Kwanini kuchelewa kupata mtoto kunaweza kuvuruga ndoa?

Aseeee!
Ngoja nitafute nauli...nitarudi hapa.
 
Kwa sababu wanaume ni wajanja, hata akiamua msipate mtoto anaenda kujilipa mtaani watoto wake kadhaa afu anakuletea kitambi chake wewe ukitunze.

Mkija anza kuzaa wewe mama unakua unalea wajukuu zako wakati mwenzio ana wajukuu na watoto.

Ku-adopt kwa kacha ya kiafrika, si bora kuchukua watoto wa ndugu kama dada/kaka na kuwalea, it is not our thing to adopt
 
Polen badada mnaotumia dawa za kinga za mimba pasipo mtaalam, ila izi dawa jaman c nzuri kabisa! kuna jirani yangu ye na mke wake wana watto wawili bt baada yakutumia izo dawa wakaacha ili watafute mtto wa 3 ngoma haishki! mpka saiv ni miaka 3 mwanamke hatumii kinga yoyote na mimba haishki! so bora ata yy anao 2 wakuzuga, je ambaye hana! wengi wanaachanaga!
 

Bila 'kutaka' mtoto/watoto?...nadhani ni wachache sana 'wasiotaka' (na hasa wengi ni wale wanaooana katika umri mkubwa say mume 50 mama over 45!), lakini kwa vijana below 35 sidhani kama kwa huku kwetu ni wengi(kama wapo) wanaoamua kuoana bila ile hamu ya kupata mtoto.

Kama kuna nia ya kupata mtoto/watoto, hata bila ya msukumo kutoka nje bado naamini wanandoa wengi wangependa kupata mtoto mapema tu baada ya ndoa (ukiacha cases chache ambapo kutokana na majukumu mengine kama shule nk pengine wanaweza kujichelewesha kidogo). Sasa hapa ndipo kwenye chanzo cha frustrations katika ndoa....wakati mwingine mnataka mtoto lakini haji kwa wakati mnaotaka na waktai mwingine hospitali wanasema hawaoni tatizo kwa mmoja wenu na kati yenu!

Adoption? Sio ya kiafrika! Objective huwa ni 'kuzaa' sio 'kulea'.

Kuna mzee mmoja jirani yetu aliwahi kunisimulia kuhusu ndoa yake. Yeye alioa akiwa kijana tu...wakakaa na mkewe kwa miaka kumi bila kupata mtoto. Baadae wakaamua kuachana na kwa bahati kila mmoja akafanikiwa kupata mwenza mpya...na katika hali ya kushangaza kila mmoja akapata 'watoto' na huyo mwenza mpya! (kuelezea hili baadae nilikuja kufikiri pengine kulikuwapo na tatizo la rhesus factor, ambayo kwa sasa nafahamu ni tatizo lenye suluhu ya kitabibu). Lakini sio mara zote kuachana kunaweza kuleta matokeo mazuri na ukiweka na factor ya imani/dini inaweza kuwa complicated...so wanaume wengi huishia kutafuata nyumba nyingine/ndogo!
 

Hapa bongo ni rahisi foregners kuja na kufanya adoption kuliko mzawa kwanza utapingana na familia, mfano mzuri ni mimi ninamiika 9 kwenye ndoa sijapata mtoto na wife haelewi wala nini nikizungumza adoption, pili ukienda ustawi wa jamii nao wanakatisha tamaa bila sababu za msingi. Kiujumla jamii yetu hapa bongo ni bado sana kwenye suala zima la adoption. Sasa kwangu miye inakuwa changamoto sana mpaka wakati mwingine kufikiria kuzaa pembeni ingawa nitakuwa simtendei haki mwenzangu, inachanganya sana yaani
 
MKJJ wewe una mtoto?
 
Uislaam unatowa jibu zuri sana kwa hilo. "Ruksa" kuoa mpaka wanne. Hapo kama tatizo ni mwanamme litajulikana tu, hata kama hataki kwenda Hospital.

Na jibu la pili ni kuwa Uislaam unaruhusu mwanamke "kupewa talaka" ikiwa mumeo hana uwezo wa kukuzalisha.
 
Duh!

Haya weh!
 
..........Hili ni jaribu lingine la ndoa, ujue kipindi cha uchumba watu mnakuwa na malengo kwa tuzae watoto kadhaa..........sasa mnaingia kwenye ndoa miaka inakatika bila mtoto, aisee ni jaribu gumu mno.

Mie naona bora watu wasiwe wanazungumzia idadi ya watoto wala kuzaa kipindi cha uchumba, watu waamue kuishi pamoja kama mke na mume na kufanya watoto ni majaaliwa.

