Kwanini Christmas iwe 25 December?

Kwanini Christmas iwe 25 December?

Jamani tuwe tunatumia akili ya kawaida,tarehe,majina ya miezi,majina ya siku yote ni naming tu hayana maana yoyote hapo kabla.Ni watu ndio wamevipa maana ni kama wewe leo uokote kitu polini ambacho hukijui halafu ukaamua kukipa jina-hivyo haimanishi hilo jina ndio uhalisia wa hicho kitu.
 
Wakuu

Bikra Mariam alipata mimba mwezi June Kwa uwezo wa roho mtakatifu.

Sasa iweje Pasaka iwe 25 December? Means alizaliwa December au alizaliwa njiti..

Mbona kama hesabu haipo sawa.

Soma Luka 1:26-35
Sasa Pasaka na mimba ya Yesu wapi na wapi? Halafu una uhakika Yesu alitungwa mimba mwezi wa 6? Nenda kasome upya, ule sio mwezi wa sita like June, ni miezi 6 since malaika Gabriel alipomtokea Zakaria na mkewe Elizabeth kuhusu mimba ya nabii Yohana mbatizaji; in other words, Yesu na Yohana mbatizaji wanatofautiana miezi 6 kuzaliwa.
Now back to the topic (yote haya ni kwa mujibu wa mtazamo wangu baada ya kuisoma Biblia ). Nadhani hiyo pasaka, ulitaka kusema Christmas na sjo Pasaka; kwa ufupi hata mimi siamini kama Yesu alizaliwa tarehe 25 December. Hi siku ni ya kubuni, sio siku sahihi. Ninazo sababu kubwa 2, moja ambayo ni ya uhakika ni hi, sherehe zote za Kikristo zina mizizi agano la KALE, Pasaka, Pentecost, Ijumaa kuu nk zote zilianza kwenye agano la kale; yaani matukio yote ya Yesu na kanisa, misingi yake iliwekwa kabla Yesu hajazaliwa, kwasababu ya muda sitazifafanua hizo sherehe maanake zipo wazi sana kwa Biblia, Kristmas haipo, sio miongoni mwa hizo sherehe. Sababu yangu ya pili ni ya kutokuamini kwamba Yesu hakuzaliwa mwezi December ni ya Kijiografia na kihistoria. Biblia inasema, wakati Yesu anazaliwa, kulikua na baadhi ya wachungaji wako porini wakichunga wanyama wao (you may put kondoo hapa ) ilikua usiku or alfajiri; kwa mujibu wa majira ya kijografia na kihistoria, mwezi December ni kipindi cha baridi kali sana and hence wasn't possible kwa watu kua nje usiku or alfajiri; kipindi hicho wachungaji walikua wanawalisha mifugo yao akiba ya chakula ambacho walikiandaa miezi ya joto. Kwasababu hizo 2, Yesu hakuzaliwa December, possible ilikua kati ya September or August.
 
Tarehe ya huyo YESU ni changamoto Kwa sababu na kiuhalisia hajawai kuwepo, na hakuna ushahidi mahala popote hapa duniani inaonesha Kuna mtu wa aina yake aliishi hapo Yerusalem(Israel) ya mchongo hapo middle east miaka 2000 iliyopita.

Kilichofanyika na hao watunzi wa dini, ilikuwa kuhamisha hadithi na stories za Miungu ya zamani iliyoabudiwa na wamisri, wahindu, wabudha, n.k, stories ambazo zilihusu uzao wa nusu Mtu nusu Mungu, yaani stories za akina krisha,Zeus, Mithra,Horus, na habari hizo kuingizwa ktk bible huku akiundwa Character mpya ambaye wangemfanya kama unganiko la zama za kale(old testament) na zama mpya(new testament), huku zama hizo zikiwakilishwa na huyo character ambaye alibatizwa majina mazuri ambayo hayaondoi uhalisia wake kuwa ndie yule yule aliyeabudiwa na jamii za kale na Sasa kupewa majina mapya ambayo yangeficha uhalisia wake.

Yesu ni aina ya Mzimu/Pepo, ambalo lipo enzi na enzi limeabudiwa na jamii nyingi kwa majina tofauti na staarabu tofauti, ndiomaana uhalisia wake wa kuzaliwa ni ule ule, hauwezi kubadilishwa.

Narudia Tena, yesu wa biblia ama huyo Issa bin Mariam wa Quran hajawai kuwepo, chunguza mwenyewe hata ktk nakala za kihistoria hutoona hadithi za uwepo wa historia ya yesu zaidi ya kuona maandiko ya kidini

Iyo Israel yenyewe haijawai kuwepo kabla ya kuundwa hapo juzi na umoja wa mataifa, je huyo Jesus aliishi wapi?, miaka 2000 iliyopita hapo Israel hapakuwai kuwa na stories za yesu wala jamii inayomjua yesu, wala wao wenyewe waisrael hawakuwai kuwepo, zaidi ya utawala wa wazungu matapeli wanaojiita waisrael ilihali ni wazungu na baadhi ya waarabu ambao Leo hii nao wanaojiita wapalestina ama wengine wanajiita wazawa wa ibrahimu ambaye nae hajawai kuwepo, na hawana uhusika nae.

