Kwanini Kenya itambulike kama taifa linalozungumza Kiswahiili na si Tanzania

Kwanini Kenya itambulike kama taifa linalozungumza Kiswahiili na si Tanzania

Chagga King

JF-Expert Member
Joined
Jul 6, 2011
Posts
1,866
Reaction score
1,076
nimekuwa nikipenda kutumia kiswahili sana kwenye simu hasa katika miongozo mbalimbali katika simu, katika hali ya kustaajabisha, hasa pale ninapochagua lugha, ni dhahiri kuwa lugha ni utambulisho wa taifa fulani, na hata kama lugha hiyo itatumika na taifa zaidi ya moja basi itaelezwa jina la lugha na taifa lenyewe mfano, kiingereza cha uingereza (British english) kiingereza cha Australia (Australia English) kiingereza cha marekani (American English) and e.t.c.

Hali ni tofauti kwa lugha ya kiswahili, unapochagua lugha ya kiswahili hasa kwenye simu, unakuta taifa la kenya ndilo linalowekwa kama wazungumzaji wa lugha hiyo. nimesikitika sana kwani kiswahili pamoja na kwamba kinazungumzwa pia nchini kenya, lakini ni lugha mama ya katika nchi ya Tanzania na ni fahari ya Tanzania, iweje fahari yetu imezwe na nchi nyingine?, yaani isitambulike kama ni lugha iliyochimbukia nchini Tanzania?, maana katika mitandao mbalimbali lugha ya kiswahili unakuta imewekewa BENDERA ya kenya, na hili nimeliona mara nyingi nikiwa naperuzi.

Pamoja na kwamba wakenya wamekuwa kimbelembele kujifanya kuwa wao ndiyo wazungumzaji halisi wa lugha ya kiswahili, hata kufikia hatua ya kuwa watafsiri wa maneno katika kamusi mbalimbali na pia kuweka maneno ya kiswahili katika vifaa vya kielektroniki kama vile simu, wamekuwa WAKIHARIBU MANENO YA KISWAHILI katika uandishi na matamshi yake, hivyo kupoteza maana kabisa na kufanya lugha ya kiswahili kuiona mpya na ngumu katika vifaa hivyo.

kwa kuwa mimi sijafanya utafiti rasmi, lakini ninaweza thibitisha haya, maana mifano na ushahidi vipo vya kutosha, ningependa wewe kama mtanzania, taasisi za kiswahili, na serikali kwa ujumla kuchukua hatua stahiki ili kutetea FAHARI yetu ya lugha ya kiswahili kwa heshima ya Tanzania.

tunyang'anywe madini na rasilimali nyingine, na kugha ya kiswahili tunyang'anywe vilevile?. haiwezekani.

.....ieleweke kuwa suala la Kenya kutangaza lugha ya kiswahili ni sahihi kwakuwa inasaidia katika ukuaji wake, tatizo ni kuwa inapotosha utaifa wa lugha hiyo ambayo inazungumzwa kwa ufasaha zaidi nchini Tanzania.

invisible kama utaona kuna umuhimu wa hili suala naomba ulitafutie namna hata kwa kuanza kuubandika (stick) huu uzi ingawa najua kuwa sijauandika vizuri kwa sababu ya uharaka.

cc: invisible
 
Una haki ya kulalamika kaka lakini pia WATANZANIA tumezidi kuzorota, Tumelala usingizi wa Pono, Tumeendekeza siasa na ufisadi ktk kila idara acha wajanja wenye kujua nini maana ya uzalendo waendelee kujifanyia yao... na bado, Kwa tanzania yangu hii na viongozi wangu wa namna hii tutaanza kudhulumiwa mpaka lugha za makabila c kiswahili tu kudadadeki.
 
