Kwanini isichukuliwe ile Rasimu ya Katiba Mpya ya Jaji Warioba?

Kwanini isichukuliwe ile Rasimu ya Katiba Mpya ya Jaji Warioba?

Mwamba 3

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2018
Posts
253
Reaction score
285
Tunashukuru Rais wetu Mtukufu ameridhia hitaji la katiba mpya .

Na itapendezwa zaidi Rais atakapong'olewa baadhi ya meno kuepusha utawala wa kibabe
Binafsi baadhi ya mambo ambayo natamani yawepo kwenye Katiba ni Rais kuchunguzwa na kushtakiwa baada ya Urais wake endapo kulikuwa na ubadhilifu wa mali za umma , Kupinga matokeo ya uchaguzi mahakamani endapo kama kulikuwa na dosari zozote za usimamizi , Kuhusu Tume huru ningependekeza ingekuwa inaundwa na Bunge ili iwajibike chini ya bunge ( bahati mbaya bunge lenyewe halina upinzani ), Serikali kutoingilia mihimili mingine hasa mahakama .n.k

Lakini nirudi kwenye mada tajwa hapo juu. Najua mchakato wa kuandaa katiba mpya una mambo mengi na gharama nyingi na huenda figisufigisu nyingi . Ili kuepusha hayo kwa nini isingechukuliwa Rasimu ya katiba ya Jaji Warioba kutokana na sababu zifuatazo

Kwanza ; Rasimu ya katiba ya Jaji Warioba ilipatikana kipindi ambacho walau kulikuwa na vugu vugu la upinzani hivyo ilibeba mambo mazuri tofauti na hali iliyopo sasa

Pili ; Kwa asilimia kubwa ya Watanzania walipendezewa na ile Rasimu , hivyo hakuna haja mambo ya kuunda tume jingine ni kupoteza hela tu . Maana mambo mazuri yalikuwemo mule .

Tatu ; Inasemekana mchakato wa kudai katiba mpya haujaanza leo wala jana . Ulikuwepo na tume zikaundwa likini wenye nchi hawakosi kuleta vikwazo mambo yanaishia tu kwenye kupata rasimu basi. Mambo ili yasiwe hivyo na kama tuna dhamira ya dhati ya kuipatia Tanzania katiba mpya basi tuitumie ile Rasimu ya Warioba

Nne; Watanzania tulikuwa na imani sana na rasimu ya Jaji walioba kwa sababu Ilibeba matakwa ya kweli ya Watanzania. Huyu Mkandala ni tofauti na Warioba maana Mkandala hana kabisa msukumo wa ndani wa kuwapatia Watanzania katiba ya kweli

Je, ni nini tunakitafuta , kwa nini tusiitumie ile Rasimu ya katiba ya Jaji Warioba , ina dosari gani ?

Karibuni ili tufumbuane macho maana wengine huenda hatuna jicho la tatu
 
Binafsi siiafiki katiba pendekezwa ya Jaji Warioba. Ila ningependekeza kuongezwa Muhimili miwili ya serikali
1) serikali
2) bunge
3) mahakama
4) maridhio na habari
5) Machifu

Kuna matatizo ya wananchi ambayo yameshindwa kutatuliwa na mihimili iliyopo hivyo iongezwe mihimili

1) kutanua mgawanyo wa keki ya taifa
2) kuongeza wigo wa kutatua changamoto za wananchi
3) kujenga tumaini jipya la maisha mapya kwa wananchi
4) mihimili iliyopo imezidiwa
5) kuongeza uwajibika wa serikali kwa wananchi
 
Binafsi siiafiki katiba pendekezwa ya Jaji Warioba. Ila ningependekeza kuongezwa Muhimili miwili ya serikali
1) serikali
2) bunge
3) mahakama
😁
4) maridhio na habari
Serikali hiyo hiyo au watu wa serikali watakuwa wamiliki wa hizo media na haitafanya chochote cha maana.
5) Machifu
Hawa watu mara nyingi huongoza leave kutumia Mila, desturi, na ubabe maana madaraka ni ya kurithishana.

