Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,468
- 911,184
Kwanini DOLA yetu inawaabudu sana wawekezaji kutoka nje?
Katika kampeni za JK za Uraisi za mwaka 2010 alisisitiza ya kuwa bila ya misaada nchi haiendesheki! Kwa lugha nyingine ni kuwa nchi hii siyo ya kujitegemea kama katiba inavyotamba bali ni nchi inayoendeshwa kwa huruma za wageni.
Wanasiasa wote hudai kuamini ya kuwa nchi hii itajengwa na watanzania wenyewe. Lakini inapokuja utekelezaji imani hii huwekwa kando na wageni kutukuzwa kama miungu wadogo hususani kwenye maeneo yafuatayo:-
1) Hupewa misaada na dola ya misamaha ya kodi ambayo ni ya kibaguzi na hivyo katiba ya nchi hukiukwa. Misamaha hiyo hufifilisha dhana nzima ya ushindani na hivyo kuondoa makali ya nguvu za soko na kukatisha tamaa wawekezaji wa ndani kwenye fani husika ambao hawakupewa misamaha tajwa.
Dola inayojiheshimu na ambayo ingependa iheshimiwe kwenye sheria zao hukataza misamaha ya kodi ya aina zozote na kuhakikisha misamaha kama ipo inufaishe walengwa wote waliowekeza kwenye sekta husika.
2) Sera ya mwenyeji mpishe mgeni huchachamaa sana kwa hoja zisizo na mashiko ya kuwa mwekezaji mgeni atazalisha ajira, kuleta kasi ya maendeleo wakati ukweli ni kuwa kazi ya kuamua hilo lilikuwa lifanywe na mwenyeji ambaye serikali badala ya kumwezesha kwa sheria inamdumaza na kumfilisi kwa sheria hizo hizo kwa fidia kiduchu na kusukumwa maeneo ambayo hayana rutuba au mbali na mvuto wa kisoko.
3) Dola kwa kutupiwa peremende ambazo hufichwa kwenye akaunti za ughaibuni za baadhi ya wanasiasa na watendaji waandamizi serikalini basi huwa ni kichocheo cha kumdhulumu raia na kuhakikisha mwekezaji mgeni ndiye mwenye haki na raia mwenyeji kuonekana ni msumbufu na anachelewesha maendeleo.
4) Jitihada zinafanyika hata kuwawezesha wazawa ambao waliukana uraia na kujiandikisha uraia wa nchi nyingine kwa kuwavika vilemba vya ukoka kama Balozi maalumu ili kuwasaidia waandamizi tajwa katika kujenga mazingira ya kuwafilisi wenyeji raia hata kila kidogo walichonacho.
5) Mwekezaji mwenyeji anaonekana ni mnyonge sana na hivyo hastahili kuwezeshwa zaidi ya kuandaliwa awe manamba wa kulipwa kiduchu na mwekezaji mgeni.
6) Pamoja na mwekezaji mwenyeji kuonekana si mali kitu inapokuja dhana nzima ya kujitawala wenyewe waandamizi tajwa huwa wakali wanaposhurutishwa kukabidhi dola kwa hao wageni kwa sababu kwa kufanya hivyo watakuwa wamesalimisha mkate wao.
Swali langu huwa hivi yawezekana kweli tuwe huru kisiasa bila ya kuwa huru kiuchumi? Kama uhuru wa kiuchumi tunawamilikisha wawekezaji wageni ni kwa sababu ipi inatuzuia tusiwamilikishe na dola pia? Kama hatuwezi kwenye nyanja ya kiuchumi yawaje tuweze nyanja ya kisiasa?
7) Nguvu ya kiuchumi ya vyama vya siasa na wagombea kwenye nafasi za juu za taifa hivi sasa kimyakimya zinategemea sana ruzuku kutoka kwa makampuni makubwa kutoka nje. Kwa vile tumefikia hatua kuwa gharama za kampeni za kupata uhalali wa kusimamia dola zinatoka kwa wawekezaji hao wakubwa hivi uhuru wetu hata huo wa kisiasa sasa uko wapi?
8) Jitihada za kumwezesha mwekezaji wa ndani zinadhoofishwa na viwango vikubwa vya kodi, urasimu wa kuanzisha na kuendeleza biashara ikiwa na pamoja na mtazamo wa serikali kuwa mwekezaji wa ndani siyo mwekezaji bali mbabaishaji tu.
