Kwanini kuna mgawanyiko katika Ligi ya Premia kuhusu uungaji mkono wa kampeni ya wapenzi wa jinsi moja?
Uamuzi wa nahodha wa Ipswich Town Sam Morsy wa kutovaa jezi ya upinde wa mvua kuunga mkono kampeni ya kuunga mkono haki za wapenzi wa jinsi moja na jamii ya LGBTQ+ ya Rainbow Laces ya Ligi kuu ya England umezua mjadala.
Morsy alivaa jezi ya kiwango cha juu badala ya muundo wa upinde wa mvua wakati waliposhindwa 1-0 na Nottingham Forest Jumamosi kwa "imani za kidini" MUISLAMU, kulingana na klabu yake Ipswich.
Alifanya hivyo katika mechi ya Ipswich dhidi ya Crystal Palace Jumanne usiku.
Je, ni nini sababu za uamuzi - na majibu yamekuwa ni yapi?
Je, Kampeni ya Rainbow Laces ni nini? Ligi Kuu hushirikiana na watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsi moja na LGBTQ + kwa ujumla na hisani ya Stonewall kwenye kampeni ya Rainbow Laces (nembo ya wapenzi wa jinsi moja na LGBTQ+) kila msimu.
Mpango huo unahusisha wachezaji wa juu wenye hadhi ya juu kuhimizwa kuvaa alama za rangi ya upinde wa mvua na mikono ya nahodha kuonyesha uungaji mkono kwa haki za watu wa LGBTQ +, kuhamasisha kukubalika miongoni mwa watoto na vijana, na kukuza usawa na utofauti.
Nembo hiyo ya Rainbow Laces ilizinduliwa kwa mara ya kwanza mwaka 2013, na kwa kawaida hudumu kwa wiki moja na imekuwa ikiungwa mkono na vilabu vyote na idadi kubwa ya manahodha wa Ligi Kuu tangu wakati huo.
Uamuzi wa nahodha wa Ipswich Town Sam Morsy wa kutovaa jezi ya upinde wa mvua kuunga mkono kampeni ya kuunga mkono haki za wapenzi wa jinsi moja na jamii ya LGBTQ+ ya Rainbow Laces ya Ligi kuu ya England umezua mjadala.
Morsy alivaa jezi ya kiwango cha juu badala ya muundo wa upinde wa mvua wakati waliposhindwa 1-0 na Nottingham Forest Jumamosi kwa "imani za kidini" MUISLAMU, kulingana na klabu yake Ipswich.
Alifanya hivyo katika mechi ya Ipswich dhidi ya Crystal Palace Jumanne usiku.
Je, ni nini sababu za uamuzi - na majibu yamekuwa ni yapi?
Je, Kampeni ya Rainbow Laces ni nini? Ligi Kuu hushirikiana na watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsi moja na LGBTQ + kwa ujumla na hisani ya Stonewall kwenye kampeni ya Rainbow Laces (nembo ya wapenzi wa jinsi moja na LGBTQ+) kila msimu.
Mpango huo unahusisha wachezaji wa juu wenye hadhi ya juu kuhimizwa kuvaa alama za rangi ya upinde wa mvua na mikono ya nahodha kuonyesha uungaji mkono kwa haki za watu wa LGBTQ +, kuhamasisha kukubalika miongoni mwa watoto na vijana, na kukuza usawa na utofauti.
Nembo hiyo ya Rainbow Laces ilizinduliwa kwa mara ya kwanza mwaka 2013, na kwa kawaida hudumu kwa wiki moja na imekuwa ikiungwa mkono na vilabu vyote na idadi kubwa ya manahodha wa Ligi Kuu tangu wakati huo.