Kwanini binadamu hawazi kufa kwake bali kwa wenzake tu?

Kwanini binadamu hawazi kufa kwake bali kwa wenzake tu?

kissa anyigulile

JF-Expert Member
Joined
Apr 21, 2017
Posts
1,550
Reaction score
1,742

Huwa najiuliza: kwa nini binadamu hawazii hata kidogo kufa kwake bali kwa wenzie tu: Mifano ifuatayo:-​


1. Mume ana miaka 70, mke ana miaka 67. Mume anauza shamba milioni 30. Mke anakodi majambazi wanamuua mume abaki na hizo milioni 30(wastani wa maisha ya mtu ni miaka 80) Mmeoana mkiwa 17 & 20 yrs.

2. nk.
Hivi tunapumbazwa na nini?
 
Mume alikuwa WA Kwanza kumtafutia mke majambazi wamuue ili auze shamba aoe mke mwingine. Majambazi wakasanua issue Kwa mama akapanda dau Mzee akatangulizwa.
 
Alichowaza mleta mada sicho alichoandika maana hakuna mahusiano yoyote ya mada na mfano wa kumuwazia mtu kifo. Ila tusimlaumu sana mleta mada. Huenda tatizo ni background ya alikofundishwa kuandika insha!
 
Ni kama katili mwendazake alidhani ataishi milele kwa kummiminia risasi Braza Lissu utadhani Lissu siyo binadamu ni mnyama. Halafu hadi akapanga msiba na mazishi yake yatakavyokuwa badala yake yeye katangulia.
 
Sometimes na nyie wanaume mnaboa.

Mushi alipitiwa na bomba la gesi kalipwa 70m/= , kanunua gari mpya mkewe anaenda church na bodaboda,

Majuzi hapo kaopoa mtoto nyie mnawaita teketeke kamwibia milioni nzima.

Haya mama mushi bado anavaa suti zile za miaka ya 80.

Hivi mama mushi ana moyo wa chuma?

Wababa fanyeni hata kwa siri siri kidogo,
 
Nilidhani mada inazungumzia sisi kama binadamu tunawaza zaidi kuwapoteza vipenzi vyetu na watu wetu wa karibu kuliko kuondoka sisi wenyewe. Kuja kusoma mada ni mazigazi.
 
mfano wako bado, hauna maelezo ya kutosha
Nadhani atakuwa anarejea like tukio la mkoa wa Rukwa ambapo mme alimkodia wauaji mkewe na mke akamuwahi akaowaongezea dau wauaji wakamuuwa mumewe. Akamzika kwa kificho akauza mashamba akakimbia ila jana kadakwa. Nimeipata habari asubuhi visa redio.
 
Hao wame grow old together lakin pesa zinawatenganisha
 
Alichowaza mleta mada sicho alichoandika maana hakuna mahusiano yoyote ya mada na mfano wa kumuwazia mtu kifo. Ila tusimlaumu sana mleta mada. Huenda tatizo ni background ya alikofundishwa kuandika insha!
Haya, nitakupa mfano mdogo uelewe.
Tuseme ulikuwa na kazi nzuri. Mshahara mnono.
Kwenu unaonewa wivu sana.
Ghafla unapoteza kazi. Unarudi kwenu. Mawazo mengi, msongo wa mawazo mkali sana.
Ni wazi majirani wamefurahi, lakini wanajifanya kukupa pole ya kinafiki.
Pembeni wananong'ona: "Aaa huyu hana mwaka mmoja tutakuwa tumempoteza. Si mnaona alivyokonda?"Jambo hilo unalitambua, unavumilia. Na ulikuwa unawafadhili sana! Hawakumbuki fadhila.
Kumbe unahangaikia sehemu nyingine nzuri zaidi. Baada ya miezi nane hivi, unafanikiwa, unaondoka pale kwenu kimyakimya.
Unarudi baada ya mwaka hivi, uko vizuri zaidi ya pale mwanzoni.
Ukiulizia walipo wabaya wako waliokuwa wanasubiri " hatma yako" wengi wameondoka(wamekufa) au hali zao sio nzuri.
Waliobaki wanakuonea aibu saaana hadi huruma.(True story)
 
Kweli kabisa

mfano wako bado, hauna maelezo ya kutosha

Sijaelewa uzi


Alichowaza mleta mada sicho alichoandika maana hakuna mahusiano yoyote ya mada na mfano wa kumuwazia mtu kifo. Ila tusimlaumu sana mleta mada. Huenda tatizo ni background ya alikofundishwa kuandika insha!

Nilidhani mada inazungumzia sisi kama binadamu tunawaza zaidi kuwapoteza vipenzi vyetu na watu wetu wa karibu kuliko kuondoka sisi wenyewe. Kuja kusoma mada ni mazigazi.


 
Nadhani atakuwa anarejea like tukio la mkoa wa Rukwa ambapo mme alimkodia wauaji mkewe na mke akamuwahi akaowaongezea dau wauaji wakamuuwa mumewe. Akamzika kwa kificho akauza mashamba akakimbia ila jana kadakwa. Nimeipata habari asubuhi visa redio.
Ugumu tu wamaisha na kupenda mali, kuuwa mtu kwa sasa ni kawaida tu.
Ukizubaa dakika mbili washa kuchinja.
 
Back
Top Bottom