Kwanini kugombea Uenyekiti CHADEMA ni dhambi?

Kwanini kugombea Uenyekiti CHADEMA ni dhambi?

econonist

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
20,189
Reaction score
29,663
Nashangaa sana wazee wa mwanzoni akina Mtei na Makani walifanya uenyekiti wa CHADEMA kama nafasi huru hawakutaka kukaa madarakani mpaka waondolewe kwa nguvu. Kwa Sasa ni CHADEMA imejenga mtindo wa kwamba akitokea kiongozi mwenye ushawishi akagombea uenyekiti wa chama huwa anageukwa na kuitwa msalaiti.

Mifano ni mingi Sana:
1. Kuna chaha wangwe, huyu hadi alisimamishwa chama, kutokana na kuwa na msimamo mkali dhidi ya mwenyekiti na kutaja hadharani angependa awe yeye mwenyekiti wa chama.

2. Kuna Zitto Kabwe naye alipojaribu alizuiliwa na kuitwa majina mengi na hata baadae kuhama chama.

3. Kuna Kansa Mbaruk, alipojaribu alikutana na kigingi mpaka alipohamia ACT.

4. Kuna Sumaye, yeye alipojaribu aliambiwa sumu haionjwi kwa kulamba. Ikabidi arudi CCM alikotokea.

5. Kwa Sasa tunaye Tundu Lissu, yeye kashatangaza kugombea uenyekiti wa CHADEMA na kashachukua na kurejesha fomu ya uenyekiti. Ila amepata mashambulizi mengi Sana. Mara anatumika na CCM , mara anafadhiliwa na CCM akiharibu chama, mara ni kirusi ndani ya CHADEMA etc. Leo Lissu anatukanwa kisa tu kachukua fomu ya uenyekiti. Bila fomu ya uenyekiti Leo hakuna mtu angemsema Lissu vibaya.

Najiuliza swali moja kubwa, je ni dhambi kugombea uenyekiti CHADEMA? Kama ni dhambi iandikwe kwenye Katiba kwamba mpaka Mbowe afe ndipo watu wenye ushawishi kwenye chama watagombea Uenyekiti. Leo Lissu amekuwa shetani kwa kuchukua fomu ya uenyekiti, Leo Lissu anazodolewa na Wana CHADEMA kisa kachukua fomu ya kugombea uenyekiti.

Inasikitisha sana, Kwa chama kama CHADEMA kinahangaika kuutukuza ufalme na kutokupokezana uongozi.

Inasikitisha sana.
 
Mbona hata Mbowe anapitia hayo hayo humu jamvini thread kibao za kumponda. Kama Mbowe anagombea na havunji sheria na taratibu za chama haina shida na Lissu pia, tuache box la kura liamue.
 
Nashangaa sana wazee wa mwanzoni akina Mtei na Makani walifanya uenyekiti wa CHADEMA kama nafasi huru hawakutaka kukaa madarakani mpaka waondolewe kwa nguvu....
sio dhambi hata kidogo gentleman,

ila kukurupuka kwa pupa, uchu wa cheo, tamaa ya madaraka, mdomo na makelele mengi ndilo haswaa tatizo, hususan kwa miongoni mwa wagombea wa uongozi wa nafasi mbalimbali chadema, ambao ni wazi watajiengua mapema kabla ya uchaguzi :BASED:
 
Mbona hata Mbowe anapitia hayo hayo humu jamvini thread kibao za kumponda. Kama Mbowe anagombea na havunji sheria na taratibu za chama haina shida na Lissu pia, tuache box la kura liamue.

Issue sio kugombea. Issue ni kwamba miaka yote anapotokea mtu mwenye influence kutaka uenyekiti, huwa anageuziwa Kibao. Fuatilia kuanzia chaha wangwe Hadi Zitto Kabwe mpaka Lissu. Kwa Sasa watu wanatumia common reasoning dhidi ya Mbowe kitu ambacho huko nyuma hakikuwepo.
 
Sio dhambi hata Mbowe akiendelea kuongoza
 
Issue sio kugombea. Issue ni kwamba miaka yote anapotokea mtu mwenye influence kutaka uenyekiti, huwa anageuziwa Kibao. Fuatilia kuanzia chaha wangwe Hadi Zitto Kabwe mpaka Lissu. Kwa Sasa watu wanatumia common reasoning dhidi ya Mbowe kitu ambacho huko nyuma hakikuwepo.
Nakubaliana nawe. Lakini naona mambo ni fair Lissu kachukua fomu hajazuiwa, ni mapema mno wafuasi na wapenzi wa Lissu kuwa katika panic mode.
 
Issue sio kugombea. Issue ni kwamba miaka yote anapotokea mtu mwenye influence kutaka uenyekiti, huwa anageuziwa Kibao. Fuatilia kuanzia chaha wangwe Hadi Zitto Kabwe mpaka Lissu. Kwa Sasa watu wanatumia common reasoning dhidi ya Mbowe kitu ambacho huko nyuma hakikuwepo.
Mbowe kaigeuza chadema kuwa mradi wake
 
Mbona hata Mbowe anapitia hayo hayo humu jamvini thread kibao za kumponda. Kama Mbowe anagombea na havunji sheria na taratibu za chama haina shida na Lissu pia, tuache box la kura liamue.
Mbowe ndiyo kansa ya demokrasia.
 