Katika kampeni za JK za Uraisi za mwaka 2010 alisisitiza ya kuwa bila ya misaada nchi haiendesheki! Kwa lugha nyingine ni kuwa nchi hii siyo ya kujitegemea kama katiba inavyotamba bali ni nchi inayoendeshwa kwa huruma za wageni.
Wanasiasa wote hudai kuamini ya kuwa nchi hii itajengwa na watanzania wenyewe. Lakini inapokuja utekelezaji imani hii huwekwa kando na wageni kutukuzwa kama miungu wadogo hususani kwenye maeneo yafuatayo:-
1) Hupewa misaada na dola ya misamaha ya kodi ambayo ni ya kibaguzi na hivyo katiba ya nchi hukiukwa. Misamaha hiyo hufifilisha dhana nzima ya ushindani na hivyo kuondoa makali ya nguvu za soko na kukatisha tamaa wawekezaji wa ndani kwenye fani husika ambao hawakupewa misamaha tajwa.
Dola inayojiheshimu na ambayo ingependa iheshimiwe kwenye sheria zao hukataza misamaha ya kodi ya aina zozote na kuhakikisha misamaha kama ipo inufaishe walengwa wote waliowekeza kwenye sekta husika.
2) Sera ya mwenyeji mpishe mgeni huchachamaa sana kwa hoja zisizo na mashiko ya kuwa mwekezaji mgeni atazalisha ajira, kuleta kasi ya maendeleo wakati ukweli ni kuwa kazi ya kuamua hilo lilikuwa lifanywe na mwenyeji ambaye serikali badala ya kumwezesha kwa sheria inamdumaza na kumfilisi kwa sheria hizo hizo kwa fidia kiduchu na kusukumwa maeneo ambayo hayana rutuba au mbali na mvuto wa kisoko.
3) Dola kwa kutupiwa peremende ambazo hufichwa kwenye akaunti za ughaibuni za baadhi ya wanasiasa na watendaji waandamizi serikalini basi huwa ni kichocheo cha kumdhulumu raia na kuhakikisha mwekezaji mgeni ndiye mwenye haki na raia mwenyeji kuonekana ni msumbufu na anachelewesha maendeleo.
4) Jitihada zinafanyika hata kuwawezesha wazawa ambao waliukana uraia na kujiandikisha uraia wa nchi nyingine kwa kuwavika vilemba vya ukoka kama Balozi maalumu ili kuwasaidia waandamizi tajwa katika kujenga mazingira ya kuwafilisi wenyeji raia hata kila kidogo walichonacho.
5) Mwekezaji mwenyeji anaonekana ni mnyonge sana na hivyo hastahili kuwezeshwa zaidi ya kuandaliwa awe manamba wa kulipwa kiduchu na mwekezaji mgeni.
6) Pamoja na mwekezaji mwenyeji kuonekana si mali kitu inapokuja dhana nzima ya kujitawala wenyewe waandamizi tajwa huwa wakali wanaposhurutishwa kukabidhi dola kwa hao wageni kwa sababu kwa kufanya hivyo watakuwa wamesalimisha mkate wao.
Swali langu huwa hivi yawezekana kweli tuwe huru kisiasa bila ya kuwa huru kiuchumi? Kama uhuru wa kiuchumi tunawamilikisha wawekezaji wageni ni kwa sababu ipi inatuzuia tusiwamilikishe na dola pia? Kama hatuwezi kwenye nyanja ya kiuchumi yawaje tuweze nyanja ya kisiasa?
7) Nguvu ya kiuchumi ya vyama vya siasa na wagombea kwenye nafasi za juu za taifa hivi sasa kimyakimya zinategemea sana ruzuku kutoka kwa makampuni makubwa kutoka nje. Kwa vile tumefikia hatua kuwa gharama za kampeni za kupata uhalali wa kusimamia dola zinatoka kwa wawekezaji hao wakubwa hivi uhuru wetu hata huo wa kisiasa sasa uko wapi?
8) Jitihada za kumwezesha mwekezaji wa ndani zinadhoofishwa na viwango vikubwa vya kodi, urasimu wa kuanzisha na kuendeleza biashara ikiwa na pamoja na mtazamo wa serikali kuwa mwekezaji wa ndani siyo mwekezaji bali mbabaishaji tu.