Kwanini kitabu cha Muongozo wa Utoaji Haki za Wanawake kimeandikwa kwa Kiingereza

Kwanini kitabu cha Muongozo wa Utoaji Haki za Wanawake kimeandikwa kwa Kiingereza

zandrano

JF-Expert Member
Joined
Jan 24, 2017
Posts
7,893
Reaction score
8,816
Jana Mhe .Rais Samia alizindua Kitabu cha muongozo kwa Majaji na Mahakimu kinachohusu jinsi ya utoaji wa Haki za wanawake na watoto ktk kesi za mirathi ndoa na talaka n.k.

Sisi wananchi tunashukuru kwa hatua hiyo lakini tumeshangaa sana kuona kitabu hicho kuandikwa kwa lugha ya kizungu wakati haki zilizo andikwa ni za wananchi wa Tanzania ndio maana Mhe. Rais akasema kitafsiriwe haraka kwa lugha ya kiswahili, lkn swali la kujiuliza hawa waandisha wa kitabu hiki waliwalenga kina nani haswa? Watanzania au Wazungu?!

Hata kama walifadhiliwa na nchi hisani lkn haki zilizo kusudiwa ni za Watanzania hivyo ilikuwa ni lazima kitabu hicho kuandikwa kwa lugha ya Kiswahili na sio kizungu.

Viongozi wetu haswa Muhimili wa mahakama acheni kuwahadaa Watanzania; kama kweli lengo lenu ni kutoa haki za Watanzania basi tumieni lugha ya Watanzania, acheni kuwafurahisha wageni na kuwaumiza Watanzania.

Haki za Watanzania lazima ziandikwe kwa lugha ya Kiswahili
 
Tunasubiri uzinduzi wa kitabu Cha mwongozo wa utoaji haki kwa Wanaume.
 
Kinacho washangaza na kuwaduwaza Wananchi walio wengi ni kuona wanatengwa kwa kuandikiwa mambo muhimu yanayo husu Haki zao kwa Lugha ya Kizungu badala ya Lugha yao ya Kiswahili!

halafu wakati huo huo eti tunaambiwa Haki hizo zilizo andikwa kwa Lugha kizungu zinawahusu watanzania!!! aisee!!! kweli kabisaa

Nchi yetu imepata uhuru tangu 1961 lkn bado tumetawaliwa uwezo wetu wa kufikiri wenyewe kwa lugha yetu wenyewe!

Bado mpaka leo Jaji au Hakimu wa Kitanzania anajisikia fahari kumpa Haki mtazania mwenzake kwa lugha ya kizungu!!
 
Jana nilibahatika kusikiliza hotuba ya rais katika uzinduzi huo. Nilichojifunza ni kwamba tuna rais asiyejiamini, asiyeamini anayoyasema, anaongea bila mpangilio. Kifupi nimethibitisha kuna ombwe kubwa pale
 
Kuna atakayenunua kweli hicho kitabu? Au kinagawiwa bure na kulazimishwa kusoma?
 
Kuna atakayenunua kweli hicho kitabu? Au kinagawiwa bure na kulazimishwa kusoma?
wanajitahidi kuiuwa kabisa Lugha ya Kiswahili.
Lugha ya Kiswahili inazungumzwa na kueleweka kwa watanzania 99%.
Kizungu kinaeleweka kwa 1%
lkn cha kushangaza haki za watanzania bado zinatolewa kwa lugha ya kiingereza!!
 
Back
Top Bottom