Sana Sana watazidisha chuki na mgawanyiko wa kikabila tu.
Kuna matatizo ya wananchi ambayo yameshindwa kutatuliwa na mihimili iliyopo hivyo iongezwe mihimili

1) kutanua mgawanyo wa keki ya taifa
2) kuongeza wigo wa kutatua changamoto za wananchi
3) kujenga tumaini jipya la maisha mapya kwa wananchi

4) mihimili iliyopo imezidiwa
5) kuongeza uwajibika wa serikali kwa wananchi
 
Kuchukua Rasimu ya Warioba ni kujinyima ulaji, wale waliopitisha rasimu ile ni wale na walishakula pesa zao, sasa ni ZAMU yetu, pesa zetu! TOZO = Rasimu + Sensa ya watu + Sensa ya Makazi + Miradi mipya hewa
 
Tunashukuru Rais wetu Mtukufu ameridhia hitaji la katiba mpya .

Na itapendezwa zaidi Rais atakapong'olewa baadhi ya meno kuepusha utawala wa kibabe
Binafsi baadhi ya mambo ambayo natamani yawepo kwenye Katiba ni Rais kuchunguzwa na kushtakiwa baada ya Urais wake endapo kulikuwa na ubadhilifu wa mali za umma , Kupinga matokeo ya uchaguzi mahakamani endapo kama kulikuwa na dosari zozote za usimamizi , Kuhusu Tume huru ningependekeza ingekuwa inaundwa na Bunge ili iwajibike chini ya bunge ( bahati mbaya bunge lenyewe halina upinzani ), Serikali kutoingilia mihimili mingine hasa mahakama .n.k

Lakini nirudi kwenye mada tajwa hapo juu. Najua mchakato wa kuandaa katiba mpya una mambo mengi na gharama nyingi na huenda figisufigisu nyingi . Ili kuepusha hayo kwa nini isingechukuliwa Rasimu ya katiba ya Jaji Warioba kutokana na sababu zifuatazo

Kwanza ; Rasimu ya katiba ya Jaji Warioba ilipatikana kipindi ambacho walau kulikuwa na vugu vugu la upinzani hivyo ilibeba mambo mazuri tofauti na hali iliyopo sasa

Pili ; Kwa asilimia kubwa ya Watanzania walipendezewa na ile Rasimu , hivyo hakuna haja mambo ya kuunda tume jingine ni kupoteza hela tu . Maana mambo mazuri yalikuwemo mule .

Tatu ; Inasemekana mchakato wa kudai katiba mpya haujaanza leo wala jana . Ulikuwepo na tume zikaundwa likini wenye nchi hawakosi kuleta vikwazo mambo yanaishia tu kwenye kupata rasimu basi. Mambo ili yasiwe hivyo na kama tuna dhamira ya dhati ya kuipatia Tanzania katiba mpya basi tuitumie ile Rasimu ya Warioba

Nne; Watanzania tulikuwa na imani sana na rasimu ya Jaji walioba kwa sababu Ilibeba matakwa ya kweli ya Watanzania. Huyu Mkandala ni tofauti na Warioba maana Mkandala hana kabisa msukumo wa ndani wa kuwapatia Watanzania katiba ya kweli

Je, ni nini tunakitafuta , kwa nini tusiitumie ile Rasimu ya katiba ya Jaji Warioba , ina dosari gani ?

Karibuni ili tufumbuane macho maana wengine huenda hatuna jicho la tatu

Umeongea point sana
 
Tunashukuru Rais wetu Mtukufu ameridhia hitaji la katiba mpya .

Na itapendezwa zaidi Rais atakapong'olewa baadhi ya meno kuepusha utawala wa kibabe
Binafsi baadhi ya mambo ambayo natamani yawepo kwenye Katiba ni Rais kuchunguzwa na kushtakiwa baada ya Urais wake endapo kulikuwa na ubadhilifu wa mali za umma , Kupinga matokeo ya uchaguzi mahakamani endapo kama kulikuwa na dosari zozote za usimamizi , Kuhusu Tume huru ningependekeza ingekuwa inaundwa na Bunge ili iwajibike chini ya bunge ( bahati mbaya bunge lenyewe halina upinzani ), Serikali kutoingilia mihimili mingine hasa mahakama .n.k

