Kwanini klabu ya Yanga inapendelea kuweka kambi nchi ya Uturuki?

Jacobus

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2011
Posts
4,703
Reaction score
1,724
Wakuu, japo tunapenda kuwa kama Ulaya lakini hili la timu ya Yanga kuweka kambi nchini Uturuki haliingii akilini. Klabu yenyewe haina uwanja wa mazoezi lakini inatumia pesa nyingi kwenda huko hata kwa mechi inayochezwa hapa hapa! Ama pana zaidi ya mazoezi?
 
Upatikanaji wa tende na haruwa kule Uturuki ni easy sana compared to Tanzania. Hilo tu!
Duh! Hii kali, kumbe wanachofuata sio soka!!!!!!!!!!?
 
Washindwe kuwa na uwanja wao na hata kwenda uturuki washindwe?
Angalia gharama mkuu ya kuipeleka timu huko na kuanzisha ujenzi wa uwanja wao kipi kiwe kipaumbele?
 
Angalia gharama mkuu ya kuipeleka timu huko na kuanzisha ujenzi wa uwanja wao kipi kiwe kipaumbele?
Iwapo pesa ni ya klabu ni sahihi kwa usemalo lkn kama ni pesa ya mtu.basi pesa inatumika sawa na hitaji la huyo atowae.
 
Kwa mfano, wewe ulikuwa unapendekeza waweke wapi Kambi?
 

Choko choko kutoka matopeni...mwambie Manara amuulize Muro halafu mpate majibu pendwa mje tuyajadili....oooh Muro kakiuka haki za wanawake, mara sijui Muro anajisikia....0382 300 231 hiyo namba ya Muro.
 
Sababu ni ulaya tu, na Jerry ametoa onyo kwa wanaopenda kuizodoa Yanga eti haina uwanja, wakati wao hufanyia mazoezi ulaya. Huku wengine wakienda ulaya wanaenda kucheze mpira wa kulipwa.
 
Sababu ni ulaya tu, na Jerry ametoa onyo kwa wanaopenda kuizodoa Yanga eti haina uwanja, wakati wao hufanyia mazoezi ulaya. Huku wengine wakienda ulaya wanaenda kucheze mpira wa kulipwa.

Uturuki ni ulaya Mkuu?
 
Kule ndio Center ya dope(Madawa ya Kulevya) kutoka Iran, Pakistan na Afghanistan
Kwa iyo nadhani wanakuwa wanaenda kuwashauri waache kufanya iyo biashara kwa sababu wanakuwa wanamkosea mwenyezi mungu. Uturuki haha [emoji23] haha [emoji23] haha [emoji23] haha [emoji23] haha [emoji23] haha [emoji23]

MO dewji nae akichukua timu ya Simba Sport club. Itakuwa inaenda Colombia kufanya mazoezi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…