.......Adoption ni nzuri, ila mtoto wa kumzaa ana raha yake, una adopt mtoto na bado atakuja tu kusema kwa watu kwamba yeye ni adopted.
 
Kwani akisema kwa watu ni adopted kuna ubaya gani?
Kwani mtu anapoadopt anajaribu kutrick watu wengine waamini kwamba yeye ndie aliezaa?
 
.......Adoption ni nzuri, ila mtoto wa kumzaa ana raha yake, una adopt mtoto na bado atakuja tu kusema kwa watu kwamba yeye ni adopted.
[/QUOTE]

Pretta,
Adoption sio siri kwamba mtoto asiseme ni kitu cha wazi na kinatakiwa kueleweka kwa namna hiyo, ndiyo sababu inasumbua kwa jamii yetu kufanya adoption kwa hofu kama hizo
 
Kaaaazi kweli kweli.
 
Tatizo letu wabongo kuolewa ni sawa na kuzaa. Mimi nilipata first born wangu baada ya miaka minne ya ndoa kwa sababu kuzaa hakukuwa sababu ya kwanza iliyotufanya tuoane.

Tulioana ili tuwe closer; na sote tulikuwa na majukumu ambayo yalitufanya tuone kuwa inafaa tusubili kwanza kabla ya kufikiria swala la kuwa na watoto.

Namshukuru Mungu sikuwahi kuulizwa na mtu yeyote si wa upande wangu wala wa mume wangu kwanini hatuzai. Hivyo ninaamini these days jamii imeelimika. Si wote wasiozaa immediately wana matatizo; kuzaa si jambo la mchezo linataka mipango.

Watoto ni wazuri sana na ni wafariji hasa mkiwapata kwa muda muafaka.

 
Kwasababu ya maneno ya nje (ndugu, marafiki, majirani)




Wakuu heshima kwenu!

Lakini mimi nina tofautiana na mitizamo yenu. Suala alilosema Mwanakijiji ni pana sana; hapo suala la upendo wa dhati kwa hao wanandoa lazima ufikiriwe; suala la maamuzi ya wanandoa wenyewe pia lazima lifikiriwe.

Kwanza lazima tujiulize, kuhusu chanzo na msingi wa hao watu kuwa wanandoa. Je, wanapendana kwa dhati? Je, walielewa mafundisho ya ndoa? Maana kama wanapendana kwa dhati, naamini wataweza kukabiliana na changamoto zozote ambazo zitatokea katika maisha yao ya ndoa (ukosefu wa mtoto ikiwa ni mojawapo). Pia mafundisho ya ndoa (kwa dini ya kikristo) yanazungumzia juu ya suala hili; na ukosefu wa mtoto katika ndoa sio suala la kuweza kutengana kwa wanandoa, labda iwe nje ya taratibu za kidini, ambapo husipotengana ndani ya taratibu za kidini na ukamwacha mkeo/mmeo, utakua ukizini unapofanya tendo la ndoa na mwanamke/mwanamume unaeamini mtapata nae mtoto.

Suala la external forces katika ndoa si lakuvumiliwa na kudekezwa hata kidogo. Watu wakishakuwa mume na mke, wanapaswa wasisikilize wala kujali hizo pressure toka nje. Ndio maana wenzetu (watu wa Ulaya na Marekani) hapa wanakua wanatuzidi sana (once they are husband and wife, they don't give a damn about outsiders' gossips). Kwetu sisi waafrika hizi outsiders' gossips zinatuamiza vichwa sana kiasi kwamba ndio sababu ya ndoa nyingi kuvunjika. Sasa tukiweza kuhimili na kuignore hizo pressure toka nje (pamoja na kuzingatia mafundisho ya dini/ndoa) nadhani kesi za kuachana kwa wanandoa kutokana ukosefu wa mtoto zitapungua sana.
 
Wataanzia wapi kuignore maneno ya nje wakati wengine hao hata ndoani wanaingia kutokana na hayo maneno?Huku kwetu maneno ya watu yanaongoza maisha ya wengi. . . na mpaka hilo litakapopungua ndo watu wataanza kujali hisia na matakwa yao wenyewe pale wanapofanya mamb😵therwise tukubali tu kwamba ndoa nyingi zinazovunjika kwa ukosefu wa mtoto/watoto sio kwa mapenzi ya wenye ndoa bali maneno ya wanaowazunguka.
 
Mtoto ni heshima na ndo kitu mtu anategemea zaidi kuliko vyote pindi anapoolewa/kuowa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…