Kwanini jana na wala siyo Jumamosi RAILA & CORD walishindwa kesi ya URAIS wa Kenya!

Kwanini jana na wala siyo Jumamosi RAILA & CORD walishindwa kesi ya URAIS wa Kenya!

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
219,468
Reaction score
911,184
Kiini cha kesi ya Raila na CORD dhidi ya tamko la IEBC kuwa Uhuru Muigai Kenyatta alishinda Uraisi wa Kenya ni kuwa zilikuweko mbinu chafu za kuhakikisha mitambo ya IEBC haifanyi kazi hivyo hesabu za kura hazikufanywa na mitambo ila watu ambao walitumia mwanya huo kutengua ushindi wa Raila.

Ili kuthibitisha dhana hiyo Raila & CORD waliomba ifanyike
forensic auditing ya kuhakiki kila kilichofanyika IEBC. Supreme Court ya Kenya jana ilikataa kufanyika kwa zoezi hilo kwa sababu zifuatazo:-

1) Maombi hayo hayatekelezeki kwa kuwa yanahitaji muda mwingi zaidi ya siku 14 za kikatiba za kuusikiliza mgogoro tajwa.

2) CORD walikuwa na nafasi ya siku 16 tangia IEBC imtamke Uhuru kuwa kashinda uraisi sasa walikuwa wapi siku zote hizo kudai haki hizo mahakama Kuu ambako ndiyo wenye haki ya kiawali ya kusikiliza madai ya namna hiyo.

3) Maombi yao mahakamani hapo hayakuzingatia taratibu za kiufundi za uendeshaji wa suala hilo katika SUPREME COURT.

4) Maombi yao yaliwahusisha makandarasi wa IEBC ambao hawakuwashitaki na hivyo sheria hairuhusu kuwashurutisha watu au makampuni ambayo siyo sehemu ya mgogoro kutekeleza amri za mahakama bila kushirikishwa watajwa hao katika suala zima lililoko mahakamani.

5) Maombi hayo hayakuonyesha ni jinsi ipi mahakama itazitumia taarifa hizo na hivyo kunufaisha uendeshaji wa kesi husika. CORD walishindwa kuonyesha jinsi itakavyotumia manufaa ya maombi hayo na hivyo kuonekana walikuwa wanafanya kitu kinachoitwa ni utafiti au "
fishing expedition." Mahakama siyo mahali pa kufanyia utafiti ila kuamua mashauri tu kulingana na ushahidi ambao upo mahakamani hapo.

6) Fomu namba 34 na 36 zilitosha kulitathmini zoezi zima la uchaguzi kama ulifanyika kwa haki na tayari SUPREME COURT ilikuwa imetoa amri uhakiki wa zoezi zima ufanyike kwenye FOMU namba 34 na 36 ikiwa ni pamoja na vituo 22 vya kupigia kura ujumlishwaji kura urudiwe. Hivyo kufanya maombi haya kuwa yamepitwa na wakati.

7) Ratiba ya kulisikiliza na kuliamua shauri lenyewe lazima ufanyike ndani ya siku 14 kulingana na katiba ya Kenya hivyo hapakuwepo muda wa kulifanya zoezi la
"forensic auditing" tajwa ndani ya muda huo.


8) CORD walishindwa kuonyesha ni nani aifanye kazi hiyo ya
"forensic auditing" na kwa muda gani na atakuwa hana upendeleo kwa upande wowote na hivyo matokeo ya uchunguzi wake kuweza kupewa na nguvu ya sheria na mahakama ya kileleni.

9) CORD walishindwa kuonyesha mapungufu ya
Fomu na. 34-36 na hivyo kuhitajika uhakiki wa ziada kupitia "forensic auditing" tajwa.

10) Siku ya Jumatano na Alhamisi zilipangwa kusikilizwa kesi kama maombi ya CORD yangelisikilizwa basi ingebidi kesi ianze upya kabisa hata hivyo muda wa kufanya hivyo haupo kulingana na katiba.


Baada ya haya maelekezo ni wazi kuwa bila ya hiyo forensic auditing FOMU 34, 35 na 36 hazitakuwa na msaada kwa CORD maana kama zingelikuwa na msaada wasingewekeza sana nguvu zao kwenye forensic auditing ambayo hata matunda yake hawayafahamu yangelikuwaje.

Hivyo kauli za Raila kuwa alimshinda Uhuru kwa zaidi ya kura 1.3m alizitoa mfukoni mwake! Kama Raila angelikuwa ni mkweli basi angelianza kuutumia ushahidi tajwa leo na kesho na kuishinda kesi badala ya kuendelea kudai apewe ushahidi mpya ili athibitishe madai yake ambayo sasa imethibitika ni utapeli mtupu amekuwa akiufanya.Tegemea Raila kwenda Kibera Jumapili na kuanza kujenga mazingira ya rabsha ya kupinga uamuzi wa mwisho wa kupinga matokeo ya Uraisi wa kenya.
 
Raila round hii wanambana vyema coz wanamjua hachelewi kuanzisha machafuko kama kawaida yake .Chezea kikuyu !

