Last Seen
JF-Expert Member
- Jun 7, 2013
- 229
- 566
Mambo vipi wanajamvi?
Nimewaza Mara kadhaa kuhusu bidhaa zinazoletwa sokoni na Bwana Chibu Dangote kwa nini hazidumu katika soko?
Chibu ni kijana mpambanaji mwenye uchu wa mafanikio makubwa na amethubutu kuwekeza ndani na nje ya Muziki wake, ametoa ajira kwa vijana kadhaa. Lakini swali moja ninalijiuliza ni kwa nini bidhaa zake zinakufa na kupotea katika soko baada ya muda mfupi?
Tumeshuhudia akizindua Diamond Karanga, wasafi.com, Chibu perfume na zote hizi hazipo sokoni au hazalishi tena bidhaa hizo (biashara imebuma).
Na miaka kadhaa nyuma amefungua Kituo cha Runinga na Redio ambavyo vilipokelewa kwa hamasa kubwa na wafuasi wake, lakini kwa upande mwingine wamekuwa wakilalamikiwa kurusha maudhui yasiofaa na mara kadhaa wamekutana na rungu la TCRA. Je, Wasafi Media itapotea kama biashara zake zilizopita?
Wasafi bet ni biashara ingine aliyoitambulisha hivi karibuni je, itahimili ushindani dhidi ya kampuni zingine za kubashiri?
Mwisho, Mimi sio mtalamu wa biashara na nngependa kujua nini inachangia kufeli kwa bidhaa zake nyingi, nini ushauri wako kwa Baba
Tiffah.
Nimewaza Mara kadhaa kuhusu bidhaa zinazoletwa sokoni na Bwana Chibu Dangote kwa nini hazidumu katika soko?
Chibu ni kijana mpambanaji mwenye uchu wa mafanikio makubwa na amethubutu kuwekeza ndani na nje ya Muziki wake, ametoa ajira kwa vijana kadhaa. Lakini swali moja ninalijiuliza ni kwa nini bidhaa zake zinakufa na kupotea katika soko baada ya muda mfupi?
Tumeshuhudia akizindua Diamond Karanga, wasafi.com, Chibu perfume na zote hizi hazipo sokoni au hazalishi tena bidhaa hizo (biashara imebuma).
Na miaka kadhaa nyuma amefungua Kituo cha Runinga na Redio ambavyo vilipokelewa kwa hamasa kubwa na wafuasi wake, lakini kwa upande mwingine wamekuwa wakilalamikiwa kurusha maudhui yasiofaa na mara kadhaa wamekutana na rungu la TCRA. Je, Wasafi Media itapotea kama biashara zake zilizopita?
Wasafi bet ni biashara ingine aliyoitambulisha hivi karibuni je, itahimili ushindani dhidi ya kampuni zingine za kubashiri?
Mwisho, Mimi sio mtalamu wa biashara na nngependa kujua nini inachangia kufeli kwa bidhaa zake nyingi, nini ushauri wako kwa Baba
Tiffah.