mkuu madhumuni ya bima ya afya ni tofauti na bima ya mkopo... hii mikopo pamoja na kwamba wanakata bima pia kuna dhamana... mbna stanbic kenya walinirudishia, why hizi bank zetu za ndani hazirudishi?Bima hairudishwi mkuu, tafasiri nyepesi ni kuwa wakati wewe umerejesha mkopo smooth, kuna mwingine hakurejesha kabisa labda kafariki, kwa hiyo kiasi ulichotoa wewe na mwingine na mwingine kama bima kinaenda kufidia deni la yule ambaye hakurejesha kwa sababu hizo. Mfano bima ya afya, usipougua wewe katika kipindi hicho cha bima haina maana kuwa pesa yako utarudishiwa, kwani kuna mwingine kanufaika kupitia pesa yako ( kwa kupata matibabu zaidi ya kile alichochangia katika bima yake.
Swali: Kama usingemaliza mkopo, je unafikiri kile kiasi ulichokatwa kama bima kingetosha kulipia mkopo uliobakiza?? Je? Kama hakitoshi fedha nyingine inatoka wapi kulipia deni lako?Mi nimemaliza mkopo iwaje nilipe fidia ya wengine bado jibu halijakaa sawa
Ninachofahamu mimi ni kuwa dhamana haitachukuliwa endapo mkopaji kashindwa kurejesha mkopo kutokana na sababu zilizoainishwa labda kifo, ulemavu wa kudumu nk. Hapo ndo bima inachukua nafasi ya kulipia deni. Yaani mfano mtu kafariki, kaweka nyumba kama dhamana, hiyo nyumba haitachukuliwa na kuuzwa na taasisi ya fedha kisa marehemu hakumaliza kulipa mkopo wake.ndio maana kuna dhamana mkuu, nadhani unaelewa
sidhani kama hii itakuwa logic otherwise bank wanatumia kichaka hiki kupiga pesa ndani ya ukopaji kwa kisingizio cha bima ya mikopoNinachofahamu mimi ni kuwa dhamana haitachukuliwa endapo mkopaji kashindwa kurejesha mkopo kutokana na sababu zilizoainishwa labda kifo, ulemavu wa kudumu nk. Hapo ndo bima inachukua nafasi ya kulipia deni. Yaani mfano mtu kafariki, kaweka nyumba kama dhamana, hiyo nyumba haitachukuliwa na kuuzwa na taasisi ya fedha kisa marehemu hakumaliza kulipa mkopo wake.
Bima hairudishwi mkuu, tafasiri nyepesi ni kuwa wakati wewe umerejesha mkopo smooth, kuna mwingine hakurejesha kabisa labda kafariki, kwa hiyo kiasi ulichotoa wewe na mwingine na mwingine kama bima kinaenda kufidia deni la yule ambaye hakurejesha kwa sababu hizo. Mfano bima ya afya, usipougua wewe katika kipindi hicho cha bima haina maana kuwa pesa yako utarudishiwa, kwani kuna mwingine kanufaika kupitia pesa yako ( kwa kupata matibabu zaidi ya kile alichochangia katika bima yake.
mkuu kuna vitu unachanganya bima ya gari ni tofauti kabisa na hii na hata ulipaji wake, hii bima wanakata bank na makubaliano ni ya maneno hakuna documentation inayoonesha umelipia... mkopo wako ukitoka wao wanakata moja kwa moja kinachoitwa bima ya mkopo kwenye huo mkopo wako, hapa ina maana hii pesa inarudi kwao bank wenyewe na haiendi kwa kampuni wala taasisi za bimaVipi unapolipia bima ya gari, na gari isipopata ajali unarudishiwa pesa uliyolipia?!
Una uhakika kuwa hio hela haiendi kwenye taasisi za bima?mkuu kuna vitu unachanganya bima ya gari ni tofauti kabisa na hii na hata ulipaji wake, hii bima wanakata bank na makubaliano ni ya maneno hakuna documentation inayoonesha umelipia... mkopo wako ukitoka wao wanakata moja kwa moja kinachoitwa bima ya mkopo kwenye huo mkopo wako, hapa ina maana hii pesa inarudi kwao bank wenyewe na haiendi kwa kampuni wala taasisi za bima
Hiyo ni bima sio dhamana mkuu, kwani bima ya gari usipopata ajali unarudishiwa?Habari zenu wanajamvi
Miaka sita (6) iliyopita nilichukua mkopo bank ya CRDB kwa dhamana ya utumishi na marejesho yakiwa yanakatwa moja kwa moja kwenye mshahara, moja ya masharti ya ule mkopo ilikuwa ni lazma ukatiwe bima dhidi ya kifo au ulemavu wa kudumu, maafisa mikopo wa CRDB walinielimisha vizuri sana kuhusu hii bima amabayo wanaikata kwenye kile kiasi ulichoomba mkopo, nadhani ni kama 200k+ kama sikosei.wakanielieza kwamba
Kile kiasi cha pesa kilichokatwa kwenye mkopo nilioomba kama Bima kinasimamia upotevu wa fedha,mali iliyokatiwa Bima kutokana na kutokuwepo kwa uaminifu kutoka kwa waajiri wakati wafanyakazi wakiwa kazini. Bima hii pia inasimamia usalama wamali iliyochukuliwa kama dhamana. Wakaendelea kusema,
Bima hiyo inalipia hasara ya fedha anayoipata mkopeshaji ( ambao ni wao CRDB Bank) kutokana na matatizo aliyopata mdeni kufuatia majanga ya kifo au ulemavu wa kudumu kabla hajamaliza kulipa deni. Husaidia kupunguza hasara ikilinganishwa na dhamana iliyowekwa. Kwa wakopaji wasio na dhamana za kazi Bima hii ina hakikisha familia ya mhanga haiachwi bila makazi au mzigo wa kuendelea kulipia deni linalodaiwa pale mkopaji anapofariki au kupata ulemavu wa kudumu.
