini vyovyote, tunataka majibu ya uhakika na si kutupiga fiksi na maneno mengi mengi.
 
Nyanda za juu kusini, kunakolisha mabwawa mvua zimepiga sana. Lakini vyovyote, tunataka majibu ya uhakika na si kutupiga fiksi na maneno mengi mengi.
"Tunataka majibu" ww na nani? Unaichimba biti serikali?
Sikutishi but unaeza andika barua kwa waziri au wizara husika maana ni haki yako kupata taarifa. Si kulazimisha

Iko hivi nyanda za juu zimepiga ndio? But kiasi gani?
Imejaza mabwawa kwa kiasi gani? Volume iliyopo sahizi inaweza generate umeme kwa muda gani?

Shida ni kuwa hatuna chanzo kingine zaidi ya umeme wa maji tokea enzi za uhuru.
Ndio maana maji ya kipungua kidogo mgao..matatizo ya umeme yanaanza. Lazima tutoke huko else tutatalalamika mpaka kihama.

Miaka nenda miaka rudi, tumeshindwa hata kuweka miundombinu ya umeme na upepo? Umeme wa gas? Umeme wa nuclear?
 
"Tunataka majibu" ww na nani? Unaichimba biti serikali?
Sikutishi but unaeza andika barua kwa waziri au wizara husika maana ni haki yako kupata taarifa. Si kulazimisha

Iko hivi nyanda za juu zimepiga ndio? But kiasi gani?
Imejaza mabwawa kwa kiasi gani? Volume iliyopo sahizi inaweza generate umeme kwa muda gani?

Shida ni kuwa hatuna chanzo kingine zaidi ya umeme wa maji tokea enzi za uhuru.
Ndio maana maji ya kipungua kidogo mgao..matatizo ya umeme yanaanza. Lazima tutoke huko else tutatalalamika mpaka kihama.

Miaka nenda miaka rudi, tumeshindwa hata kuweka miundombinu ya umeme na upepo? Umeme wa gas? Umeme wa nuclear?
Serikali kuanzia rais, mawaziri na watumishi wote wameajiriwa na wananchi. Nikiwemo mimi. Ndiyo maana ya jamhuri. So nikiwa kama muajiri nataka majibu ya kueleweka na kwa lazima.
 
Serikali kuanzia rais, mawaziri na watumishi wote wameajiriwa na wananchi. Nikiwemo mimi. Ndiyo maana ya jamhuri. So nikiwa kama muajiri nataka majibu ya kueleweka na kwa lazima.
Haya nenda ikulu na wizara husika kawaamrishe wakupe hizo taarifa. Hapa jf si sehemu sahihi mana hutopata kitu.

Ni vema ukawafuata wenyewe ukawaambia. Halaf uaikilize majibu yao.
 
Mwezi wa 11 walisema ni kawaida kuwa na mgao kila mwaka. Hadi Zitto akawaunga mkono. Kama mwezi wa kumi na mbili Wakasema tena kuwa ndani ya siku mbili watatoa majibu na kukomesha mgao. Mwezi huu wakasema mgao mpaka tarehe kumi utakuwa historia lakini wakasema hakuna haja upo wa kutosha.

Maneno yote hayo, na mvua zote hizi lakini bado umeme ni shida. Wameshakata saa hizi. Kazi yangu imeshakwama. Tupate majibu ya ukweli na si maneno mengi. Shida ni nini kwenye umeme?
sababu za kukatika kwa umeme ni nyingi sana mzee.
 
Mimi wala silaumu serikali, tunajilaumu sisi kwa kufanywa wajinga (na kiukweli sisi ni wajinga) kiasi kwamba kwa miaka yoote hiyo tunaambiwa hadithi zile zile na bado tunaziamini eti kwa sababu tu wasimuliaji hadithi ni tofauti
 
Back
Top Bottom