Kwanini biashara ya sukari na mafuta ya kula huwa na zogo na vurumai nyingi sana nchini?

Kwanini biashara ya sukari na mafuta ya kula huwa na zogo na vurumai nyingi sana nchini?

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Ni nadra sana kusikia mwaka umeisha bila kelele, vurumai na sarakasi za kila aina kwenye biashara ya hizi bidhaa mbili za sukari na mafuta ya kula. Nini hasa kinasababisha haya yote ukizingatia ni bidhaa rahisi sana kuzalishwa, nchi nyingi tu wanazalisha na hata sisi wenyewe tukiamua na kuweka nia tunaweza kuzalisha hadi na ziada ya kuuza kwa majirani?

Nini hasa kinazifanya bidhaa hizi mbili kuwa keki au special hivyo kiasi kwamba lazima zilete zogo kila wakati?

Nini kinazifanya lazima zipande bei kila mwaka kwa kiasi kikubwa?

Nini kinapelekea wafanyabiashara kudaiwa kuzificha wakati mwingine hadi kupelekea wakuu wa wilaya na TRA wakisaidiwa na polisi kuzisaka kwa bunduki na watu kuwekwa ndani kwa sababu yake?
 
Ni nadra sana kusikia mwaka umeisha bila kelele, vurumai na sarakasi za kila aina kwenye biashara ya hizi bidhaa mbili za sukari na mafuta ya kula. Nini hasa kinasababisha haya yote ukizingatia ni bidhaa rahisi sana kuzalishwa, nchi nyingi tu wanazalisha na hata sisi wenyewe tukiamua na kuweka nia tunaweza kuzalisha hadi na ziada ya kuuza kwa majirani?

Nini hasa kinazifanya bidhaa hizi mbili kuwa keki au special hivyo kiasi kwamba lazima zilete zogo kila wakati?

Nini kinazifanya lazima zipande bei kila mwaka kwa kiasi kikubwa?

Nini kinapelekea wafanyabiashara kudaiwa kuzificha wakati mwingine hadi kupelekea wakuu wa wilaya na TRA wakisaidiwa na polisi kuzisaka kwa bunduki na watu kuwekwa ndani kwa sababu yake?
Biashara ya sukari na mafuta zinalipa sana sababu hizo bidhaa ni Mtambuka.Matajiri wengi wametajirika kupitia hizo bidhaa.sukari pia ni malighafi za bidhaa zingine.
 
Sukari na mafuta vinatumiwa sana na either matajiri ama maskini, kwaio ni bidhaa mbili ambazo ni chaka la mafisadi kujipatia utajiri wa kutisha.
 
Sukari na mafuta vinatumiwa sana na either matajiri ama maskini, kwaio ni bidhaa mbili ambazo ni chaka la mafisadi kujipatia utajiri wa kutisha.
Kwa nini hao matajiri hawawekezi kwenye viwanda ili wafaidike zaidi?
Kama wangewekeza kwenye viwanda si wangeuza zaidi ndani na nje ya nchi?
 
Sukari na mafuta vinatumiwa sana na either matajiri ama maskini, kwaio ni bidhaa mbili ambazo ni chaka la mafisadi kujipatia utajiri wa kutisha.
Mbona biashara za sabuni, unga, mchele, mkaa na gesi hazina hizo vurumai?
 
Hizo bidhaa mbili zinahitajika/tumika sana kwenye jamii bila kujali uwezo wa mhitaji.
Ni bidhaa ambazo zinauzika kipndi chote cha mwaka, hazina msimu.

Kwa kuliona hilo, wapigaji huwa wanatengeneza 'demand' fake kwa kuminya 'supply' ili waweze kupandisha bei watakavyo kwa vile wanajua bidhaa zitanunuliwa tu.

Mchezo huo ili ufanikiwe ni lazima uhusishe viongozi wa kisiasa.
Na ndivyo unavyofanyika.
 
Hizo bidhaa mbili zinahitajika/tumika sana kwenye jamii bila kujali uwezo wa mhitaji.
Ni bidhaa ambazo zinauzika kipndi chose cha mwaka, hazina msimu.

Kwa kuliona hilo, wapigaji huwa wanatengeneza 'demand' fake kwa kuminya 'supply' ili waweze kupandisha bei watakavyo kwa vile wanajua bidhaa zitanunuliwa tu.

Mchezo huo ili ufanikiwe ni lazima uhusishe viongozi wa kisiasa.
Na ndivyo unavyofanyika.
Demand fake inatengenezwaje wakati viwanda vya sukari ndivyo vyenye vibali ya kuingiza sukari pia? Serikali kila mwezi ina makadirio ya sukari inayohitajika na kupitia hayo makadirio ndio inatoa vibali kwa viwanda vya sukari kuagiza sukari ya ziada, sasa demand fake inatengenezwaje hapo wakati inajulikana kabisa mwezi huu tutahitaji sukari tani kadhaa?! Labda kama makadirio ya serikali huwa yanakuwa ya mbali sana, ya kuchelewa au viwanda havina uwezo wa kufanya hiyo biashara ya kuagiza sukari kutoka nje hivyo kuleta ubabaishaji.
 
Mtu aliyefanikiwa kuwa tajiri unasemaje ana akili ndogo mkuu?
Utajiri ni generational.

If you are rich but watoto wako ni one step closer na uchawa ni kilaza uliyepata fluke ya kuwa tajiri.

Hawa wenyeviti na matajiri aina ya Musukuma kasheku ni one step closer ya kuwa machawa
 
Demand fake inatengenezwaje wakati viwanda vya sukari ndivyo vyenye vibali ya kuingiza sukari pia? Serikali kila mwezi ina makadirio ya sukari inayohitajika na kupitia hayo makadirio ndio inatoa vibali kwa viwanda vya sukari kuagiza sukari ya ziada, sasa demand fake inatengenezwaje hapo wakati inajulikana kabisa mwezi huu tutahitaji sukari tani kadhaa?! Labda kama makadirio ya serikali huwa yanakuwa ya mbali sana, ya kuchelewa au viwanda havina uwezo wa kufanya hiyo biashara ya kuagiza sukari kutoka nje hivyo kuleta ubabaishaji.
Mchezo huo ili ufanikiwe ni lazima uhusishe viongozi wa kisiasa.
Na ndivyo unavyofanyika.
 
Back
Top Bottom