Kwanini elimu inaonekana haina thamani kama zamani?

sirluta

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2012
Posts
6,325
Reaction score
2,491
Elimu ya sasa inaonekana haina thamani ukilinganisha na zamani kwa jinsi zamani msomi alikuwa akiheshimiwa.

"shule ya msingi niliyosoma nakumbuka tulimaliza kama 80 lakini tuliofaulu kwenda kidato cha kwanza tulikuwa wanne. Nakumbuka kipindi hicho watu walikuwa wakitoka kanisani ile ibada ya kwanza wanapitia pale nyumbani kunipa hongera.

Kuna mtu mmoja wa same nae alinihadithia wakati huo anamaliza darasa la saba, kijiji kizima alifaulu mwenyewe kwenda kidato cha kwanza, akasema alikuwa akifungiwa ndani ili asilogwe hadi aliposafiri kwenda shuleni.

Kuna injinia mmoja nae alinisimulia wakati anasoma ILBORU sec, alikuwa anasindikizwa na kijiji kizima kutoka ngarenanyuki hadi usa river halafu wanarudi maana wakati huo magari hayakuwepo pia kwa usalama zaidi(ngarenanyuki to usa river ni zaidi ya km 50). Hiyo ndo tofauti ya elimu ya enzi hizo na sasa.

Kama na wewe una historia yako tupe tafadhali tuone tulikopitia!
 
Waulize ccm maana ndio wanaounda serikali mwaka wa 50 huu ndugu usitafute mchawi .
 
Utandawazi ndugu! Hata vitu vilivyoonekana vya thaman enzi hizo havina thaman tena. Mf. Nyumba nzur wakat huo, magar, nakumbuka miaka ya tisini tukiwa na cmu ya mezan kwetu (ya waya) nlkua naringa sana naona n kitu cha pekee! Same applies to education Qualifications itafikia hatua kila nyumba kutakua na Profesa. Ka unabisha nenda UDSM uone wanachuo wanavyobanana darasan (kumbi kubwa tuu) had wengne kusimama madirishan! Na huku zaman degree walisoma wachache tuu kwa raha zao.
 
Elimu hailipi siku hizi,,hasa kubwa kubwa.
 

mkuu heshima hii leo itatoka wapi wakati wanaofaulu darasa la saba kwenda kidato cha kwanza hawajui kusoma wala kuandika hata majina yao? Je! Upo uwezekano wa kijiji kumsndikiza huyu mwanafunzi kutoka Ngarenanyiki mpaka Ilboru ilihali wanajua hawezi hata kuandika jina lake lakini amefauru? Zamani hakukua na BRN badala yake serikali iliwajali walimu nao wakaipenda kazi yao na wakafundisha kwa moyo mweupe watoto wakafaulu sio serikali hii ya magamba inayotishia walimu badala ya kuwalipa stahiki zao ili waifurahie kazi yao.
 

kuna mambo ya kusalitiana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…