Achaneni na dini mnapotezewa muda wenu.
 
Wakuu,

Bikra Mariam alipata mimba mwezi June Kwa uwezo wa roho mtakatifu.

Sasa iweje Pasaka iwe 25 December? Means alizaliwa December au alizaliwa njiti..

Mbona kama hesabu haipo sawa.

Soma Luka 1:26-35
Hio ni kumbukumbu sio kwamba ndo siku halisi.....orthodox wengi Christmas ni mwezi wa kwanza
 
Jamani tuwe tunatumia akili ya kawaida,tarehe,majina ya miezi,majina ya siku yote ni naming tu hayana maana yoyote hapo kabla.Ni watu ndio wamevipa maana ni kama wewe leo uokote kitu polini ambacho hukijui halafu ukaamua kukipa jina-hivyo haimanishi hilo jina ndio uhalisia wa hicho kitu.
Hakuna jambo kama Hilo, Kila kitu kina maana, hata hivyo vitu vya kuokotwa vinapewa majina kulingana na uhalisia wake, ndiomaana Kuna scientific names kwa mimea, chemicals, wanyama n.k, Kila kitu kina uhalisia wake.

Ni ktk dini tu mambo ya uhalisia na ukweli yanapigwa vita, yaani wafuasi wa dini mnafunzwa kuamini badala ya kutafakali na kuhoji ukweli wa mambo, hili ndiko limewafanya watu wengi ktk hiyo mikusanyiko kulishwa uongo wa Kila aina na wanaogopa kuhoji

Hizo TAKATAKA ziitwazo dini, kama zingefundishwa bila vitisho na kuruhusu mahojiano, nina uhakika hakuna ambaye angebaki ktk hizo kanisa na misikiti.
 
Kwanini hujafikiria labda alizaliwa mwezi wa12 mwaka uliofuata...?
 
Sasa Pasaka na mimba ya Yesu wapi na wapi? Halafu una uhakika Yesu alitungwa mimba mwezi wa 6? Nenda kasome upya, ule sio mwezi wa sita like June, ni miezi 6 since malaika Gabriel alipomtokea Zakaria na mkewe Elizabeth kuhusu mimba ya nabii Yohana mbatizaji; in other words, Yesu na Yohana mbatizaji wanatofautiana miezi 6 kuzaliwa.
Now back to the topic (yote haya ni kwa mujibu wa mtazamo wangu baada ya kuisoma Biblia ). Nadhani hiyo pasaka, ulitaka kusema Christmas na sjo Pasaka; kwa ufupi hata mimi siamini kama Yesu alizaliwa tarehe 25 December. Hi siku ni ya kubuni, sio siku sahihi. Ninazo sababu kubwa 2, moja ambayo ni ya uhakika ni hi, sherehe zote za Kikristo zina mizizi agano la KALE, Pasaka, Pentecost, Ijumaa kuu nk zote zilianza kwenye agano la kale; yaani matukio yote ya Yesu na kanisa, misingi yake iliwekwa kabla Yesu hajazaliwa, kwasababu ya muda sitazifafanua hizo sherehe maanake zipo wazi sana kwa Biblia, Kristmas haipo, sio miongoni mwa hizo sherehe. Sababu yangu ya pili ni ya kutokuamini kwamba Yesu hakuzaliwa mwezi December ni ya Kijiografia na kihistoria. Biblia inasema, wakati Yesu anazaliwa, kulikua na baadhi ya wachungaji wako porini wakichunga wanyama wao (you may put kondoo hapa ) ilikua usiku or alfajiri; kwa mujibu wa majira ya kijografia na kihistoria, mwezi December ni kipindi cha baridi kali sana and hence wasn't possible kwa watu kua nje usiku or alfajiri; kipindi hicho wachungaji walikua wanawalisha mifugo yao akiba ya chakula ambacho walikiandaa miezi ya joto. Kwasababu hizo 2, Yesu hakuzaliwa December, possible ilikua kati ya September or August.
Hii tar.25Dec.,kiuhalisia ni siku ya kuzaliwa kwa Prince Tammuz.
Hii siku ilikuwa ikiadhimishwa kila mwaka kipindi cha Rumi ya kipagani hadi walipo kubaliani na wakristo wa kale kuiingiza sikukuu hiyo kwenye dini,iwe sikukuu ya kidini [ili kulinda na kutunza desturi zao],ikiambatana na kuabudu siku ya kwanza ya juma [jumapili]ambayo kwao [warumi]ni siku ya mungu jua.
Hizi ni baadhi ya desturi nyingi za kipagani zilizoingizwa kwenye dini/ibada kwa makubaliano maalum ya kukomesha mateso na mauaji kwa wakristo wa wakati huo.
 
Back
Top Bottom