Kwanini hatuwaoni matajiri wazawa wakisaidia timu za mpira ,tatizo nini ?

Kwanini hatuwaoni matajiri wazawa wakisaidia timu za mpira ,tatizo nini ?

py thon

JF-Expert Member
Joined
Sep 11, 2016
Posts
2,476
Reaction score
4,448
Klabu ya Ndanda imesaini mkataba wa mwaka mmoja wa udhamini na kampuni ya Motisun.

65880c7e01b22598c775cdb664963de4.jpg



65f7bb27658b809b5df8d6066d2cf35f.jpg

Tangia nifuatilia mpira na ligi ya Vpl naona makampuni ya watu wenye asili ya nje kusaidia vilabu vyetu kwenye udhamini nk ,kuanzia simba ,yanga ,mbeya city ,coastal union ,ndanda nk


Utawakuta akina Bin slum,kassim dewji ,Mo ,quality group ,migodi nk

Kwanini matajiri wenye asili au makampuni ya wenye asili kama IPP ,matajiri wengine hatuwaoni wakisaidia vilabu vyetu

Mfano Arusha kuna matajiri kibao lakini cha kushangaza hakuna timu inayoshiriki ligi kuu kwa muda mrefu ,Moshi pia ,Dodoma nk.


Tatizo nini wabahili sana au hatuna moyo mweupe
 
Tatizo hela zao ni zakutengenezea juice tuuu
 
Nakumbuka mzee Mengi alikuwa ana nia ya kuidhamini timu ya Yanga.
Lakini kuna siku pale uwanja wa taifa wa ndani, wanamochezea basketball, kulikuwa na mkutano wa wanachama wa Yanga. Sikumbuki walitofautiana kitu gani, kikasababisha wamsulubu huyo mzee na nusura wampige na mawe, toka siku hiyo akajiondoa kuifadhiri Yanga fc.
Tatizo matajiri wazawa asilia, wanashindwa kuhimili mikikimikiki ya timu za tanzania.
Mikikimikiki hiyo inaambatana na kudhihakiwa, kulaumiwa, kutukanwa na hata kupigwa kama hujajilinda vizuri.
Jambo hili linasababishwa usumbufu mkubwa kuweza kustahili kuvunjiwa heshima mbele ya familia na ndugu na jamaa zao.
Angalia mfano usumbufu unaofanywa na akina mzee Kilomoni na Akilimali.
Ustaarabu unakuwa mdogo mtu anatoa pesa yake kwa moyo wa kusaidia timu anaishia kudhalilishwa.
Matajiri wa kibongo hawapendi huu usumbufu.
 
Nakumbuka mzee Mengi alikuwa ana nia ya kuidhamini timu ya Yanga.
Lakini kuna siku pale uwanja wa taifa wa ndani, wanamochezea basketball, kulikuwa na mkutano wa wanachama wa Yanga. Sikumbuki walitofautiana kitu gani, kikasababisha wamsulubu huyo mzee na nusura wampige na mawe, toka siku hiyo akajiondoa kuifadhiri Yanga fc.
Tatizo matajiri wazawa asilia, wanashindwa kuhimili mikikimikiki ya timu za tanzania.
Mikikimikiki hiyo inaambatana na kudhihakiwa, kulaumiwa, kutukanwa na hata kupigwa kama hujajilinda vizuri.
Jambo hili linasababishwa usumbufu mkubwa kuweza kustahili kuvunjiwa heshima mbele ya familia na ndugu na jamaa zao.
Angalia mfano usumbufu unaofanywa na akina mzee Kilomoni na Akilimali.
Ustaarabu unakuwa mdogo mtu anatoa pesa yake kwa moyo wa kusaidia timu anaishia kudhalilishwa.
Matajiri wa kibongo hawapendi huu usumbufu.
Wakina. KILOMONI na AKILIMALI wale wazee ni wachawi sana, usiombe
 
Wakina. KILOMONI na AKILIMALI wale wazee ni wachawi sana, usiombe

Sababu kubwa ni kuwa kiwango cha utajiri wao hakiwezi kukidhi mahitaji ya ushindani wa sasa. Ukweli ni kuwa kabla ya hawa wakubwa kipesa akina Dewji na Manji wenye utajiri mkubwa sana, walikuwepo wengine wenye utajiri lakini wa chini yao, wote wa asia na weusi akina Azim Dewji, Hanspope (mzungu na mweusi), Friends of Simba ( weusi, mchanganyiko etc.), Yusuph Hazali etc. kwa Simba, akina David Mosha, Clement Sanga etc., kwa upande wa Yanga. Hivyo ni kuzidiana tu. Kwa kuwa wa Asia ndiyo wanaoongoza kwa sasa kipesa, kuna uwezekano mkubwa zaidi wa kuwepo wenye nia na weledi wa ku-sponsor.
 
Back
Top Bottom