Kenya imeipokonya Tanzania si kiswahili tu ila pia mlima Kilimanjaro.Makampuni/Mashirika makubwa kwa mfano Google, Microsoft,Yahoo yanapohitaji kutumia kiswahili kwenye kazi zao hutumia wataalamu wa kiswahili kutoka Kenya.Sababu kubwa ni kwamba wakenya ni hodari sana kujitangaza na kwa kuwa Kenya ilitokea kuwa koloni pendwa la waingereza wakenya wana aina ya kaupendeleo kimataifa.Hata kwenye utalii wanaonekana kwenye kioo cha mataifa kwamba wana vivutio bora na huduma zaidi afrika mashariki.Yote haya ni kwa sababu wanajua namna ya kujitangaza.Kwenye kiswahili hata waalimu wanaofundisha kiswahili kwenye vyuo mbalimbali duniani ni kutoka kenya.Tanzania kimataifa ni nchi iliyolala isiyojua kujitangaza.
Kwa hiyo kuanzia miaka mingi iliyopita dunia inaelewa kwamba kenya ni taifa la kiswahili, pia ukitaka kupanda mlima kilimanjaro unaanzia Nairobi Kenya.
Na hali hii itaendelea na kuwa kubwa zaidi kama Tanzania itaendelea kulala!
 
Sasa hii ni akili waziri wa utalii kuchukua mwanamke street na kwenda naye USA kutangaza utalii?. Ndio uone tulivyo mapompopo.
 
Mbona na mimi wanantumia kutafsiri baadhi ya maneno au sentensi......
 
Nirekebishe misconception moja hapa. Na kabla sijasema, mimi si Mkenya. Mbongo wa kutokea kusini kabisa mwa nchi. Chimbuko la Kiswahili si Tanzania. Chimbuko la Kiswahili pwani ya Kaskazini Kenya karibu na mpaka wa Somalia. Nikiwaelekezeni kwa wataalamu wa nje, mtapiga tena kelele. Waandishi kadha wa Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili na sasa Taasisi ya Taaluma ya Kiswahili (UDSM) wameelezea hayo na ushahidi uliotumika kuthibitisha hilo.
Kuwa na idadi kubwa ya wasemaji wa Kiswahili hakuna maana ya kwamba hapa kwetu ndiyo chanzo cha lugha hiyo. Marekani ina wasemaji wengi wa Kiingereza, walakini Marekani si chanzo cha Kiingereza. Na kwa Wamarekani kuipuuzia lahaja ya wasemaji wa Australia au Uingereza ni jambo la kustaajabisha. Lakini linatokea kila siku.
 
Kama madini yapo na hakuna processing unit. Wakichukua Kiswahili ndio unaumia zaid???!!!
 
Hata mlima kilimanjaro wazungu wanajua uko kenya
 
kwa upande wangu sioni tatizo kwa wakenya. tatizo lipo kwa sisi watanzania. tupo nyuma sana na akili zetu zinafikiria mambo ya udaku kuliko mambo muhimu kwa ustawi wa nchi yetu na dunia kwa ujumla. ni ukweli husiopingika hata kwenye mtandao taarifa kuhusu lugha ya kiswahili ni chache ukilinganisha na kiingereza. ukitaka kuamini hili, jaribu kuperuzi (kusearch/google) swali la kiswahili utapata jibu mwenyewe. kama sisi tunashindwa kujitangaza na kukitangaza kiswahili si dhambi wala kosa wao kufanya hivyo. ni wakati wetu sasa kuweka taarifa za kiswahili mtandaoni na kuzitangaza na si kutumia muda mwingi kwenye mapenzi na udaku wa akina dimond na alikiba.
 
Kiswahili ni lugha ya Afrika mashariki, sio kenya wala tz pekee. Sio vema Kusema Kiswahili ni ya Tz ikiwa pia Kenya kuna waswahili halisi.
 
Kiswahili ni lugha ya Afrika mashariki, sio kenya wala tz pekee. Sio vema Kusema Kiswahili ni ya Tz ikiwa pia Kenya kuna waswahili halisi.
Uko sawa mkuu, Kiswahili ni Lugha ya Pwani hii, kuinasibisha na kundi fulani pekee ni makosa. Wapo pia wasemaji wa Kiswahili wanaopatikana Kongo MAshariki, hujulikana kama Wangwana.
 
kiswahili chimbuko lake mombasa- kimvita.
iwe una fanya research kabla kutoa mada
 
kiswahili chimbuko lake mombasa- kimvita.
iwe una fanya research kabla kutoa mada

Usiseme Mombasa sema Zanzibar mzizi wa kiswahili ndipo ulipotokea Mombasa,Unguja,Pemba all ni Zanzibar ila mafisadi wenu wakauza Mombasa ;-);-);-)
 
Back
Top Bottom