Kwanini Jf imejaa member waoga ?

Mtatumia mbinu nyingi kutaka tujulikane lakini mtachemsha .....



Kama umetumwa kawambie wana jf sio wa mchezo mchezo.


Humu jf ni noma unaweza tumwa kama hivi kutafuta taarifa, halafu bosi wako akatumia hizi hizi ID feki na mbinu fulani pia kutujuza wana jf.

Kwa hiyi kama umetumwa
Uache kihele hele
 
Ubaya ni kwamba mnataka kujifunza uinformer bila kutumia akili.
Uzuri ni kwamba tumeshawagundua.
 
Mala weka sehemu unakotoka umpate rafiki memba wa jf
Ooo weka jina lashule yako ya msingi uwapate ulio sijui nini......

Baada ya kukosa,

Oooooh jf ni waoga

Sasa kinachofuata hapa, sijui

Ni oooo

Utasikia nini sijui nini....
Bado kutuambia tuweke picha za viganja tuone kama vinafanana na mwenzio
 
Bado kutuambia tuweke picha za viganja tuone kama vinafanana na mwenzio
Mimi sasa hivi nilishazima hata kamela yangu ya mbele


Hawa watu hawachelewi kutuhaiti hapa.

Hawajui tunajaribu angalau kumsaidia Melo kutuficha??

Hawajui kama hata gwanda za jeshi zimetawaliwa na kijani ili iwe rahisi kujificha vichakani!?


Utasikia futia kio cha simu yako kwa nywele na upige picha vidole gumba?


Sasa hivi tutazikimbia hizi simu za kugusa, make hawa ambao wanadumisha urafiki na mchina asee wanaweza fanya maajabu yao
 
Watu wana mbinu sijawahi ona


Cc Smart911
Hapo ndio watajua aliegundua kufuli, mwenzake aligundua funguo malaya.

Aliegundua bunduki,
Mwenzie akagundua vikinga risasi

Ukigundua kutuhoji,
Sie tunagubdua kukupa majibu unayoyapenda lakini ya uongo.


Maanake hizi juhudi zooote ni kutaka kuficha ukweli, basi sili ya kuficha ukweli ni uongo tu na si vinginevyo
 
hao waliokutuma wenyewe nao pia wanatumia fake I'd humu
waambie wao waanze kutumia I'd zao halisi kwanza kisha ndio uwafnyie hiyo kazi yko but sidhani kama utafaulu pia
 
Kwanza nenda kajifunze maana ya online forum.ukishajua ndo utaelewa kuwa kuna utafauti kati ya jamii forums na hizo soshonetweki kama fb na insta.ukishajua ndo utafahamu kuwa nyinyi mnaoweka mapicha na majina yenu halisi ndo mnaokosea.

Akhsante kwa Kutuelimishia ' Mpuuzi ' Mkuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…