Kwanini kocha wa SIMBA anakua mzito kumuingiza Medie Kagere

Airmanula

JF-Expert Member
Joined
Nov 30, 2016
Posts
3,527
Reaction score
5,762
Tuliongalia game ya Leo, Simba dhidi ya Plateau ya Nigeria, tunashangaa kuona kwanini Kocha ameona kabisa watu hawa wawili, Boko na Mzamiru wamecheza fyongo lakini anakua mzito sana kufanya maamuzi ya kumtoa haswa Boko na kumuingiza Medie Kagere

Tunajua MK 14 uwezo wake mkubwa wa kuona nyavu na kufunga magoli, na pia uwezo wake mkubwa wa mechi za kimataifa, sasa kwanini inakua ngumu sana kocha kumpanga, hajaona aibu anamuingiza Kagere dakika ya 89 kweli?! Au ndio kupigana "misumari"

Boko Ni mchezaji mbovu. Mnaokaa naye mfikishieni salamu hizo, wakati mwingine aone aibu mwenyewe aombe kutoka nje sio kung'ang'ania huku akijua hafanyi lolote uwanjani.

Hili jambo kwa mechi za mbele za kimataifa litakuja kutugharimu , pale ambapo kocha unatakiwa kufanya maamuzi ya haraka na ya muhimu lakini sababu ya ulimbukeni unachelewa na kuigharimu timu na kutolewa nje ya michuano.
 
Na hitari kuwashobokea wachezaji ambao unaona kabisa wamechemsha huku nje una Kagere,Kahata na Ndemla!
Huyu mzungu huwa sikuelewi kabisa!
Hii Timu akipewa Julio ...mhamasishaji !
Makundi tunaenda😂
 
Yule kocha atakua pale kwa mpango wa mtu si bure, btw tumevuka tunasonga mbele ila kocha abadilike vinginevyo atakuja kutupa aibu sie mashabiki. Mechi ya leo ilitakiwa tushinde goal tatu kama hizi sub zingefanyika
Bocco[emoji680]Kagere
Dilunga[emoji680] Morison/Kahata
Mzamiru [emoji680] Ndemla.
All in all nmpongeza Nyoni ameonesha utulivu na ukomavu wa hali ya juu.
 
Kacheze wewe
 
Huyu kocha ngoja tufungwe atatoka kwa lazima, haiwezekani bocco ananguka tu uwanjani anamwacha kagere benchi,

Mchezaji analipwa pesa nyingi anaishia bench qmmke zake refa
 
mnajifanya makocha kumbe atatim yamtaani kwenu ujawai isaidia
 
 
Huyu kocha ngoja tufungwe atatoka kwa lazima, haiwezekani bocco ananguka tu uwanjani anamwacha kagere benchi,

Mchezaji analipwa pesa nyingi anaishia bench qmmke zake refa
Tukishafungwa hata akitoka tayari anakuwa keshatugharimu. Dawa aondoshwe sasa hivi kabla hajatufelisha. Kagere si wa kuingia dakika ya 89 tena team ikiwa haijafunga goli.
 
kimoko
 
Kuweni na heshima bas kwa John Bocco hampaswi kumbeza mfungaji bora wa mda wote
 
Nyoni alifaa awe nahodha anajua kuongoza na kuituliza timu niliona alivyomfokea Morison alipofanya upuuzi
 
Mm pia bado naamini kocha hawatumii ipasavyo baadhi ya wachezaji....kuna wachezaji wanapata nafasi...uwezo wao wa kawaida.... kuna wachezaji wana uwezo mkubwa wanakaa benchi....hawa wanaigeria hawana kiwango kabisa... tulitakiwa tuwapige 4-0
 
Mm pia bado naamini kocha hawatumii ipasavyo baadhi ya wachezaji....kuna wachezaji wanapata nafasi...uwezo wao wa kawaida.... kuna wachezaji wana uwezo mkubwa wanakaa benchi....hawa wanaigeria hawana kiwango kabisa... tulitakiwa tuwapige 4-0
Anaua viwango vya wachezaji makusudi, Rashid Juma, Shibob alikuwa hawapangi sasa hivi ni Kahata na Kagere hata Fraga alianza kucheza baada ya Mkude kupata majeraha.
 
Anaua viwango vya wachezaji makusudi, Rashid Juma, Shibob alikuwa hawapangi sasa hivi ni Kahata na Kagere hata Fraga alianza kucheza baada ya Mkude kupata majeraha.
Kweli kabisa.... angalau hata dk 15 za mwisho....na hawa walioko kwenye ubao waingie.....unakuta walioko ndani wamezidiwa....au timu inaongoza...kocha anakomaa tu....kahata... Bwalya wote bado wana nafasi ya kuanza
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…