Kwanini kujiendeleza kwa walimu hukuleti tija ya kuinua ubora na kiwango cha elimu?

Kwanini kujiendeleza kwa walimu hukuleti tija ya kuinua ubora na kiwango cha elimu?

Mbogi

JF-Expert Member
Joined
Oct 10, 2021
Posts
803
Reaction score
997
1. Nianze hoja kwa kuomba wahusika na wadau wa idara, kurugenzi na wizara wafanye uchunguzi ili wajiridhishe na kuthibitisha uhalisia wa swali hili.

2. Lengo la serikali kuwapa watumishi wake fursa ya kujiendeleza kimasomo (mafunzo kazini) ni kuweza kuongeza ufanisi katika utendaji kazi kwa watumishi na hatimaye kuleta tija stahiki kwa serikali na umma kuwa ujumla.

3. Pamoja na malengo hayo tumeshuhudia mara nyingi na kwa wingi walimu wengi wakipata fursa ya kujiendeleza na hivi sasa yawezekana kuwa tunao walimu wengi hasa wa shule ya msingi walio na kiwango cha shahada na kwa takribani karibu walimu wote Wana kiwango cha stashahada.

3. Hoja ni ipi? Mwalimu anapokwenda masomoni kwa maana ya mafunzo kazini ni matarajio makubwa kuwa akirudi atakuwa na mbinu mpya za kiutendaji Katika kile alichokwenda kuongeza ujuzi ila kwa sasa imekuwa kinyume chake, maana akirudi hata zile mbinu zake za awali anakuwa amezisahau na pengine hata ujuzi anaorudi nao unakuwa hauna nafasi katika kazi yake ya msingi, na hili hutokea Sana kwa walimu wa shule ya msingi.

4. Maoni yangu ni kwamba kuna haja ya kupitia aina ya mafunzo yanayolenga mafunzo kazini ili yalenge kuboresha mbinu na kuongeza ujuzi wa juu na ulio bora wa somo lilelile alilokuwa akifundisha kuliko kufundishwa kozi ambazo pengine ni mpya na haziwezi kutumika katika kazi yake.

5. Hapo nyuma tuliona kilianzishwa chuo cha stashahada ya ualimu kwa shule za msingi, kwa muda mfupi nilioshuhudia wahitimu wake walikuwa wameongeza kitu kipya na bora kilichoweza kutumika katika masomo yao.

Ni vizuri wangeweza kuboresha zaidi kuliko kuifuta stashahada hiyo na kulazimisha kila mwalimu awe na stashahada ya sekondari.

Ni kweli kwa sasa walimu karibu wote Wana stashahada ya sekondari lakini matumizi yake ni sawa na bure.

Karibuni kwa mjadala.
 
1. Nianze hoja kwa kuomba wahusika na wadau wa idara, kurugenzi na wizara wafanye uchunguzi ili wajiridhishe na kuthibitisha uhalisia wa swali hili.

2. Lengo la serikali kuwapa watumishi wake fursa ya kujiendeleza kimasomo (mafunzo kazini) ni kuweza kuongeza ufanisi katika utendaji kazi kwa watumishi na hatimaye kuleta tija stahiki kwa serikali na umma kuwa ujumla.

3. Pamoja na malengo hayo tumeshuhudia mara nyingi na kwa wingi walimu wengi wakipata fursa ya kujiendeleza na hivi sasa yawezekana kuwa tunao walimu wengi hasa wa shule ya msingi walio na kiwango cha shahada na kwa takribani karibu walimu wote Wana kiwango cha stashahada.

3. Hoja ni ipi? Mwalimu anapokwenda masomoni kwa maana ya mafunzo kazini ni matarajio makubwa kuwa akirudi atakuwa na mbinu mpya za kiutendaji Katika kile alichokwenda kuongeza ujuzi ila kwa sasa imekuwa kinyume chake, maana akirudi hata zile mbinu zake za awali anakuwa amezisahau na pengine hata ujuzi anaorudi nao unakuwa hauna nafasi katika kazi yake ya msingi, na hili hutokea Sana kwa walimu wa shule ya msingi.

4. Maoni yangu ni kwamba kuna haja ya kupitia aina ya mafunzo yanayolenga mafunzo kazini ili yalenge kuboresha mbinu na kuongeza ujuzi wa juu na ulio bora wa somo lilelile alilokuwa akifundisha kuliko kufundishwa kozi ambazo pengine ni mpya na haziwezi kutumika katika kazi yake.

5. Hapo nyuma tuliona kilianzishwa chuo cha stashahada ya ualimu kwa shule za msingi, kwa muda mfupi nilioshuhudia wahitimu wake walikuwa wameongeza kitu kipya na bora kilichoweza kutumika katika masomo yao.