Sijui kama kuna ukikuyu ndani yake ila nionacho ni kuwa Raila hana organizational skills za kuweza kufanikisha azma zake za kisiasa na mbinu zake za kuchoma madaraja ambayo kesho yake anayahitaji kuyapita ni udhaifu ambao sasa unamwelekeza kustaafu. Kenya is tired of his mischief and so is the rest of East Africa.
 
The Supreme Court has rejected Raila Odinga's application to admit additional evidence in his petition challenging the electoral commission's declaration of Uhuru as President-elect.
The judges ordered the 839-page affidavit to be expunged from the court records.
Earlier, the court struck out Mr Odinga’s application for a forensic audit of the IEBC Information Technology (IT) system.
The Supreme Court ruled that Mr Odinga's application was time barred and could therefore not be allowed.
The judges also rejected a request by Katiba Institute to be enjoined in the suit as 'amicus curiae' (friend of the court).


Kwa maelezo hayo hapo juu, inaonyesha IEBC wame collaborate na Supreme court kukataa maombi ya Raila & cord kwa maana kwamba wakikubali itakuwa aibu kubwa sana.
Hii inadhihirisha kwamba Wakikuyu na Wakalenjin ndiyo wenye hati miliki ya kuitawala kenya.

 

Kwa maelezo hayo hapo juu, inaonyesha IEBC wame collaborate na Supreme court kukataa maombi ya Raila & cord kwa maana kwamba wakikubali itakuwa aibu kubwa sana.
Hii inadhihirisha kwamba Wakikuyu na Wakalenjin ndiyo wenye hati miliki ya kuitawala kenya.


Siyo hivyo. Wenye hati miliki ya Kenya ni wakenya wote. Khoja zako nyingine ni za kuhisia tu na wala siyo hivyo hata kidogo.
 
Rutashubanyuma hii kitu imeshanichosha!! All in all Kenyata ndiye "Mshindi" hata kama kushinda kwake kuna walakini na jua kwamba mahakamani huwa haitafutwi haki bali ushindi wa kisheria!!
 
Last edited by a moderator:
Mungu nishamehe sioni why watawala wa Kenya always watoke kwa izo tribe mbili tuu!

Are they not Kenyans. I thought elections is about best candidates not detremining them according to their pedigrees?
 
Rutashubanyuma hii kitu imeshanichosha!! All in all Kenyata ndiye "Mshindi" hata kama kushinda kwake kuna walakini na jua kwamba mahakamani huwa haitafutwi haki bali ushindi wa kisheria!!

Nimepitia ushaidi wote wa Raila hawana khoja ya msingi ya kutengua matokeo husika. hata kinara wa mawakili wao amenukuu hukumu ya mahakama ya India ambayo nayo inalonga kuwa uwezekano wa kutengua matokeo ya uraisi ni pale tu ambapo kuna ushahidi wa sauti ya wapigakura kubatilishwa jambo ambalo siyo kesi hii.
 
Raila round hii wanambana vyema coz wanamjua hachelewi kuanzisha machafuko kama kawaida yake .Chezea kikuyu !


Kumbe Raila si mkomavu wa kisiasa. Jana wakati Kenyatta anaapishwa yeye yuko South Africa. Makamo wa Rais bw. Kalonzo Msyoka naye eti hakuwepo! Hawa jamaa wanaonekana wana kinyongo kweli kweli bila hicho kinyongo wangekaa na kuwakabidhi wenzao madaraka ni kuiona serikali yao ikimaliza muda wao hapo jana.
 
Mungu nishamehe sioni why watawala wa Kenya always watoke kwa izo tribe mbili tuu!

Mkuu awamu hii ni Raila aliyekosea mahesabu. Kumbuka mwaka 2007 Raila alivyodai ameishinda alikuwa na support ya Rutto. Rutto wakati huo alikuwa si ngulu wa siasa za Kenya lakini aliungwa mkono na jamii ya Wakalenjini. Mambo yakaenda lakini along the way Raila akakosana na Rutto na mwishowe kuwaundia zenge la ICC. Rutto akawa mashuhuri kwenye jamii nzima ya Kalenjini na kwa kuwa kalenjini ni kama kabila la tatu kubwa Kenya basi Rutto akawa ni King Maker. Na matokeo yake ni Rutto kuungana na Kenyatta kwenye Jubilee na kutwaa madaraka huku raila na Musyoka wakiweweseka. Kama Raila asingekuwa mgomvi na hivyo kuendelea na Rutto hakika sasa hivi tungekuwa na Rais Raila.

Raila ni mgomvi tu kuanzia Ford Kenya, New KANU, ODM. Hakai na watu wakamaliza salama.
 
Kumbe Raila si mkomavu wa kisiasa. Jana wakati Kenyatta anaapishwa yeye yuko South Africa. Makamo wa Rais bw. Kalonzo Msyoka naye eti hakuwepo! Hawa jamaa wanaonekana wana kinyongo kweli kweli bila hicho kinyongo wangekaa na kuwakabidhi wenzao madaraka ni kuiona serikali yao ikimaliza muda wao hapo jana.
watoto wa town (Nairobi) walishaapa kamwe Raila na vizazi vyake hata itawala Kenya maisha ! ,maandiko yanatimia taratibu
 
Back
Top Bottom