Ninajaribu kufikiri kipi chaweza msaidia mtanzania kujitunzia akiwa, ikikumbukwa kuwa ni jamii ambayo haikuwa na utamaduni huo. Kama unaweza kutoa pesa M-Power kama vile unavyoweza kutoa M-Pesa, siioni ikimsaidia asiye na desturi ya kuweka, maana atazitoa tena akipata dharura au akiwa kwenye starehe. Bora wangeweka option ya kuzifungia pesa zako, mfano kwa mwezi, miezi miwili, mitatu nk. Ili kwa kipindi hicho uweze kuweka lakini huwezi kuzitoa mpaka muda ufike. Ikimsaidia mtu kuona umuhimu wake, na kumfunza kuvumilia ili aongezeke.