Ni vizuri wangeweza kuboresha zaidi kuliko kuifuta stashahada hiyo na kulazimisha kila mwalimu awe na stashahada ya sekondari.

Ni kweli kwa sasa walimu karibu wote Wana stashahada ya sekondari lakini matumizi yake ni sawa na bure.

Karibuni kwa mjadala.
None Sense [emoji24][emoji24][emoji24]
 
Mkuu uliyoyaandika ungeweka na ushahidi yangesaidia kueleweka zaidi ila hata hivyo bado umeonesha hisia zako tu na siyo nguvu ya hoja
 
Mkuu uliyoyaandia ungeweka na ushahidi yangesaidia kueleweka zaidi ila hats hivyo bado umeonesha hisia zako tu na siyo nguvu ya hoja
Ndugu victor kama wewe ni mdau wa elimu sidhani kama utahitaji ushahidi maana upo wazi kabisa,

1. Ushahidi upo katika matokeo ya wanafunzi hasa kwa shule za serikali. Tulitegemea kuwa kadri walimu wanavyojifua ktk kozi ndivyo matokeo yangekuwa mazuri zaidi. Hapa fuatilia utaona.

2. Fuatilia maudhui ya mtaala wanaosoma ukihusianisha na matumizi yake ktk kazi zao lakini pia fuatilia kwa walimu wakuu wakupe ukweli wa walimu wengi wanaotoka kujifua kwamba wanaongeza tija kiasi gani ktk kupata matokeo tarajiwa.

3. Lengo la uzi huu ni kuwapa hoja ya kufanyia ufuatiliaji ili kujiridhisha na kama kuna walakini kuwe na marekebisho, ila kama wewe umeamua kuhukumu bila kufuatilia sitashangaa maana elimu yetu imekuwa dhaifu kutokana na waliopewa dhamana kuziba masikio kusikiliza maoni ya walioko ktk utekekezaji.
 
Lengo la kujielimisha halipimwi Kwa kigezo kimoja cha matokeo ya wanafunzi Mkuu, matokeo kuwa mazuri au mabaya yanasababishwa na intervening variables lukuki....Broh
 
Lengo la kujielimisha halipimwi Kwa kigezo kimoja cha matokeo ya wanafunzi Mkuu, matokeo kuwa mazuri au mabaya yanasababishwa na intervening variables lukuki....Broh
Suala la kujielimisha lipo, ni tofauti na hili la walimu.
Mfano Mwl anapokwenda kusoma ugavi hapa tunaita kujielimisha maana serikali haitatambua ujuzi huo hadi atakapohama idara.

Tukisema kujiendeleza/ kujifua (mafunzo kazini) maana yake ni kwamba unaenda kuongeza mbinu mpya za ufanisi na kuongeza tija ktk kazi yako. Mfano daktari akienda kujiendeleza anarudi akiwa na ziada au bingwa ktk kazi yake vivyo hivyo ktk kada nyingine na ufanisi huonekana.

Unaposema ufaulu inategemea mambo mengi ni kweli lakini ukubali kuwa anayepaswa kuratibu mambo yote hayo ni mwalimu maana ndiye anaye paswa kuwa mbunifu kulingana na changamoto anazokabiliana nazo na hapa ndipo mafunzo yenye maudhui sahihi ya kukabiliana na changamoto kazini yanapo hitajika na kuleta tija.
 
Suala la kujielimisha lipo, ni tofauti na hili la walimu.
Mfano Mwl anapokwenda kusoma ugavi hapa tunaita kujielimisha maana serikali haitatambua ujuzi huo hadi atakapohama idara.

Tukisema kujiendeleza/ kujifua (mafunzo kazini) maana yake ni kwamba unaenda kuongeza mbinu mpya za ufanisi na kuongeza tija ktk kazi yako. Mfano daktari akienda kujiendeleza anarudi akiwa na ziada au bingwa ktk kazi yake vivyo hivyo ktk kada nyingine na ufanisi huonekana.

Unaposema ufaulu inategemea mambo mengi ni kweli lakini ukubali kuwa anayepaswa kuratibu mambo yote hayo ni mwalimu maana ndiye anaye paswa kuwa mbunifu kulingana na changamoto anazokabiliana nazo na hapa ndipo mafunzo yenye maudhui sahihi ya kukabiliana na changamoto kazini yanapo hitajika na kuleta tija.
Suala linaloitwa elimu linahitaji collective effort and accountability......elimu ni mali na amali ya jamii. Lazima kila upande uwajibike kwenye hili Mkuu. Mwalimu kuwajibishwa peke yake siyo sawa hata kidogo
 
Back
Top Bottom