Kwanini kutoa msaada ni ibada

Kwanini kutoa msaada ni ibada

matunduizi

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2018
Posts
7,968
Reaction score
19,368
Watu wa dini, wasioamini Mungu, freemasons kupitia charity zao, wote wanaunganishwa katika jambo moja la kutoa msaada kwa watu wenye shida.

Kutoa kwa kusukumwa na huruma kwa mwanadamu mwenzako ni ibada kamili iliyokamilika. Hii kazi ilipaswa kufanywa na Mungu mwenyewe aliyemuumba huyo mtu, wewe kuingilia kati ni kuamua kishirikiana na Mungu kufanya jambo la kiungu.

Kutoa msaada kwa kusukumwa na sifa binafsi, kupata umaarufu au kuwapiga chenga watu kuficha uovu wako kwa kuhamisha malengo ni ibada binafsi ambazo anayeabudiwa hapo ni wewe na waliokusukuma qu kinachokusukuma kufanya hivyo.

Ufanye nini sasa.
Hakikisha unatoa msaada ukisukumwa na huruma bila kuwa na nia kificho au faida binafsi katika msaada huo. Hiyo ni ibada kwa Mungu na atakufanya kuwa mfereji wa kupitishia utajiri wake ili watu wengi wanufaike.

Ni hilo tu
 
Wewe pokea msaada, mengine siyo kazi yako hayakuhusu.

Angalia msaada wanaotowa Freemason kupitia Lions club na Rotary club halafu fananisha na makanisa na misikiti wanatowa nini zaidi ya kuwakamuwa waumini?
 
Wewe pokea msaada, mengine siyo kazi yako hayakuhusu.

Angalia msaada wanaotowa Freemason kupitia Lions club na Rotary club halafu fananisha na makanisa na misikiti wanatowa nini zaidi ya kuwakamuwa waumini?
Yap freemasons wanajitahidi kuchimba visima vijijini etc, nakumbuka kuna mahali mmoja alitaka kuchangia ujenzi wa kanisa kwa sharti la kuweka tu jiwe la msingi ila anajenga lote wajumbe wakabishana mbabe ikabidi ale kona.

Kuhusu kupokea msaada mkuu mpokeaji hana ishu, ishu ya ibada ni kwa mtoaji. Maana ibada ni kutoa sio kupokea. Hii ni kanuni ya Mungu. Kama hakuna kutoa hakuna ibada. Nadhani ndio maana hata hao freemasons na clubs zao wamejikita kwenye kutoa zaidi.
 
Back
Top Bottom