Kwanini Klopp anapewa Kocha bora wa ligi ikiwa wao sio mabingwa?

Unashinda makombe mawili kwa penati
Huna kombe la EPL
Unakuwaje kocha wa ligi kuu?
.
Basi La liga wampe Xavi kocha bora maana kaifikisha timu nafasi ya pili huku timu ikitumia vijana wengi tena wakiwa na hali mbaya ya kiuchumi na kutafuta vigezo ambavyo sio kubeba ubingwa katika michuano husika IMO

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Mkuu hii tuzo wanaangalia epl tu ...


Narudia Tena wanaangalia performance kwa epl pekee yake ...


Uefa watatoka tuzo yao kama klopp akichukua uefa ....


Usilete mambo ya uefa kwenye PL ...


Pep kafeli uefa na hawezi pata tuzo yeyote lakin epl kampiga chin klopp na hio tuzo aliyochukua klopp ni ya pep kabisa ....

Note; hio tuzo hawaangalii fa ,carabao Wala uefa ....wanaangalia PL pekee ....
 

Unaweza kusema hivyo lakini tukiangalia overall perfomance ya hao makocha wawili hata wewe ukiweka ushabiki pembeni utagundua kwamba Klopp anahitaji kupongezwa kwa aina ya kikosi alichokuwa nacho na budget yake ikilinganishwa na city.


Sasa hata hapo Epl pep kamzidi kipi Klopp? Maana hata huo ubingwa ulikuwa ni wa kupimuliana mpaka dakika za mwisho, head to head kati ya klopp na Pep kwenye ligi zimekaaje?
 
Hii hapa list ya Makombe ya kandanda most expensive Duniani.

10. English Premier League trophy – $10,000
9. UEFA Champions League – $15,000
8. Bundesliga Meisterschale – $57,102
7. Serie A trophy – $66,000
6. Africa Cup of Nations trophy – $150,000
5. Ballon d’Or trophy
4. The FA Cup trophy – $1,180,000
3. UEFA Europa League trophy – $4.5 million
2. Copa Libertadores trophy – $8.5 million
1. FIFA World Cup trophy – $20,000,000

Source: 247NEWS
 
Kwanza kombe la FA ndio kombe la pili kwa thamani duniani baada ya world cup.

Pili klopp anatumia hela kidogo kuliko pep.
Wee nae ni mwana michezo? [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
UEFA CHAMPIONS LEAGUE dola elfu kumi na tano?
 
Duuuu fake fake fake fake [emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]
 
Issue ni kuwa kawin PL [emoji28]

Kwenye football always the first is the first waliobaki wote ni loser ....hii haijalishi ni namna gani mwenzio kachukua ubingwa ....

Ndio maana katika historia ya vitabu msimu wa 2021/2022 city ndio ataongelewa kama bingwa na sio liverpool, Liverpool ni loser na habari zake zimeishia pale that is football [emoji28]...!

Ni kama uefa ,hata kama umefika final kama hujachukua Hilo kombe wewe ni loser tu ,haijalishi ulimiliki mchezo ,umekosa penalty ,umegonga mwamba mara kumi ,issue ni kuwa kama hujachukua kombe habari yako imeishia hapo na habari ya mjini itakuwa kwa yule aliyeshinda ....

Ukija H2H ya pep na klop msimu huu ni

Liverpool Vs man city (2-2)

Man city Vs Liverpool (2-2)

Yaani kifootball hiyo tuzo ni ya pep ,ila wameamua kumpoza klopp tu .....
 
Hii list inaonyesha thamani ya makombe sio kiasi anachovuta bingwa. Bingwa wa UEFA ndiye anayevuta mkunjwa mrefu zaidi.
 
Hapo umepuyanga

Kwenye epl msimu wa 2020/21​



Liverpool 0 - 1 Fulham, ilikuwa 7/3/2021


Liverpool 0 -1 Chelsea , ilikuwa 4/3/2021
Hajafungwa Anflied uwe unatuliza kichwa
 
Thibitisha unachosema sio porojo
 
Kwani team ikichukua kombe ndiyo inachukua tuzo zote?
 
Kama huoni uhalali wa klopp kupewa tuzo eti kwakua tu pep kachukua tena kwa tofauti ya point moja, basi hata zile tuzo za kocha bora wa mwenzi angepewa yeye zote kwakua alikuwa at the top😂. Wenzako hawaanalyse ubora wa kocha kizembe hivyo.

Pep hafati kwa klopp ikiwa utawatazama kimafanikio katika msimu huu, najua wewe ni kinda wa city lakini huu ndo ukweli.

Ikiwa klopp utamuita loser kwenye UEFA pamoja na kufika final, pep utamuitaje kwa jinsi alivyopoteza nusu fainali ambayo ilikuwa mkononi mwake mpaka dakika ya 80?

Angalia performance yao katika mashindano yote ambayo walishiriki kwa pamoja (namaanisha yote) kisha urudi kumdharau klopp tena.

Angepewa pep au klopp kama hivi bado hakuna sababu ya malalamishi, wamefanya vikubwa kwa pamoja msimu huu.
 
Mkuu Soma maandishi yangu vzuri ...

Pep ni loser uefa mwaka Jana ndio maana habari za man city ziliishia pale na Chelsea alikuwa talk of the town ,....

Kloop ni loser kwenye PL na talk of the town ni man city ,hii Haina ubishi ..kwenye league always the first is the first wengine wote ni loser tu ...

Kloop ni loser kwenye uefa 2019 ndio maana baada ya ile game madrid ndio ikawa habari ya mjini ....

Usianze kuleta huruma kwenye football kama ukishindwa unakaa pembeni na winner ndio anaongelewa that is football ....hakuna mtu atakayepoteza muda kufuatilia et ulikuwa unakaribia kuchukua kombe ,sijui kwa point 1 au GD kiufupi wewe ishakuwa loser kaa pembeni [emoji28][emoji28][emoji28]


Harafu ukiaanza kuleta debate ya pep Vs klopp basi unajidhalilisha mkuu[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]....

Pep ni level nyingine kabisa ,kwa kila kitu [emoji28]....

Hiyo uefa unayoisema pep kashaandika historia kitambo ....

Kloop kachukua hiyo uefa akiwa Liverpool mbele ya Spurs 2019 ,kitu ambacho pep kashafanya kitambo wakati klopp Bado anahangaika na Mainz huko Germany ....
 
Thibitisha unachosema sio porojo
Hivi mkuu huoni hata jina " premium league manager of the season "[emoji28][emoji28][emoji28]

Mashindano ya fa yapo hapo ?

Mashindano ya carabao yapo ?

Mashindano ya eufa yapo hapo ?

Mashindano ya Europa yapo hapo?

Mashindano ya uefa conference league yapo hapo ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…