HOJA YANGU
Deni langu lilikuwa la miaka mitano (5) na mwaka jana nilimalizana na hili deni, yaani hawanidai tena tangu mwaka jana, nilitegemea baada ya deni kumalizika hawa CRDB bank wanirudishie ile pesa yangu Zaidi ya 200K kwa vile mkopo wao tayari nimeurudisha wote pamoja na riba na bila usumbufu, mwanzoni mwa mwaka huu niliwatumia barua kuwakumbusha kuhusu kunirejeshea hii pesa hawajanijibu hadi leo, jana nimewatumia email kupitia kwa DG wao bado pia naona kimya.
Hii kitu imeekaaje kwa hapa bongo, au ndo bank inadhulumu wateja wao…, nakumbuka nilikopaga pesa stanbic bank nikiwa Kenya kwa mda wa mwaka mmoja na baada ya mkopo kuisha nikarejesehewa hii pesa tena wakani email kabisa kunitaarifu.
Najua wakopaji kwenye hizi taasisi za kifedha wako wengi na najua na wao hawajui kama wanatakiwa kurudishiwa hii pesa baada ya mikopo kumalizika , naombeni kujulishwa kama hapa bongo hii pesa huwa hairudi hata kama deni lao umemaliza lote?
Mkuu acha roho ya kwa nini, hivi uko serious kufananisha bond ya Simu na BIMA? Hivi hiyo 200k ndio Iwe bond ya 10m ulizovuta? Hivi uonagi wenzako bond zao huweka nyumba na Mali nyingine zenye thamani zaidi ya kile walichopewa?hivi mkuu nikiweka bond simu kwako ukanipa 120K kwa makubaliano nikilipa deni lako na riba uliyonipa unirudishie simu yangu, nikimaliza deni utakatalia simu yangu?
Akili yako kama yangu mkuu, umekata bima ya gari baada ya miaka 5 unaliuza kwa mtu mwingine ana unaachana na mambo ya magari au chombo chochote cha moto, vp hapo mleta mada unataka bima wakulipe hela yako hiyo.?Sizani kama ni rahisi kurudishiwa bima ya mkopo kwa sababu hata wao benki hiyo hela wanayokukata kama bima wanaenda kuilipa kwenye kampuni ya bima na hawabaki nayo kama faida.
Mfano mzuri umekata bima ya gari lako hauwezi kwenda kudai kwa sababu eti gari lako halijapata ajali katika huo mwaka husika ambao umekata bima.
mkuu roho ipi ya kwa nini? hiyo 200K sio ndogo ingekuwa ndogo wasingechukua..., stanbic bank branch ya kenya wao mbona walinirudishia mkuu...na kumbuka hao wanaoweka bond nyumba lakini pia wanakatwa hii bima kwenye mikopo wanayochukua sasa why wasirudishiwe pesa yao wanapomaliza deni laoMkuu acha roho ya kwa nini, hivi uko serious kufananisha bond ya Simu na BIMA? Hivi hiyo 200k ndio Iwe bond ya 10m ulizovuta? Hivi uonagi wenzako bond zao huweka nyumba na Mali nyingine zenye thamani zaidi ya kile walichopewa?
Tatizo kubwa watu hatupendi kusoma maandishi mengi, BIMA ni moja ya sharti la kupewa kwako mkopo, na ungesoma kabla ungeelewa vizuri ila kwa sababu ulikuwa na hamu ya manoti muda huo hukujali. Nadhani ndio maana wenzako hawakujibu simply they know your fault.
wabongo tunapigwa sana maana hatutaki kufuatilia vitu, hawa wajinga wanatupiga sana pesa kwa sisi kutotaka kujua vituAkili yako kama yangu mkuu, umekata bima ya gari baada ya miaka 5 unaliuza kwa mtu mwingine ana unaachana na mambo ya magari au chombo chochote cha moto, vp hapo mleta mada unataka bima wakulipe hela yako hiyo.?
sasa hawa si ra di bi hawakunipa na sidhani kama wanawapa wateja wao hii cover note, wao wanakata juu kwa juu tu unapewa maelezoNiliwahi chukua mkopo toka benki moja (jina kapuni) na marejesho yake yalikuwa ni miaka mitatu. Baada ya mwaka mmoja, mwajiri akasitisha mkataba hivyo nikawa sina uwezo wa kulipa mkopo. Benki wakaja juu wanataka hela yao, tukakaa mezani nami nikawaambia sina kazi ya kunipa kipato cha kurejesha mkopo. Hatukuelewana, wakampa debt collector kazi ya kunidai.
Uzuri wake waliponipa mkopo walinipa na cover note ya insurance, nikampa huyo debt collector wao, nakala ya insurance cover note na barua yangu ya kuvunjwa mkataba wa kazi, nikamuomba tuonane mahakamani. Sikuwaona tena.
Ushauri wa bure: Wakikukata bima ya mkopo, dai insurance cover note, likitokea la kutokea, wao wakapambane na kampuni ya bima. ILA mkopo ukiisha kwa musjibu wa mkataba, bima ya mkopo HAIRUDISHWI kwako mteja.
Mkuu ni wajibu wako kuwadai wakupe, kwani mlipaji wa hiyo bima ni wewe!sasa hawa si ra di bi hawakunipa na sidhani kama wanawapa wateja wao hii cover note, wao wanakata juu kwa juu tu unapewa maelezo