Nashangaa sana wazee wa mwanzoni akina Mtei na Makani walifanya uenyekiti wa CHADEMA kama nafasi huru hawakutaka kukaa madarakani mpaka waondolewe kwa nguvu. Kwa Sasa ni CHADEMA imejenga mtindo wa kwamba akitokea kiongozi mwenye ushawishi akagombea uenyekiti wa chama huwa anageukwa na kuitwa msalaiti.

Mifano ni mingi Sana:
1. Kuna chaha wangwe, huyu hadi alisimamishwa chama, kutokana na kuwa na msimamo mkali dhidi ya mwenyekiti na kutaja hadharani angependa awe yeye mwenyekiti wa chama.

2. Kuna Zitto Kabwe naye alipojaribu alizuiliwa na kuitwa majina mengi na hata baadae kuhama chama.

3. Kuna Kansa Mbaruk, alipojaribu alikutana na kigingi mpaka alipohamia ACT.

4. Kuna Sumaye, yeye alipojaribu aliambiwa sumu haionjwi kwa kulamba. Ikabidi arudi CCM alikotokea.

5. Kwa Sasa tunaye Tundu Lissu, yeye kashatangaza kugombea uenyekiti wa CHADEMA na kashachukua na kurejesha fomu ya uenyekiti. Ila amepata mashambulizi mengi Sana. Mara anatumika na CCM , mara anafadhiliwa na CCM akiharibu chama, mara ni kirusi ndani ya CHADEMA etc. Leo Lissu anatukanwa kisa tu kachukua fomu ya uenyekiti. Bila fomu ya uenyekiti Leo hakuna mtu angemsema Lissu vibaya.

Najiuliza swali moja kubwa, je ni dhambi kugombea uenyekiti CHADEMA? Kama ni dhambi iandikwe kwenye Katiba kwamba mpaka Mbowe afe ndipo watu wenye ushawishi kwenye chama watagombea Uenyekiti. Leo Lissu amekuwa shetani kwa kuchukua fomu ya uenyekiti, Leo Lissu anazodolewa na Wana CHADEMA kisa kachukua fomu ya kugombea uenyekiti.

Inasikitisha sana, Kwa chama kama CHADEMA kinahangaika kuutukuza ufalme na kutokupokezana uongozi.

Inasikitisha sana.
Kwa mujibu wa mbogamboga ni dhambi
 
Nashangaa sana wazee wa mwanzoni akina Mtei na Makani walifanya uenyekiti wa CHADEMA kama nafasi huru hawakutaka kukaa madarakani mpaka waondolewe kwa nguvu. Kwa Sasa ni CHADEMA imejenga mtindo wa kwamba akitokea kiongozi mwenye ushawishi akagombea uenyekiti wa chama huwa anageukwa na kuitwa msalaiti.

Mifano ni mingi Sana:
1. Kuna chaha wangwe, huyu hadi alisimamishwa chama, kutokana na kuwa na msimamo mkali dhidi ya mwenyekiti na kutaja hadharani angependa awe yeye mwenyekiti wa chama.

2. Kuna Zitto Kabwe naye alipojaribu alizuiliwa na kuitwa majina mengi na hata baadae kuhama chama.

3. Kuna Kansa Mbaruk, alipojaribu alikutana na kigingi mpaka alipohamia ACT.

4. Kuna Sumaye, yeye alipojaribu aliambiwa sumu haionjwi kwa kulamba. Ikabidi arudi CCM alikotokea.

5. Kwa Sasa tunaye Tundu Lissu, yeye kashatangaza kugombea uenyekiti wa CHADEMA na kashachukua na kurejesha fomu ya uenyekiti. Ila amepata mashambulizi mengi Sana. Mara anatumika na CCM , mara anafadhiliwa na CCM akiharibu chama, mara ni kirusi ndani ya CHADEMA etc. Leo Lissu anatukanwa kisa tu kachukua fomu ya uenyekiti. Bila fomu ya uenyekiti Leo hakuna mtu angemsema Lissu vibaya.

Najiuliza swali moja kubwa, je ni dhambi kugombea uenyekiti CHADEMA? Kama ni dhambi iandikwe kwenye Katiba kwamba mpaka Mbowe afe ndipo watu wenye ushawishi kwenye chama watagombea Uenyekiti. Leo Lissu amekuwa shetani kwa kuchukua fomu ya uenyekiti, Leo Lissu anazodolewa na Wana CHADEMA kisa kachukua fomu ya kugombea uenyekiti.

Inasikitisha sana, Kwa chama kama CHADEMA kinahangaika kuutukuza ufalme na kutokupokezana uongozi.

Inasikitisha sana.
Unakaribishwa kugombea na wewe mkuu kama alifanya Lissu na wengine.
 
Back
Top Bottom