Kwanini kila pakiboreshwa wateja wanakimbia?

Ni kama mimi vile ambavyo sioni umuhimu wa kwenda hata Mlimani City eti nikazagae tu bila ishu ya maana. Ila kunao vijana ambao wao ndio sehemu yao ya kutakatisha majina kwa vibinti.
MTU anaenda kutwa nzima anakunywa Maji eti Staff
 
Wateja hawapendi usafi, wanahisi utapandisha gharama za vyakula, ni hilo mkuu hakuna mchawai[emoji1787][emoji1787]

Sent using Jamii Forums mobile app

Weka tangazo la bei zako nje, watu wengi wana associate usafi na bei hivyo wanaogopa Watangazie kama wiki mbili tatu wajue bei ni ile ile.
 
Wateja wako wanajiona hawastahili kula hapo, wanataka sehemu chafu chafu ili waendane na hali zao, wanajua labda bei itapanda.
Kabla ya kuboresha ungeongea na wateja zako kwanza ndo upabadilishe.
 
Huenda kuna marekebisho umefanya lakini sio rafiki kwa wateja na siku zote tabia za wateja hubadilika kila uchao, labda umeboresha mazingira ukasahau kuboresha chakula kutokana na kwamba radha au matarajio ya mteja ni kukidhi haja(satisfaction).
Ushauri: unaweza ukafanya utafiti wa muda mfupi ujue ni kwanini wateja walihama, utafiti huo utakuwa ni kuwauliza wateja waliokuwepo awali baadhi tu(used to use customers) ili uweze kupata maoni, ushauri na mapendekezo yao jinsi gani ya kuwavutia tena. Lakini pia weka mlango wazi kwa wateja waliopo ili wakupe feedback jinsi gani wanavyoiona huduma?, wanaipokeaje huduma? Je, wanaridika? majibu ya maswali haya machache yatakupa mwanga kidogo katika namna ya kuongeza kile kisichokuwa na kupunguza kisichotakiwa katika utoaji wa huduma.
vile vile kuna kitu kinaitwa customer relationship management huenda pia hakipo katika biashara yako ndo maana wanakimbia, kwahiyo jaribu kuchunguza vizuri.
 
Watu wa marketing tunaita CONSUMER BEHAVIOUR sio psychology.
 
Itakuwa Wateja wako ni wale mahardcore sio mabishoo ,hii inanikimbusha mgawanyiko wa wanafunzi A level na O level yaani ukienda kula chipsi au kwenye vibanda vizuri vizuri tunakuona bishooo tu

Njoo uku uswazi kwenye mihogo na kachumbali mixer ugali

So Wateja wako wengi walikuwa wazee wa ubanda na wewe ukawaletea ubishoo mambo ya masaki wakaamua watafute sehemu nyingine inayoendana nao
 
Umesomea marketing wapi ambako hukusoma CONSUMER BEHAVIOUR.
Sio kila kitu kiandikwe unavyotaka wewe. We ulisikia wapi psychology ya wateja?
 
Wamebaini hila zako.Lengo ni kupandisha bei za vyakula.
 
Ungewaandaa wateja kujua namna unavyotaka kuboresha. Yaani kama mwezi 1 hivi kabla wakati wa kuwahudumia unhekuwa unawasemesha kuwa "ngoja niwawekee feni na viti vizuri hapa mzidi kufaidi na ninavyowapenda siongezi bei ya chakula chochote."

Yaani ile kiutani utani. Ungeawaandaa kujua kwamba kuna maboresho yanakuja ambayo hayaathiri bei.

Contingency plan: weka bei elekezi nje...kama ni mafundi wafate site kuwaambia
Na watakaokuja jenga nao urafiki ili wafikishe taarifa kwa wengine kuwa bei ipo vile vile.
 
Hao aina ya Wateja uliowataja wengi wao ni vijana ambao hawapendi kukaa baa za wazi hasa zenye mionekano mizuri kutokana na kwamba watakutana na Wateja wa rika ya kati ambao wengi wao(wanavipesa pesa) wanakuwa wanyaji wazuri ambapo watawatawala na watashindwa kuwa huru kama inavyojulikana vijana wanapenda kuwa huru kufanya mambo yao mengi ya kijinga jinga

Kumbuka hawa rika ya kati wengi ni wajivuni na wanawadharau hawa vijana so automatically jamiii zinajigawa kwa hivo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…