Kwanini ajenda ya kupanda miti ni muhimu sana kwa sasa

Kwanini ajenda ya kupanda miti ni muhimu sana kwa sasa

N'yadikwa

JF-Expert Member
Joined
Aug 10, 2014
Posts
7,427
Reaction score
10,905
Hali ya upungufu mkubwa wa mvua imeshatukabili, maeneo mengi ya nchi yetu January hii ya 2022 yanashuhudia uhaba mkubwa wa mvua.

Jitihada zetu kama Tanzania kwenye upandaji na utunzaji miti bado sio za kiwango cha kuridhisha.

Uvunaji miti holela kwa ajili ya makaa na kuandaa mashamba mapya unatuondolea uoto maeneo mengi.

NINI TUFANYE
Ifanyike kampeni ya kitaifa ya upandaji miti kwa angalau miaka mitatu mfululizo kwa ushirikiano wa:-
  • Wananchi
  • Serikali Kuu (Wizara ya mazingira)
  • Local governments
  • JKT

Tupande miti angalau miti Milioni Tano kila Halmashauri kwa mwaka kwa mfululizo wa miaka mitatu ili tupate mvua. Hali ilivyo haitii moyo kabisa.

Aidha tuwezeshe uzalishaji mkaa wa kupikia kutoka teknolojia ya taka tuachane na makaa ya miti...kama italazimika iwe kwa vibali maalum kwa mapori yaliyotengwa na kwa masharti ya KATA MTI PANDA MTI.

Wizara ya Mazingira kwa ushirikiano na TAMISEMI ije na Kampeni ya kitaifa itakayosimamiwa kwa dhati kila kaya iwajibike kupanda miti michache na kuitunza.

Tusanuke hali si nzuri.
 
Ni mawazo mazuri lakini haya mawazo yako hayapo kwenye vichwa vya viongozi hawa wa serikali ya CCM,sasahivi agenda yao ni kukopa pesa na uchaguzi wa 2025
Simanjiro huko mifugo zaidi ya 62,000 imekufa kwa ukame ila wenye mamlaka hata hawashtuki
 
Ni mawazo mazuri lakini haya mawazo yako hayapo kwenye vichwa vya viongozi hawa wa serikali ya CCM,sasahivi agenda yao ni kukopa pesa na uchaguzi wa 2025
Simanjiro huko mifugo zaidi ya 62,000 imekufa kwa ukame ila wenye mamlaka hata hawashtuki
Wanaccm wangapi wamekufa?
 
Hizo ni ajenda za mabeberu wanataka tuishi maporini ndio maana tuliamua kukata miti mingi wakati wa kuanza ujenzi wa Stiglaz Jogi🤣🤸🐒
 
Washushe gharama za umeme na gesi kwa Matumizi ya majumbani tofauti na hapo mtawataka watu ubaya
 
Ukiwa unaenda Tabora, barabarani Mpya kutoka dodoma - singida(sikumbuki jina vizuri), kuna mapori mkubwa ya asili. Watu wamehamia wanakata miti kama vile hakuna serikali.
Unakuta nyumba ndogo ya udongo jamaa amefyeka ekari zaidi ya 10 kachomoa mkaa, na hana mipango ya kulima. Muda sio mrefu Tabora itakuwa kama singida na Dodoma kwa ukame.
 
Ukiwa unaenda Tabora, barabarani Mpya kutoka dodoma - singida(sikumbuki jina vizuri), kuna mapori mkubwa ya asili. Watu wamehamia wanakata miti kama vile hakuna serikali.
Unakuta nyumba ndogo ya udongo jamaa amefyeka ekari zaidi ya 10 kachomoa mkaa, na hana mipango ya kulima. Muda sio mrefu Tabora itakuwa kama singida na Dodoma kwa ukame.
Hii ni hatari sana. Bila shaka mamlaka zinakuona. Kuna siku nilikuwa natoka Tabora wale jamaa wanaotega vigunia barabarani huwa wanakaa kimachalemachale wakiona Land rover wanakimbia mbio za mbwa mwizi...inaonekana kazi ya kuwadhibiti nayo sio pevu...ila tuna hatari sana tusipolichukua suala la utunzaji miti kwa dhati. TUACHE VISINGIZIO tulinde miti.
 
Hali ya upungufu mkubwa wa mvua imeshatukabili, maeneo mengi ya nchi yetu January hii ya 2022 yanashuhudia uhaba mkubwa wa mvua.

Jitihada zetu kama Tanzania kwenye upandaji na utunzaji miti bado sio za kiwango cha kuridhisha.

Uvunaji miti holela kwa ajili ya makaa na kuandaa mashamba mapya unatuondolea uoto maeneo mengi.

NINI TUFANYE
Ifanyike kampeni ya kitaifa ya upandaji miti kwa angalau miaka mitatu mfululizo kwa ushirikiano wa:-
  • Wananchi
  • Serikali Kuu (Wizara ya mazingira)
  • Local governments
  • JKT

Tupande miti angalau miti Milioni Tano kila Halmashauri kwa mwaka kwa mfululizo wa miaka mitatu ili tupate mvua. Hali ilivyo haitii moyo kabisa.

Aidha tuwezeshe uzalishaji mkaa wa kupikia kutoka teknolojia ya taka tuachane na makaa ya miti...kama italazimika iwe kwa vibali maalum kwa mapori yaliyotengwa na kwa masharti ya KATA MTI PANDA MTI.

Wizara ya Mazingira kwa ushirikiano na TAMISEMI ije na Kampeni ya kitaifa itakayosimamiwa kwa dhati kila kaya iwajibike kupanda miti michache na kuitunza.

Tusanuke hali si nzuri.
Kuna Uzi humu JF nimeweka natafuta maeneo nipande miti. Mimi nitachuma matunda tu miti nitaiacha isaidie kwen carbon sequestration. Niliongea na mwenyekiti wa serikali ya mtaa ninapoishi hana idea yoyote aliyonipa!!
 
Hali ya upungufu mkubwa wa mvua imeshatukabili, maeneo mengi ya nchi yetu January hii ya 2022 yanashuhudia uhaba mkubwa wa mvua.

Jitihada zetu kama Tanzania kwenye upandaji na utunzaji miti bado sio za kiwango cha kuridhisha.

Uvunaji miti holela kwa ajili ya makaa na kuandaa mashamba mapya unatuondolea uoto maeneo mengi.

NINI TUFANYE
Ifanyike kampeni ya kitaifa ya upandaji miti kwa angalau miaka mitatu mfululizo kwa ushirikiano wa:-
  • Wananchi
  • Serikali Kuu (Wizara ya mazingira)
  • Local governments
  • JKT

Tupande miti angalau miti Milioni Tano kila Halmashauri kwa mwaka kwa mfululizo wa miaka mitatu ili tupate mvua. Hali ilivyo haitii moyo kabisa.

Aidha tuwezeshe uzalishaji mkaa wa kupikia kutoka teknolojia ya taka tuachane na makaa ya miti...kama italazimika iwe kwa vibali maalum kwa mapori yaliyotengwa na kwa masharti ya KATA MTI PANDA MTI.

Wizara ya Mazingira kwa ushirikiano na TAMISEMI ije na Kampeni ya kitaifa itakayosimamiwa kwa dhati kila kaya iwajibike kupanda miti michache na kuitunza.

Tusanuke hali si nzuri.
Unajua ubaya ni kwamba misitu ya asili inakuwa na combination ya thousands of plant species ndani yake tofauti na misitu ya kupanda ambayo inakuwa na miti jamii moja. Msitu kama wa Amazon bado hawajaweza kujua species zote zilizomo. Wanadai kuna mimea hata haijawahi gunduliwa
 
Washushe gharama za umeme na gesi kwa Matumizi ya majumbani tofauti na hapo mtawataka watu ubaya
Hii ni kweli, kitu kinacho ongoza kwa ukataji miti ni shughuri za uchomaji mkaa maana wanakata kuanzia mti mdogo had mkubwa
 
Back
Top Bottom