Kwanini baadhi ya media za Tanzania hawampendi msanii Diamond?

Naseeb Abdul ana dharau sana. alishawahi kusema hahitaji media yeyote . Media wakikuona una maringo hawakusupport kwa lolote
 
Naseeb Abdul ana dharau sana. alishawahi kusema hahitaji media yeyote . Media wakikuona una maringo hawakusupport kwa lolote
Ile kauli yake watu mliitafsiri vibaya makusudi tu kisa kasema diamond, lakini angesema msanii mwingine isingekuwa tabu.
Na alichosema ni ukweli mtupu, akiamka asubuhi akaweka video mpya youtube, then akaenda kwenye page yake ya instagram akaandika kuwa karelease wimbo mpya, huo wimbo utasambaa na utaukuta mtaani hata kama hajaupeleka redioni.
Huo ndiyo ukweli lakini kwakuwa hatupendi kusikia ukweli na EA radio walikuwa na bifu naye kisa hakushiriki tuzo zao basi wakaikuza kauli hiyo ionekane ana dharau.
 
Tuzo anazopata ni zile za kwenye Kitchen party hua media hawanaga Shobo na Tuzo hizo
 
Its obvious... inaonekana. Natazama sana taarifa mbalimbali za TVs hawakuwa na time na hiyo kitu. Hata ikitokea naona inakuwa kama "by the way"

Umeshawahi kumuona Diamond kapeleka busha lake channel ten ,star tv ,itv / eatv ,au hata azam tv? zaidi ya kutwa kushinda clouds fm /tv? Hao hao clouds anakoshinda wanatosha kutangaza habari zake .

Hata tangazo lake la Diamond karanga lipo clouds tu na halipo vyombo vingine vya habari .Hapo ndo ujue Diamond kaamua mwenyewe kuvitenga vituo vingine vya habari na kuamini clouds ndo baba na mama ake
 
Kuna asilimia kubwa sana ya wabongo wengi ni wanafiki,wivu,fitna. Wafata mkumbo ktk kila hoja yenye asili ya chuki,na kuoneana here that's why tuko nyuma ktk kila kitu
 
hongereni wote mnaomjadili platnamz badala y kukaa kufanya mambo y maana mnakalia kumjafili mtu anaestrugle n kuitumia akili yake kujitafutia tafuta chako uwe juu then utaona Kama utapendwa na kila mtu ndio uje JF kuanza kumjadili binaadam mwenzio kwan ww umekamilika??
 
ukae ukijua media ndio ilimfanya huyo dogo atoke. kuna ma underground kama mia na hawatoki yeye media ilimbeba sana leo anasema hahitaji? basi msililie media impe support aaachane na media afanye mwenyewe kwani shida nini? hamna media inayomhitaji diamond na wakiamua kutomoa support ni sababu zao binafsi huwezi ingia maamuzi ya biashara binafsi
 
Hazijatufikia ndio kwanza unatuambia. Labda haraka haraka na wenzetu wa uhuru, mzalendo na deile nyuzi wanazo.
 
Ulishawahi kumsikia yeye binafsi akilalamika kuwa media hazimsupport wala akilia?
Toka waache piga nyimbo zake hao ea radio na tv kashuka?
Kwani ni mara ya kwanza kuacha kupiga nyimbo zake?
Ile kauli waliichukulia tofauti na yeye alivyomaanisha na makusudi kabisa ndiyo maana hujasikia kituo kingine kikishikia bango statement yake zaidi ya ea tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…