Lakini nirudi kwenye mada tajwa hapo juu. Najua mchakato wa kuandaa katiba mpya una mambo mengi na gharama nyingi na huenda figisufigisu nyingi . Ili kuepusha hayo kwa nini isingechukuliwa Rasimu ya katiba ya Jaji Warioba kutokana na sababu zifuatazo

Kwanza ; Rasimu ya katiba ya Jaji Warioba ilipatikana kipindi ambacho walau kulikuwa na vugu vugu la upinzani hivyo ilibeba mambo mazuri tofauti na hali iliyopo sasa

Pili ; Kwa asilimia kubwa ya Watanzania walipendezewa na ile Rasimu , hivyo hakuna haja mambo ya kuunda tume jingine ni kupoteza hela tu . Maana mambo mazuri yalikuwemo mule .

Tatu ; Inasemekana mchakato wa kudai katiba mpya haujaanza leo wala jana . Ulikuwepo na tume zikaundwa likini wenye nchi hawakosi kuleta vikwazo mambo yanaishia tu kwenye kupata rasimu basi. Mambo ili yasiwe hivyo na kama tuna dhamira ya dhati ya kuipatia Tanzania katiba mpya basi tuitumie ile Rasimu ya Warioba

Nne; Watanzania tulikuwa na imani sana na rasimu ya Jaji walioba kwa sababu Ilibeba matakwa ya kweli ya Watanzania. Huyu Mkandala ni tofauti na Warioba maana Mkandala hana kabisa msukumo wa ndani wa kuwapatia Watanzania katiba ya kweli

Je, ni nini tunakitafuta , kwa nini tusiitumie ile Rasimu ya katiba ya Jaji Warioba , ina dosari gani ?

Karibuni ili tufumbuane macho maana wengine huenda hatuna jicho la tatu
Wanataka ya Ccm. Ya warioba wanahisi ni ya wapinzani😅😅😅
 
Kuchukua Rasimu ya Warioba ni kujinyima ulaji, wale waliopitisha rasimu ile ni wale na walishakula pesa zao, sasa ni ZAMU yetu, pesa zetu! TOZO = Rasimu + Sensa ya watu + Sensa ya Makazi + Miradi mipya hewa
😅😅😅
 
Hakuna chama tawala Duniani kinachowasaidia wapinzani wake Ili wakitoa madarakani.
.

Wapinzani wamelala.
Wanasubiri huruma ya Makada Walaamba asali.

Kuna Kauli aliitoa Mh.Spika Wa Bunge la Venezuela kuwa MTU akimsema vibaya basi Vijana Wa chama chake wanyooke Naye fasta. Yaani wamuue harakaharaka.
Cha ajabu waliolengwa Wanabaki kutwiti mitandaoni.

Wapinzani uchwara walionao Kule Venezuela hawakujua la KUFANYA Kwa tukio lile ambalo lilikua liko wazi kabisa. Ule ulikua ni upumbavu Wa Hali ya juu.
Kwa kweli sikuchangia chochote mtandaoni nikakaa kimya mana Sina mapenzi na vyama vyote zaidi ya Nchi yangu.
Ilikua ni kiasi cha Idara zote za vyama vya kisiasa makini kuja na tamko la kuhamasisha maandamano yasiyo na kikomo Nchi nzima na kumng,oa kwenye nafasi ya uspika na ingeanza kuleta mabadiliko chanya. Matamko ya kunyooka na wapinzani yanaanzaga kidogo Kidogo mwishowe wanaanza kupotezwa halafu Baadae wanaanza kulalamika Wakati walitakiwa wachukue action mapema sana. Ni wazi Hata yule Rais Wa Venezuela asingekubali nchi ichafuke Kwa matamko ya kichochezi ya spika. Angeshauriwa wewe omba radhi au ujiuzulu.

Wapinzani amkeni kumekucha. Wenzenu wameshaanza kampeni muda mrefu 2025 mtashangaa watakavyonyooka na nyie .


Bila Chadema imara Nchi itayumba.
 
Uko vizuri mtoa maoni.
Niongeze kidogo wanasiasa wasihodhi mchakato .Rasmu ya pili pendekezwa ya katiba mpya ya jaji warioba inatosha kuidhinishwa iwe ndio katiba ya Jamhuti ya Tanzania

Sent from my TECNO P701 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom